Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mwezi wa 11 uku. 8
  • Kuungana Mukono ili Kuhubiri mu Eneo Yenye Watu Wanazungumuza Luga Mingi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuungana Mukono ili Kuhubiri mu Eneo Yenye Watu Wanazungumuza Luga Mingi
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ikiwa Msikilizaji Wako Anazungumza Luga Nyingine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Njia Mbalimbali za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuhubiri Mutu Mwenye Kuzungumuza Luga Ingine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Yehova Amepanga Watu Wake ili Kuhubiria Watu Wote
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
mwb18 Mwezi wa 11 uku. 8

MAISHA YA MUKRISTO

Kuungana Mukono ili Kuhubiri mu Eneo Yenye Watu Wanazungumuza Luga Mingi

Ndugu na bibi yake wako mu mahubiri; wanakutana na mwanaume fulani na mutoto yake wenye wanazungumuza luga ingine

Kwa kawaida watu wanaitika ujumbe wa Ufalme wakati wanausikia mu luga yao ya kizalikio. Pengine, ndiyo sababu, ku Pentekoste ya mwaka wa 33, Yehova alikamata mipango ili “Wayahudi wenye kumuogopa Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu” wasikie habari njema, kila mumoja mu “luga yake mwenyewe ya kizalikio,” hata kama inawezekana walikuwa wanazungumuza luga ya watu wote, kama vile Kiebrania ao Kigiriki. (Mdo 2:5, 8) Leo, mu maeneo yenye watu wanazungumuza luga mingi, makutaniko yenye inafanya mikutano mu luga mbalimbali inaweza kuhubiri mu eneo ile ile. Namna gani wahubiri wa ile maeneo wanaweza kuungana mukono ili kuhubiria kila mutu bila kuvuruga wakaaji?

  • telefone

    Muzungumuze (Mez 15:22): Waangalizi wa utumishi wanapaswa kukutana ili kuzungumuzia na kupanga namna ya kuhubiri yenye itakuwa muzuri zaidi kwa makutaniko yote. Kama kutaniko lenye halihubiri mu luga ya kutaniko lenu liko na eneo la kidogo, linaweza kuwaomba musihubiri nyumba za watu wenye kusema luga ya kutaniko lao. Lakini, kama eneo ni ya mukubwa na wako na matatizo ya kuihubiria kwa ukawaida, wanaweza kuwaomba muhubiri nyumba zote, lakini muwaambie kwenye mutu wa luga yao alipendezwa. (od uku. 93 fu. 37) Ao wanaweza kuomba kutaniko lenu liwasaidie kupata watu wenye kuzungumuza luga ya kutaniko lao na kuandika adrese za wale watu na kuwatumia. (km 7/12 uku. 5, kisanduku) Musisahau kama, wakati fulani, mu nyumba moja munaweza kuwa watu wenye kuzungumuza luga mbalimbali. Mipango yenye mutakamata juu ya kuomba watu adrese zao, inapaswa kupatana na sheria ya inchi yenu.

  • Nyumba za mu eneo

    Musaidiane (Efe 4:16): Mufuate kwa uangalifu kila mwongozo yenye mwangalizi wa utumishi anawatolea. Je, uko na funzo ya mutu mwenye anaelewa muzuri luga yenye haiko ya kutaniko lako? Ile funzo inaweza kufanya maendeleo mbio-mbio kama unaipatia ndugu ao dada wa kutaniko ao sehemu ya karibu yenye kuzungumuza luga yake.

  • Mahali pa kuchagulia luga

    Mujitayarishe (Mez 15:28; 16:1): Kama mwenye-nyumba anazungumuza luga ingine, fanya yako yote ili kumutolea ujumbe. Unaweza kujitayarisha kwa kufikiria mbele ya wakati luga mbalimbali zenye watu wanaweza kuzungumuza mu eneo yenu, na kwa hiyo unaweza kuchukua tafsiri za Biblia na video mu zile luga na kuziweka mu tablette ao telefone yako. Unaweza pia kutumia JW Language ili kujifunza namna ya kusalimia mutu mu luga fulani.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine