“Njia Ya Mungu Huongoza Kwenye Uzima”
—Makusanyiko Ya Wilaya Na Ya Kimataifa 1998
1 Mezali 10:29 latukumbusha kwamba “njia ya BWANA [Yehova, NW] ni boma la nguvu.” Kusanyiko la wilaya la mwaka huu linacho kichwa chenye kufaa kama nini, “Njia ya Mungu Huongoza Kwenye Uzima”! Kichwa hicho kitazungumziwaje katika programu hiyo ya siku tatu? Sote tunangoja kwa hamu kile tunachowekewa akibani. Mawazo ya maana yatatolewa.
2 Wamishonari, watumishi wa kimataifa, au ndugu na dada wengine wanaotumikia katika migao ya ugenini watahudhuria makusanyiko ya kimataifa. Inatazamiwa kwamba kutakuwako maelfu ya wajumbe kutoka nchi nyingine wakiwako katika miji ambako makusanyiko ya kimataifa yatafanyika. Kwenye kusanyiko zitatolewa ripoti zinazoonyesha namna Yehova anavyobariki kazi katika maeneo mbalimbali.
3 Kuhudhuria Kunastahili Kufanyiwa Jitihada: Wengi wa akina ndugu zetu katika Afrika wanapata magumu kwa sababu ya vita na mizozo inayotikisa maeneo ya bara hilo. Kwao, makusanyiko ya watu wa Yehova huwa njia yao ya maisha. Wengine wanapaswa kutembea miendo mirefu ili kuhudhuria kwenye kusanyiko, hata hivyo hawawezi kufikiri kukosa moja. Katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (Zaïre ya kale), ndugu mmoja mwenye umri wa miaka 73 alitembea karibu kilometa 450 kwa mguu ili kuhudhuria kwenye kusanyiko. Alifika siku 16 baada ya kuondoka, miguu ikivimba, lakini akiwa mwenye furaha kuwapo. Baada ya kusanyiko, akiwa mwenye furaha sana na mwenye kutiwa nguvu kiroho, alirudi nyumbani kwake kwa mguu. Amekuwa akifanya hivyo kwa miaka mingi!
4 Katika Msumbiji, mwangalizi mmoja wa wilaya na mke wake walilazimika kupanda mlima mrefu na kuvuka jangwa kwa mguu ili kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya. Walifanya safari hiyo ya kilometa 90 kwa saa 45. Wahudhuriaji wote walitiwa moyo na kielelezo chao kizuri. Familia nyingi zilizokuwapo zilikuwa zimefanya jitihada zenye kufanana na hizo ili kuhudhuria. Mwangalizi wa wilaya huyo aliripoti kwamba ndugu fulani, kutia ndani mmoja mwenye umri wa miaka 60, walisafiri kilometa 200 kwa mguu!
5 Je! umefanya mipango dhahiri ili kuhudhuria kwenye kusanyiko la mwaka huu? Sisi pia huenda tutatembea miendo mirefu kwa mguu na tutahitaji kufanya jitihada na kujidhabihu ili kuwako kama vile familia. Panga mambo yako ili uhudhurie programu yote, tangu mwanzo hadi mwisho. Watu wengi wanaojifunza Biblia wanafanya maendeleo kuelekea ubatizo. Kwa kuhudhuria kwenye kusanyiko wataweza kuchukua uamzi mzuri. Je! umealika wanafunzi wako wa Biblia au watu wengine wenye kupendezwa wahudhurie kwenye kusanyiko pamoja nawe?
6 Kusanyiko la Siku Tatu: Mwaka huu, makusanyiko 59 yatafanyika Burundi, Congo-Brazzaville na Congo-Kinshasa. Zaidi ya Kifaransa, kusanyiko litafanywa katika Kiluba, Kirundi, Kiswahili, Lingala, Monokutuba, Otetela, Tshiluba na Uruund. Orodha ya mahali pa makusanyiko hayo imerudiliwa na kusahihishwa. Inapatikana kwenye kisanduku kilicho kwenye ukurasa 5. Kwa sasa mnajua kusanyiko ambalo kwa hilo kutaniko lenu linaalikwa.
7 Taarifa ya Pekee: Ni jambo la maana sana kwenu kuhudhuria kwenye kusanyiko ambalo kwa hilo kutaniko lenu limealikwa. Kuheshimu kwenu mipango hiyo na ushirikiano wenu vitafanya kwamba mambo yote yatukie kwa adabu na kwa mpango.—1 Kor. 14:33, 40.
8 Siku ya Tano, Siku ya Posho na Siku ya Yenga asubuhi, kusanyiko litaanza pa saa 3:30. Siku ya Tano na Siku ya Posho, litamalizika pa saa 11:00, na, Siku ya Yenga pa saa 10:00. Milango itafunguliwa kila siku pa saa 2:00 asubuhi. Wale walio na kazi peke yao ndio watakaoruhusiwa kuingia mapema. Hata hivyo, hakuna mtu atakayechungia mwingine viti kabla ya saa 2:00 asubuhi.
9 Tutakapokwenda kwenye kusanyiko au kurudi kutoka huko, tungepaswa kutafuta nafasi za kutoa ushahidi wa vivi hivi. Ujumbe wa Ufalme unaweza kupendeza watumishi kwenye vituo vya mafuta ya motokaa, wafanyabiashara, watoza-ushuru, watumishi kwenye hoteli, na wagawa-mlo. Jitayarishe kwa jambo hilo kwa kuchukua pamoja nawe trakti, magazeti ya karibuni, broshua, au vichapo vingine, ili kuchukua nafasi za kutoa ushahidi kwa watu ambao huenda hawawezi kufikiwa na habari njema kwa njia nyingine.—2 Tim. 3:17.
10 “Kazieni Uangalifu Jinsi Msikiavyo”: Wale wanaohudhuria kwenye kusanyiko hufanya vema kufuata shauri linalopatikana kwenye Luka 8:18. Kila mmoja anatiwa moyo kuleta Biblia yake, kitabu cha nyimbo na buku la kuandikia. Tusikilize kwa uangalifu mawazo makuu ya kila hotuba na tufanye maandishi mafupi. Tijiulize wenyewe namna tunavyoweza kutumikisha kibinafsi yale tunayosikia. Jioni kila siku ya kusanyiko, kabla ya kulala, kwa nini tusirudilie maandishi yetu na kujichunguza ili kuona ikiwa tunafuata kwa ukaribu njia ya Yehova inayoongoza kwenye uzima?—Mez. 4:10-13.
11 Imeonekana kwamba wakati wa vipindi, wengine hutoka mahali pa kusanyiko na kwenda kuketi nje, jambo linalofanya wakose programu. Wengine wameonwa wakitembea kwa uzembe katika vipito wakati ambapo wangekuwa wakiketi na kusikiliza. Vikundi vya vijana vilitoka mahali pa kusanyiko katikati ya alasiri (kisha mchana-kati). Watumishi fulani wa kale wa Yehova walifanya makosa mazito kwa kuwa hawakusikiliza vikumbusho kwa uangalifu. Tunataka bila shaka kuepuka kuanguka katika makosa yaleyale. (2 Fal. 17:13-15) “Mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ametayarisha mafundisho bora tunayohitaji sote. Ni jambo la lazima sana kwamba ‘tukazie uangalifu zaidi kuliko ilivyo kawaida mambo yaliyosikiwa nasi’ kwenye kila kimoja cha vipindi vya siku tatu za kusanyiko. Kila siku, jambo fulani linalotuhusu kipekee litatolewa, zaidi mawazo yatakayokuwa na uvutano mzuri juu ya namna yetu ya kuishi katika wakati ujao. Kwa kuwa waangalifu na kufanya matumizi mazuri ya kile ambacho Yehova atatutolea kwa upande wa kiroho wakati wa makusanyiko ya karibuni, tumaini letu litakazwa kikiki, jambo litakalotuzuia “kupeperushwa mbali,” yaani kujitenga mbali na njia ya Mungu iongozayo kwenye uzima.—Mt. 24:45; Ebr. 2:1.
12 Mvalio Unaomtukuza Yehova: Katika nyakati za hatari tunazoishi, tunahitaji kuwa waangalifu zaidi ili tusijiache tuvutwe na roho ya ulimwengu. (1 Kor. 2:12) Mavazi yetu na kujipamba kwetu vinapaswa kuwa vyenye kiasi na vinapaswa kuonyesha adhama (heshima) ya Mungu tunayemwabudu. (1 Tim. 2:9, 10) Si jambo la lazima kuwa na mavazi ya bei kubwa “ili kuremba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu.” (Tito 2:10) Ona mashauri bora yenye kutumika ambayo yanatokana na Maandiko, kwenye mafungu 14 hadi 18 ya Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1997, kurasa 17 na 18. Tusidharau kamwe nguvu ya ushahidi tunaoweza kutoa kwa kuwa na mavazi yanayomheshimu Yehova.
13 Mwenendo Unaomtukuza Yehova: Tunajua kwamba mwenendo wetu wa Kikristo unaweza kuwa na uvutano juu ya namna wengine wanavyoiona ibada ya kweli. Kwa hiyo, tunataka kujiendesha kila wakati kwa namna yenye kustahili habari njema na yenye kumtukuza Yehova.—Flp. 1:27.
14 Mwaka uliopita, kusanyiko la wilaya lilifanywa kwa mara ya kwanza kaskazini mwa Angola. Kwenye siku ya pili ya kusanyiko, maofisa wawili wa polisi ya mahali walitumwa kwenye uwanja wa kusanyiko kuhakikisha kwamba utaratibu wa kijamii unaheshimiwa. Walibaki mchana wote mzima. Mwishoni mwa siku, walieleza mshangao wao kwa yale waliosikia na mwenendo wenye utaratibu waliouona. Mmoja wao alisema: “Kwa nini tulitumwa hapa? Tunajua kwamba Mashahidi wa Yehova hulinda utaratibu kwenye makusanyiko yao.”
15 Mshiriki mmoja wa chama cha kisiasa katika nchi moja ya Afrika alikimbilia Ulaya, kwa kuwa washiriki wote wa chama chake waliuawa. Akiwa na matatizo mengi, yeye alivunjika moyo. Hatimaye, alikubali funzo la Biblia. Alipohudhuria kwa mara ya kwanza kusanyiko la wilaya, aliguswa moyo kuona watu kutoka mahali mbalimbali wakikusanyika pamoja katika amani na upatano, jambo lililomsadikisha kwamba aliipata kweli. Kwenye kusanyiko hilo akaamua kuvunja uhusiano wake wote wa kisiasa. Baadaye alibatizwa, na sasa yeye na watoto wake wanamtumikia Yehova.
16 Mwenendo wetu kwenye kusanyiko mwaka huu utakuwa na matokeo gani kwa wale ambao labda watakuwa wakihudhuria kwa mara ya kwanza? Je! wataona roho ya ushirikiano kuwa wazi wakati tutakapokuwa tukitumika pamoja kama waliojitolea? Je! wataguswa moyo na usafi wa uwanja na kwa kuona kwamba, kabla ya kuondoka, sisi na watoto wetu tunaokota takataka ambayo inaweza kupatikana mahali tulipo? Je! wataona mwenendo wetu mzuri wakati tunapokwenda na kutoka kwenye makao na mahali pa kusanyiko? Je! wataona kwamba sisi wazazi tunachunga kwa ukaribu watoto wetu kila wakati? Acheni tuhakikishe kwamba tunafanya yote ili kugusa moyo wa wale wanaotutazama.
17 Kulipia Gharama za Kusanyiko: Katika ulimwengu wa sasa, tikiti ya kuingia ili kuhudhuria kwenye tukio la mchezo katika uwanja wa mpira au kwa ajili ya tukio lingine lolote katika jumba la makusanyiko ni yenye bei kubwa. Hilo linasababishwa kwa sehemu na malipo ya kukodi yenye bei ya juu katika maeneo ya mijini. Kwenye makusanyiko, Sosaiti sikuzote imekuwa na kanuni “Ingia bila malipo—Hakuna sadaka.” Namna gani, basi, fedha za kukodi na gharama nyingine za kusanyiko vitalipwa? Kupitia michango ya ukarimu ya wahudhuriaji. Tuko hakika kwamba mtaonyesha roho ya ukarimu kama ile ya watumishi wa Mungu wa kale, waliomwiga Yehova Mungu na Yesu Kristo. (2 Kor. 8:7) Uangalifu mkubwa unachukuliwa ili kuweka michango yote mahali palipo salama, kuihesabu na kuitumia kupatana na kusudi layo.
18 Nafasi za Kukaa: Maagizo yaliyotolewa kwa miaka mingi bado ni yenye kufaa: VITI VINAWEZA KUCHUNGWA TU KWA AJILI YA WASHIRIKI WA KARIBU WA FAMILIA YAKO NA YEYOTE AMBAYE ANAWEZA KUWA AKISAFIRI NAWE KATIKA GARI LAKO. Ni jambo la kufurahisha kuona kwamba, miaka hii ya nyuma, wahudhuriaji zaidi na zaidi ni wenye kuheshimu mwongozo huo, jambo linaloongeza hali yenye kujaa upendo inayotawala kwenye makusanyiko yetu. Kwenye makusanyiko mengi, nafasi fulani za kuketi zinaweza kufikiwa kwa urahisi zaidi kuliko zingine. Tafadhali onyesheni wema kwa kuacha nafasi zenye kufaa zaidi kwa watu wazee-wazee na wengine ambao hali yao inaomba hizo. Kumbuka kwamba ‘upendo hautafuti masilahi yao wenyewe.’—1 Kor. 13:4, 5; Flp. 2:4.
19 Kamera, Kameskopi na Redio Kaseti: Kamera na vyombo vya kurekodi vinaweza kutumiwa. Hata hivyo, hatupaswi kukengeusha fikira za wahudhuriaji wengine kwa kuvitumia. Hatupaswi kutembea muda wa vipindi ili kupiga picha, kwa kuwa kuna hatari ya kuvuruga wengine wanaojitahidi kusikiliza. Chombo chochote, kiwe cha aina gani, hakipaswi kuchomekwa kwenye mkondo wa umeme au kwenye mfumo wa sauti wa kusanyiko, kufunga vipito, ukumbi, au kuzuia wengine wasione.
20 Msaada wa Kwanza: Idara ya Msaada wa Kwanza hutumika tu kwa ajili ya hali za dharura (haraka). Tafadhali leteni pamoja nanyi aspirini, vituliza-tumbo, vitambaa vya kidonda, pini kwa ajili ya vitoto, na mambo mengine yenye kufanana na hayo ambayo hayatapatikana kwenye kusanyiko. Wale wote walio na matatizo ya moyo, wale wenye hatari ya kuzimia kwa sababu ya ugonjwa wa kisukari au kushambuliwa, n.k., wanapaswa kuwa na madawa yanayohitajiwa. Mshiriki wa familia yao au wa kutaniko lao anayejua hali yao angepaswa kuwa daima pamoja nao ili kuwasaidia uhitaji unapojitokeza. Imefika kwamba, kwenye makusanyiko, watu walio na magonjwa yasiyokoma ambao waliachwa peke yao wakawa wagonjwa sana, jambo lililotokeza magumu. Ikiwa mtu fulani ana uhitaji wa tiba ya pekee na kwamba hakuna mshiriki wa familia yake awezaye kushughulika naye, wazee wa kutaniko wangepaswa kujulishwa hali hiyo, nao watachukuwa mipango yenye kuhitajiwa ili kumsaidia. Hakutakuwa nafasi za pekee kwa wale walio na magonjwa yanayoamka kwa wepesi.
21 Mlo: Kila mmoja angepaswa kuleta chakula chake mwenyewe badala ya kuondoka kwenye kusanyiko wakati wa pumziko dogo la mchana-kati ili kununua kitu fulani nje. Chakula chepesi, chenye kujenga mwili na kilicho rahisi kuchukua kingepaswa kutosha. Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1996, kwenye mafungu 6 na 7, inapendekeza vyakula fulani fulani. Machupa ya bilauri na vinywaji vyenye alkoholi havitaingizwa mahali pa kusanyiko. Vyombo vya kutia vyakula baridi vinapaswa kuwa vidogo vya kutosha ili kuingia chini ya kiti chako. Wahudhuriaji wameonwa wakila wakati wa programu, lakini hilo ni ukosefu wa heshima.
22 Sisi ni wenye furaha kama nini kufikiri juu ya kusanyiko la Wilaya “Njia ya Mungu Huongoza Kwenye Uzima” ambalo sasa ni karibu! Je! umechukua mipango ili kulihudhuria? Na uwe na safari njema na urudi nyumbani ukiwa mwenye kuburudishwa, ukiazimia kuendelea katika utumishi wenye thamani wa Yehova na kuendelea kufuata njia ya Mungu iongozayo kwenye uzima, kwa ajili ya furaha ya milele.
[List of locations on page 5]
Makusanyiko Ya Wilaya 1998
Agosti 14-16, 1998
BANDUNDU (LI): BD-1; BD-10
BUMBA (LI): EQ-4; EQ-12; EQ-15; EQ-20; EQ-22; OR-3; sehemu OR-10; OR-15
BUNIA (SW): OR-4; OR-12
KIKWIT (F, MK): BD-2; sehemu BD-19; BD-24; sehemu BD-22
KINSHASA (F): KN-4; KN-7; KN-10
MANONO (KU): Sehemu KT-10; KT-14; sehemu KT-16
MATADI (LI): BC-1; BC-5
MBANDAKA (LI): EQ-2; EQ-7; EQ-16; EQ-17; EQ-23
MBUJI-MAYI (F, SH): KA-2; KA-8; KA-16; KA-17; KA-20; sehemu KA-25
SANDOA (DR): Sehemu KT-5; KT-21
TSHIKAPA (F, SH): KA-6; KA-22; KA-23; KA-31
Agosti 21-23, 1998
BRAZZAVILLE (F, LI): CO-1; CO-5; sehemu CO-3; sehemu CO-7; sehemu CO-8
BULUNGU (MK): BD-5; sehemu BD-19; BD-20
GOMA (F, SW): KI-2; KI-6; KI-14
IDIOFA (MK): BD-8; BD-16
ISIRO (LI): OR-2; sehemu OR-17; OR-18
KANANGA (F, SH): KA-1; KA-9; KA-14; KA-18; KA-19; KA-28; KA-30
KIMPESE (LI): BC-2; sehemu BC-3; BC-4; sehemu BC-6; BC-7; BC-8
KINDU (SW): KI-3; sehemu KI-4; KI-13 ; sehemu OR-5; OR-16
KINSHASA (LI 1): KN-1; KN-3; KN-8; KN-12; KN-13; sehemu BC-3
KISANGANI (F): Sehemu OR-1; sehemu OR-7; sehemu OR-8; sehemu OR-10; sehemu OR-14
LISALA (LI): EQ-8; EQ-11; EQ-18; EQ-21
LODJA (OT): KA-4; KA-11; KA-12; sehemu KA-26; KA-27; sehemu KA-32
LUBUMBASHI (F, SW): Sehemu KT-1; KT-2; KT-13
MULONGO (KU): Sehemu KT-8; sehemu KT-10; sehemu KT-16
POPOKABAKA (LI): Sehemu BC-6; BD-7 ; sehemu BD-13; sehemu BD-21
Agosti 28-30, 1998
BOENDE (LI): EQ-3; EQ-6; sehemu EQ-13; EQ-24
BUKAVU (F, SW): KI-1; KI-11; KI-12
BUTEMBO (SW): KI-7; KI-9
DUNGU (LI): OR-6; OR-13; sehemu OR-17
GBADOLITE (LI): EQ-5; EQ-9; EQ-19
KABINDA (F, SH): KA-5; KA-13; sehemu KA-32
KALEMIE (SW): Sehemu KT-12; KT-18; sehemu KT-19
KENGE (MK): BD-3; BD-9; sehemu BD-21
KINKONDJA (KU): Sehemu KT-8; KT-9; sehemu KT-10; sehemu KT-16
KINSHASA (LI 2): KN-2; KN-5; KN-6;
KN-9; KN-11
KISANGANI (LI, SW): Sehemu OR-1; sehemu OR-5; sehemu OR-7; OR-9; sehemu OR-14
KONGOLO (SW): Sehemu KI-4; KT-22
LIKASI (F, SW): Sehemu KT-1; KT-17; KT-20; KT-23
NIOKI (LI): BD-4; BD-6; BD-14; BD-15
POINTE-NOIRE (F, MK-Cgo): CO-2; CO-6; sehemu CO-8
UVIRA (SW): KI-8; sehemu BU-1
Septemba 4-6, 1998
BENI (SW): KI-5; KI-10
BOKUNGU (LI): EQ-10; sehemu EQ-13
BUJUMBURA (RU): Sehemu BU-1; BU-2; BU-3
GEMENA (LI): EQ-1; EQ-14
ILEBO (F, SH): KA-10; KA-15; KA-29
KAMINA (SW, KU): Sehemu KT-4; sehemu KT-6; KT-7; KT-15
KIRUNGU/MOBA (SW): Sehemu KT-12; sehemu KT-19
KOLE (OT): KA-7; KA-21; sehemu KA-26
KOLWEZI (F, SW): Sehemu KT-1; KT-3 ; sehemu KT-5
MUKEDI (MK): BD-18; BD-23
OUESSO (F): Sehemu CO-3; sehemu CO-7
TEMBO (LI): BD-17; sehemu BD-13
Septemba 11-13, 1998
BUTA (LI): Sehemu OR-8; OR-11
GUNGU (MK): BD-11; BD-12; sehemu BD-22
KABONGO (KU): Sehemu KT-4; sehemu KT-6; KT-24
MWENE DITU (F, SH): KA-3; KA-24; sehemu KA-25
PEPA (SW): KT-11; KT-25
[Memory Aid Box on page 6]
Vikumbusho Kwa Ajili Ya Kusanyiko La Wilaya
▪ Ubatizo: Wale wanaotaka kubatizwa wanapaswa kukaa katika sehemu iliyochaguliwa kabla ya programu kuanza Siku ya Posho asubuhi. Kila mmoja anayetaka kubatizwa anapaswa kuleta nguo ya kuoga nayo yenye kiasi na kitambaa cha kupangusa maji. Wakati uliopita, wengine walivaa mavazi ambayo hayakuwa ya adabu na ambayo yalipunguza sifa ya tukio. Wazee watakaochunguza maswali ya kitabu Huduma Yetu pamoja na wanaotaka kubatizwa wanapaswa kuhakikisha kwamba kila mmoja anaelewa nukta hizo. Ubatizo, kama vile wonyesho wa wakfu wa mtu, ni jambo la kibinafsi kati ya mtu na Yehova. Hivyo, haipangwi kuwako “ubatizo wa vikundi” vya watu wawili au zaidi watakaokamatana mikononi au kushikana vidole wakati wa ubatizo.
▪ Alama: Tafadhali vaeni kila wakati alama ya 1998, iwe kwenye kusanyiko au katika safari yenu ya kwenda na kurudi. Hilo mara nyingi hutokeza nafasi za kutoa ushahidi mzuri. Alama na vishika-alama vitapatikana kupitia kutaniko, kwa kuwa havitapatikana kwenye kusanyiko. Usingoje hadi siku chache kabla ya kusanyiko ili kuomba alama kwa ajili yako na kwa ajili ya familia yako. Usisahau kuwa na kadi yako “Instructions médicales—Pas de sang” pamoja nawe.
▪ Upangishaji: Tunaomba kwa wote kushirikiana kwa kutumia TU orodha ya mahali pa kulala inayotolewa na idara ya upangishaji ya kusanyiko. Upangishaji hufanyika kwa kawaida nyumbani kwa watu binafsi. Tunapaswa kujionyesha wenye shukrani kwa ndugu na dada hao wanaokubali kutupangisha. Kwa kuongezea, lingekuwa jambo lisilo sawa kwamba wale wanaoonyeshwa ukaribishaji huo wautumie vibaya na kuomba kwamba wapangishwe muda mrefu kabla au baada ya kusanyiko. Upangishaji unatolewa tu WAKATI wa kusanyiko. Wale wanaofaidika na aina hiyo ya upangishaji wanapaswa kuheshimu mali ya yule anayewapangisha, kutoharibu chochote, kutokwenda katika nafasi wasikoalikwa, na kuangalia kwamba watoto wao wafanye vivyo hivyo. Ikiwa wapangishaji wanapambana na tatizo lolote katika jambo hilo, wanapaswa bila kukawia kujulisha idara ya upangishaji, itakayokuwa yenye furaha kutoa msaada wayo.
Zijapokuwa ‘siku za mwisho za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo’ tunazoishi, tunaamini kwamba wengi watafungua milango kwa waombaji wa mahali pa kupanga, kama ilivyokuwa Kinshasa na mahali pengine, ndugu zetu walipolazimika kukimbia vita. Ni jambo la huzuni kujua kwamba mahali pengi ndugu hujionyesha wasio tayari kutenda hivyo kuelekea wakusanyikaji. Bila shaka, hatungetaka kwamba magumu ya sasa yatufanye tupunguze upendo wetu kwa wengine kwa kutuzuia kuwa wakaribishaji tunapokuwa na uwezo wa kufanya hivyo.—2 Tim. 3:1; Ebr. 13:1, 2; Yn. 13:35.
▪ Utumishi wa Wenye Kujitolea: Je! unaweza kujiwekea kando muda mdogo wakati wa kusanyiko ili kusaidia katika moja ya idara? Tunaweza kujifanya wenye mafaa sana na kujiletea kutosheka ikiwa tunahudumia ndugu zetu, hata kwa saa chache. Ikiwa unaweza kusaidia, tafadhali fika kwenye idara ya wenye kujipendea kwenye kusanyiko. Watoto wenye umri wa chini ya miaka 16 wanaweza pia kutoa mchango mzuri kwa kutumika chini ya uongozi wa baba zao, mama zao au mtu mwingine mwenye umri mkubwa aliye na madaraka.
▪ Tuwe Tayari Kutoa Ukaribishaji Wetu: Wengi wa wale wanaohudhuria kwenye makusanyiko ya wilaya yanayofanyika katika eneo letu wanaenda, kwa kusudi hilo, mahali palipo mbali na makao yao. Wanahitaji mahali pa kupumzika usiku ili kuwa tayari kufuata programu ya siku inayokuja. Ikiwa tunaishi katika mji ambamo kusanyiko litafanyika, je! hatuwezi kushirikiana na Idara ya Upangishaji kwa kupendekeza mahali pa kupanga kwa wakusanyikaji watakaopahitaji? Hivyo tunapata nafasi ya kujionyesha wakaribishaji, jambo ambalo halitakosa kukaza vifungo vya kidugu na kuzidisha sifa kwa Yehova.—1 Pet. 4:9; Ebr. 13: 1, 2.
▪ Tuwe na Maoni Yafaayo juu ya Utumishi wa Kujitolea Wakati wa Matayarisho ya Makusanyiko Yetu: Kutayarisha kusanyiko la wilaya kunaomba nishati nyingi na wakati. Kadiri wanavyokuwa wengi wafanyakazi wenye kujitolea ili kushiriki kwenye kazi mbalimbali za matayarisho, kadiri mzigo unakuwa mwepesi. Lakini, ni nini maana ya mfanyakazi mwenye kujitolea? Kulingana na kamusi Le nouveau petit Robert, mfanyakazi mwenye kujitolea ni mtu anayetoa utumishi wake kwa kujipendea tu. Kutokana na hilo, mfanyakazi mwenye kujitolea hawezi kutazamia mshahara kutokana na utumishi wake mbalimbali anaoutoa. Ni wazi kwamba mipango midogo midogo inaweza kuchukuliwa kwa fedha kutoka makutaniko ya mahali ili kuwapa wafanyakazi wenye kujitolea wanaotumika sana angalau mlo mmoja kwa siku ili kwamba mambo yote yawe tayari kabla ya programu kuanza. Huu ungepaswa kubaki mpango wa mahali ambamo makutaniko yangejikuta yakipewa pendeleo la kutoa mchango wa vyakula au wa fedha. Hivyo, haingepaswa kutazamiwa kwamba Sosaiti ifanye jambo fulani katika njia hiyo.—Zab. 110:3.
▪ Tufaidike na Akiba Yetu: Ni akiba gani? Wakati na jitihada ambavyo kuwako kwetu kunatugharimu. Halingekuwa jambo la hekima kwamba tujitayarishe kwa makini ili kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya na baadaye turudi Siku ya Yenga jioni tukiwa tumekosa sehemu kubwa ya programu. Ikiwa sisi ni wakomavu kiroho, hatuwezi kukosa lolote la yale Yehova ametayarisha kwa ajili yetu. (1 Kor. 2:9, 10) Kila siku ya kusanyiko, tungepaswa kujikaza kuchukua nafasi kabla ya kipindi kuanza. Hata ikiwa sisi ni wenye kupitisha nyakati zenye furaha pamoja na marafiki wetu wa zamani, mwenye-kiti anapotangaza mwanzo wa programu, kuacha kuzungumza na kwenda mara moja mahali petu ni kuonyesha heshima kwa wahudhuriaji na ndugu kwa ujumla.
▪ Angalisho: Hakikisha sikuzote kwamba milango ya gari lako imefungwa kwa funguo na usiache kamwe kitu chochote kiwezacho kuvuta macho. Wevi na wagusa-mifukoni huvutwa na makusanyiko makubwa. Halingekuwa pia jambo la hakima kuacha kitu cha thamani kwenye nafasi yako. Hauwezi kuwa hakika kwamba wote wanaokuzunguka ni Wakristo. Kwa nini umweke mtu katika jaribu? Tumepata pia ripoti kwamba watu wasiojulikana wamejaribu kuvuta watoto wadogo nje. UWE MWENYE KUONA WATOTO WAKO KILA WAKATI.