MAISHA YA MUKRISTO
Yehova Amepanga Watu Wake ili Kuhubiria Watu Wote
Zamani, Yehova alipanga Waisraeli. Ni vile pia anapanga watu wake leo, juu wafanye mapenzi yake. Mu dunia yote, biro za tawi, mizunguko, makutaniko, na vikundi vya mahubiri vinatumika pamoja ili habari njema ihubiriwe. Tunahubiria watu wote, kutia ndani wale wenye wanasemaka luga ingine.—Ufu 14:6, 7.
Ulishakafikiria kujifunza luga ingine juu uitumie ili kusaidia mutu mwingine ajifunze kweli? Hata kama hauna wakati mingi ya kujifunza luga ingine, unaweza kutumia JW Language juu ya kujifunza njia fulani za mwepesi kuhusu namna ya kuanzisha mazungumuzo. Wakristo wa wakati wa mitume walifurahi sana wakati watu wa mu inchi zingine walisikia “mambo makubwa ya Mungu” mu luga yao. Na weye unaweza kuwa na furaha sana kama unatumia JW Language kwa ajili ya mahubiri.—Mdo 2:7-11.
MUANGALIE VIDEO UKUWE RAFIKI YA YEHOVA—UHUBIRI KATIKA LUGA INGINE, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Ni wakati gani unaweza kutumikisha JW Language?
Taja sehemu fulani za JW Language
Ni lazima watu wakila luga wasikie habari njema
Fasi kwenye unaishi, watu wanasemaka luga gani?
Unaweza kufanya nini kama unakuta mutu mwenye anapendezwa na ujumbe wa Ufalme, lakini mwenye anasemaka luga ingine?—od uku. 94-95 fu. 39-41