Kisanduku cha maulizo
◼ Ni nani anayepaswa kupokea kadi-kitambulisho kwa ajili ya mkusanyiko wa wilaya?
Kadi-vitambulisho kwa ajili ya mkusanyiko zinaweza kusaidia sana katika kutambulisha ndugu zetu na kuvumisha habari kuhusu mkusanyiko. Hata hivyo, hizo hazipaswi kufanyiwa ugawaji ovyoovyo. Hizo hutambulisha mvaaji kuwa na msimamo mzuri katika kutaniko fulani la Mashahidi wa Yehova.
Kadi ina nafasi kwa ajili ya jina la mtu na pia jina la kutaniko. Kwa hiyo, mtu huyo apaswa kuwa mwenye kushirikiana kwa kiasi cha kutosha na kutaniko lenye kuonyeshwa juu ya kadi. Sosaiti hutuma kiasi cha kadi kwa kila kutaniko. Lingekuwa jambo lenye kufaa kutoa kadi kwa kila mhubiri mwenye kubatizwa na asiyebatizwa. Pia, watoto na wengine ambao huhudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida na ambao ni wenye kufanya maendeleo kuelekea kushiriki katika huduma ya shambani wanaweza kupokea kadi. Halingekuwa jambo lenye kufaa kutoa kadi-kitambulisho kwa mtu aliyetengwa.
Wakati kadi zinapofanywa zipatikane, wazee wanapaswa kuangalia kwamba hizo zifanyiwe ugawaji kulingana na mwongozo huu.