Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/99 uku. 7
  • Majibu ya maulizo yenu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majibu ya maulizo yenu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tulinde Mahali Petu pa Ibada Katika Hali Nzuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Tunaweza Kufanya Nini ili Kutunza Jumba Letu la Ufalme?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Hii Ndiyo Nafasi Yetu ya Kufanyia Ibada
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Fasi Yetu ya Ibada
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 11/99 uku. 7

Majibu ya maulizo yenu

◼Ni nani aliye na daraka la kusafisha Jumba la Ufalme?

Jumba la Ufalme lililo safi na lenye kuvutia huwa na uvutano wenye kufaa juu ya ujumbe tunaohubiri. (Linganisha 1 Petro 2:​12.) Kudumisha jumba likiwa zuri na lenye utaratibu ni jambo la maana, na kila mmoja anaweza kushiriki katika kulidumisha katika hali nzuri. Hatungepaswa kutazamia watu wachache wachukue mzigo huo wote. Kwa kawaida, usafishaji hupangwa kulingana na vikundi vya Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko, kiongozi wa funzo au msaidizi wake akichukua uongozi. Katika majumba ambamo zaidi ya kutaniko moja hukutanika, wazee watapanga mambo kusudi makutaniko yote yashiriki katika kudumisha hali nzuri.

Tunawezaje kushughulikia daraka hilo kwa njia bora zaidi? Jumba la Ufalme lingepaswa kusafishwa kulingana na programu ya kawaida. Vifaa vingepaswa kuwa tayari ili vitumiwe kwa ajili ya usafishaji. Orodha ya mambo yanayohitaji kufanywa ingepaswa kuwekwa mahali ambapo wafanyakazi wanaweza kuichunguza kwa ajili ya mwongozo. Kunaweza kuwa orodha mbili tofauti, moja kwa ajili ya usafishaji usioomba kazi nyingi baada ya kila mkutano, na nyingine kwa ajili ya usafishaji kamili zaidi wa kila juma. Kiongozi wa funzo la kitabu angepaswa kupanga ule usafishaji kamili ufanywe siku au wakati wenye kufaa kwa wale wote waliopewa mgawo huo. Uangalifu wa kawaida unapaswa kutolewa pia kwa majani yanayopandwa uwanjani, maua, na miti midogo-midogo. Vijia na mahali pa kuegeshea magari vingepaswa pia kudumishwa bila takataka. Kila mwaka, usafishaji kamili unapaswa kufanywa, labda kabla tu ya Ukumbusho. Huo unaweza kutia ndani kuosha madirisha na kuta, kuosha zulia, na kusafisha pazia.

Bila shaka, kila mmoja wetu anaweza kurahisisha mzigo kwa kutoangusha takataka au vitu vyenye gundi kama bazooka, ndani au nje ya jumba. Tunaweza kusafisha choo baada ya kila matumizi, tukikiacha kikiwa safi kwa ajili ya mtu mwenye kufuata. Iweni waangalifu ili kuepuka kuvunja vifaa au kuharibu vyombo. Iweni waangalifu kwa madoa kwenye zulia, kwa viti vyenye kuharibika, matatizo ya vyombo vyenye kupeleka maji, mataa ya umeme yenye kuungua, na kadhalika, na kujulisha bila kukawia mambo hayo kwa ndugu mwenye kushughulika na uhifadhi wa Jumba la Ufalme.

Acheni sisi sote tuwe tayari kufanya sehemu yetu. Hilo hufanyiza nyumba ya ibada yenye kupendeza na hututofautisha kuwa watu safi wanaoheshimu Yehova Mungu.​​—1 Pet. 1:​16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine