Mambo Ambayo Wahubiri Walikutana Nayo
◼ Australie: John, ni mutu aliyesoma sana. Wakati alikuwa mutoto alikuwa anaenda ku kanisa. Lakini, alifikia kuwa “mutu anayeamini kama Mungu haiko.” Siku fulani, painia mumoja alimuachia broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? Wakati alimurudilia akamuachia broshua Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai. Painia huyo aliendelea kumutembelea ili kumuletea magazeti mapya, na kukazia habari zinazozungumuzia uumbaji ao unabii wa Biblia. Wakati aliona kama John anaanza kubadilisha mawazo yake, akamutolea kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Kisha kukisoma, John akaanza kukubali kwamba inawezekana mutu kuelewa mambo ya Mungu. Painia huyo akamutolea John kitabu Biblia Inafundisha, na wakachunguza sura ya pili fungu la 8 na mafungu 13-16. Maandiko waliyochunguza katika habari hiyo yalimugusa John moyo sana na akafikia kusema hivi: “Ni vizuri nichunguze kabisa Biblia.”
◼ Mexique: Mwanaume mumoja alimuambia ndugu fulani kwamba haamini kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu. Ndugu huyo alimuambia hivi: “Kama unapenda nitakuonyesha mambo yanayohakikisha kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu.” Ndugu alimutembelea kwa muda fulani, na kisha mwanaume huyo alianza kusadiki mambo ambayo alikuwa anajifunza katika Biblia. Aliguswa moyo sana wakati alijifunza kanuni za Mungu. Alimuambia ndugu huyo hivi: “Wakati tulianza kujifunza Biblia, mashauri yake yalionekana kama mashauri ya vitabu vingine na sikuguswa moyo. Lakini sasa, wakati tunaendelea kujifunza Biblia, zaidi sana mashauri ya Biblia juu ya mwenendo muzuri, ninaguswa moyo kabisa.”
◼ États-Unis: Siku fulani ndugu mumoja na bibi yake walikuwa wanahubiri mahali pa watu wengi katika muji fulani mukubwa, wakati huo mwanamuke mumoja wa Taiwan aliwakaribia. Mwanamuke huyo alikuwa anaamini kama Mungu iko, lakini alisema kama Biblia ni kitabu cha Wazungu. Alikaribia meza yetu ya vichapo ili kupata Biblia kwa sababu hata kama alikuwa na maisha mazuri aliona kama anakosewa kitu fulani. Alitumaini kama Biblia itamusaidia kuwa na maisha yenye maana kabisa. Ndugu huyo na bibi yake wakaanza kujifunza naye kitabu Biblia Inafundisha na broshua La paix et le bonheur durables : comment les trouver. Kuliko kuendelea na sura ya 2 ya kitabu Biblia Inafundisha, walizungumuzia sehemu yenye kichwa « Un guide bénéfique pour tous les humains » katika broshua hiyo. Kisha kuchunguza fungu 6 za kwanza katika sehemu hiyo, mwanamuke huyo alishangaa sana kuona kama Biblia ni kitabu tofauti na vitabu vingine vyote vya dini. Tena, wakati walizungumuzia unabii mbalimbali wa Biblia uliotimia, mwanamuke huyo alisema hivi: “Siwaze kama kuna kitabu kingine kinachoeleza mambo ya kweli kama Biblia!”
◼ Japon: Mwenye-nyumba fulani alimuambia muhubiri mumoja kwamba anaamini kama Mungu haiko. Ndugu huyo aliendelea kumutembelea ili wazungumuze naye habari zenye kichwa “Je, Kitu Hiki Kilijifanya chenyewe?” zilizo katika Amuka! Polepole, mwanaume huyo alibadilisha mawazo yake na akaanza kukubali kama inawezekana Muumbaji iko. Sasa mwanaume huyo anaamini kama Mungu iko, na anajifunza na muhubiri huyo broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!
◼ Kanada: Dada mumoja alimuachia mwanamuke fulani magazeti mapya wakati mwanamuke huyo alikuwa anatoka katika nyumba na kuenda kwenye motokari yake. Wakati dada alimurudilia, mwanamuke huyo alikataa kabisa kusikiliza na akamuambia kama hapendezwe, na haamini kama Mungu iko. Dada huyo hakuvunjika moyo, lakini alimuletea broshua Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha. Dada alimurudilia tena, na akamuambia hivi: ‘Hata kama hauamini kwamba Mungu iko, niliendelea kukukumbuka kwa sababu ninajua unachunga watoto peke yako.’ Kisha akamuonyesha mwanamuke ulizo lenye kuwa mwisho wa fungu la 6 kwenye ukurasa wa 4 wa broshua hiyo. Akamutia moyo asome somo la 2 ili kujua ni wapi anaweza kupata mashauri mazuri juu ya kulea watoto. Mwanamuke huyo alifurahi sana na akachukua broshua hiyo.