Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/99 uku. 8
  • Utasema nini kwa mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Utasema nini kwa mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Ambayo Wahubiri Walikutana Nayo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Sababu Gani Ulizo Hilo Linaulizwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Namna ya Kuwasaidia Watu Ambao Hawako Tayari Kujifunza Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Timiza Daraka Lako La Mweneza​-injili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 12/99 uku. 8

Utasema nini kwa mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu?

1 “Mimi ni mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu,” profesa mmoja kutoka Poland akamwambia mishonari mmoja katika Afrika. Hata hivyo, dada huyo aliweza kuwa na mazungumzo pamoja na mwanamke huyo na akampa kitabu La vie : comment est-elle apprue? Évolution ou création? Wakati mishonari huyo aliporudi juma lililofuata, profesa akamwambia: “Nimeacha kuamini kwamba hakuna Mungu!” Alikuwa amesoma kitabu Création chote na sasa akaomba funzo la Biblia. Unaweza kufanya nini ili kuwa na matokeo katika kutoa ushahidi kwa wale wanaosema kwamba hawaamini Mungu? Kwanza, fikiria sababu mbalimbali zinazofanya watu waseme hivyo.

2 Mambo yanayosababisha kutoamini: Kati ya wale wanaosema kwamba hawaamini kuna Mungu, si wote waliolelewa wakiwa hivyo. Wengi walikuwa katika aina fulani ya dini na wakati fulani waliamini Mungu. Walakini, matatizo makubwa ya afya au ya kifamilia, au ukosefu fulani wa haki waliopatwa nao vikadhoofisha imani yao. Kwa wengine, masomo waliyofunzwa katika shule za juu yamekuwa na uvutano usiofaa juu ya wazo lao kuhusu Mungu. Ona mifano ifuatayo ya watu walioamini kwamba hakuna Mungu, ambao baadaye walisitawisha imani yenye nguvu katika Yehova Mungu na wakawa Mashahidi wake.

3 Mwanamke mmoja katika Paris alikuwa amezaliwa akiwa na ugonjwa wa kupoozesha mifupa. Ijapokuwa alibatizwa akiwa Mkatoliki, yeye alijitangaza kuwa mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu. Wakati alipouliza watawa wa kike kwa nini Mungu aliruhusu azaliwe na ulemavu huo, jibu la watawa hao lilikuwa: “Kwa sababu anakupenda.” Mwanamke huyo alikataa kukubali wazo hilo lisilo na maana. Fikiria pia kijana mmoja katika Finland ambaye alipimwa na kuonekana kuwa na ugonjwa wa musuli usioweza kupona na ambaye alibaki tu katika kiti chake cha magurudumu. Mama yake alimpeleka kwa Mpentekoste aliyejidai kuponya watu. Lakini hakukuwa ponyo la kimuujiza. Kama tokeo, mwanamume huyo kijana akapoteza kupendezwa na Mungu na akawa mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu.

4 Mwanamume mmoja katika Honduras alilelewa akiwa Mkatoliki lakini alijifunza falsafa ya Kisoshalisti na imani kwamba hakuna Mungu. Kwa kusadikishwa na fundisho la chuo kikuu kwamba mwanadamu alitokana na mageuzi, yeye aliacha kuamini Mungu. Vivyo hivyo, mwanamke mmoja huko Marekani alilelewa akiwa Mmetodisti. Kwenye chuo kikuu, yeye alijifunza saikolojia. Imani yake ilipatwa na uvutano gani? Yeye anasema kwamba katika majira moja ya kiangazi mafunzo yake yaliharibu imani yote aliyokuwa nayo katika dini.

5 Kugusa mioyo ya wale wenye unyofu: Watu wengi ambao husema kwamba hawaamini Mungu wangethamini kujua ikiwa kuna suluhisho kwa matatizo ya afya mbaya, kutopatana katika familia, ukosefu wa haki, na kadhalika. Wao hupendezwa kwa unyofu na kupata majibu kwa maulizo kama vile: ‘Kwa nini kuna uovu?’ ‘Kwa nini mambo mabaya hupata watu wazuri?’ na ‘Ni nini maana ya uhai?’

6 Mume mmoja na mke wake wanaoishi Uswisi walilelewa wote wawili wakiwa watu wanaoamini kwamba hakuna Mungu. Wakati waliposikia kweli mara ya kwanza, itikio lao lilikuwa lisilofaa. Lakini walikuwa na matatizo makubwa ya familia na walifikiria talaka. Wakati Mashahidi walipowatembelea tena, walionyesha mume na mke hao wenye kuoana, kutoka katika Biblia, jinsi ya kushinda matatizo yao. Mume na mke hao walishangazwa na shauri lenye kutumika linalopatikana katika Maandiko, na walikubali funzo la Biblia. Ndoa yao ilitiwa nguvu, wakafanya maendeleo kiroho, na wakabatizwa.

7 Yale unayoweza kusema kwa mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu: Wakati mtu fulani anapokuambia ya kuwa anaamini kwamba hakuna Mungu, jitahidi kujua sababu inayomfanya aseme hivyo. Je! ni kwa sababu ya elimu aliyoipata, matatizo yaliyompata, au unafiki wa kidini na mafundisho ya uwongo ambayo ameona? Unaweza kumuuliza: “Je! umekuwa ukifikiri hivyo sikuzote?” au “Ni nini sababu inayokufanya ukate maneno hivyo?” Jibu lake litakusaidia uamue jambo la kusema. Mahali ambapo hoja zenye nguvu zinahitajiwa, unaweza kuhitaji kutumia kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali?

8 Unaweza kuendeleza mazungumzo na mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu kwa kuuliza:

◼ “Je! umekwisha kujiuliza: ‘Ikiwa kuna Mungu, kwa nini kuna mateso mengi sana na ukosefu wa haki ulimwenguni?’ [Acha mtu ajibu.] Je! ninaweza kukuonyesha maoni ya Biblia kuhusu habari hiyo?” Soma Yeremia 10:23. Baada ya kulisoma, muulize maoni yake juu ya andiko hilo. Kisha, mwonyeshe kurasa 16 na 17 katika broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Au, badala yake, unaweza kutumia sura 10 ya kitabu Muumba. Msihi kwa adabu akubali kichapo na kusoma habari hiyo.—Ili kupata madokezo ya ziada, ona kitabu Kutoa Sababu, kurasa 223-4.

9 Bila shaka, kati ya wale wanaoamini kwamba hakuna Mungu, si wote watakaokubali kweli. Lakini kuna wengi wanaotaka kuchunguza maoni mengineyo. Tumia njia nzuri ya kufikiri, usadikisho na, zaidi ya yote, nguvu ya Neno la Mungu ili kuwasaidia waone kweli.—Mdo. 28:23, 24; Ebr. 4:12.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine