“Wajumbe wa Amani ya Kimungu”—Kusanyiko la Wilaya 1996
1 Bila shaka kwamba kusanyiko la wilaya la mwaka huu litatusaidia kulinda amani ya kimungu na litaonyesha daraka letu kuhusu kuwasaidia wengine kupata amani hiyo. Kama ilivyotangazwa na Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 1996, kusanyiko hilo litakuwa na kichwa cha habari “Wajumbe wa Amani ya Kimungu.” Je! umejitayarisha ili kutokosa jambo lolote?
2 Kusanyiko la Siku Tatu: Tupo hakika kwamba utathamini kikamilifu kusanyiko la mwaka huu na kwamba utarudi nyumbani kwako ukiwa mwenye bidii mpya. (2 Sik. 7:10) Mwaka huu, kusanyiko litadumu pia siku tatu. Je! umekwisha kuomba likizo ili kuweza kuwako muda wa siku tatu hizo? Ikiwa una watoto wenye umri wa kwenda shuleni, je! umejulisha walimu wao kwamba hawatakupo Siku ya Tano kwa sababu ya tukio moja la maana katika mazoezi yao ya kidini?
3 Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 1996 inatoa tarehe na mahali pa makusanyiko yote yatakayofanyika katika eneo. Mwandishi wa kutaniko lenu tayari amekwisha kuwaonyesha lile ambalo mnaalikwa kwalo.
4 Kusanyiko litaanza kila siku tangu saa 3:30, na litamalizika yapata saa 10 Siku ya Yenga. Milango itafunguliwa saa 2. Ni wale tu walio na kazi fulani ya kutimiza ndio watakaoruhusiwa kuingia mapema, lakini hawataruhusiwa kuchungiana viti kabla ya majengo kufunguliwa kwa watu wote. Je! tutaonyesha wema kuelekea ndugu zetu wazee-wazee na vilema kwa kuacha nafasi huru katika sehemu ambazo ni rahisi kufikiwa na nzuri? Usisahau kwamba “upendo . . . hautafuti faida [zake] binafsi.”—1 Kor. 13:4, 5; Flp. 2:4.
5 Je! Tutanolewa? Baada ya kutaja Mezali 27:17, “chuma kinanoa chuma,” Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1993, ukurasa 8, kichwa kidogo cha habari “Jinsi Wakristo ‘Wanavyonoana’ Wamoja kwa Wengine,” fungu la 1 lilikuwa likisema: “Sisi ni kama vyombo vinavyohitaji kunolewa kikawaida. Kwa kuwa upendo tunaoonyesha kwa Yehova na maamuzi tunayochukua kulingana na imani yetu yanaomba tuwe tofauti na ulimwengu, imetupasa kujitenga na umati.” Jinsi gani kutumikisha shauri hilo?
6 Sisi ni tofauti na ulimwengu na tunapaswa kubaki hivyo. Tunapaswa kuendelea kufuatia bidii yetu ikiwa tunapenda kuwa wenye bidii kwa matendo mema. (Tito 2:14) Hiyo ndiyo sababu makala ya Mnara wa Mlinzi iliyotangulia kutajwa ilikuwa ikisema: “Tunapokuwa pamoja na wale wanaompenda Yehova, tunanoana wamoja kwa wengine, tunachocheana wamoja kwa wengine kwenye upendo na kazi zilizo nzuri.” Kusanyiko la wilaya ni mojawapo ya mipango ambayo Yehova anachukua ili kutusaidia kunoa hali yetu ya kiroho. Hatuwezi kujiruhusu kukosa sehemu moja yalo.
7 Tujionyeshe Wenye Hekima kwa Kusikiliza: Kusikiliza ni ufundi ambao unapaswa kukomazwa. Inasemekana kwamba mtu wa kawaida anachunga yapata nusu ya yale anayosikia, haidhuru uangalifu anaofikiri kutumia kwa kusikiliza. Leo, mkazo unatiliwa juu ya viburudisho; inaweza hivyo kufikia kwamba inakuwa vigumu kwetu kukaza fikira kikiki muda mrefu. Je! tunaweza kujaribu kutengeneza uwezo wetu wa kukaza fikira kikiki, hasa tunapokuwa wenye kukaa katikati ya watu wengi ili kumsikiliza mtu anayesema? Ikiwa, baada ya kurudi nyumbani kwako, wanakuomba kufanya kifupi cha kila siku ya kusanyiko, je! ungeweza kufanya hivyo? Jinsi gani tunaweza kutengeneza sote uwezo wetu wa kusikiliza, kwa namna kusikiliza kwa uangalifu uliokazwa kwa kila sehemu inayotolewa kwenye kusanyiko?
8 Ni jambo la muhimu kuonyesha kupendezwa kwa kina kirefu, kwani ikiwa sivyo hatuwezi kutumikisha zawadi ya kimungu ambayo ni ubongo. Kwa mfano, zaidi tunavyopendezwa na habari, zaidi inakuwa rahisi kwetu kukumbuka mambo makuu ya hotuba au ya sehemu ya programu. Hata hivyo, hilo lategemea katika sehemu kubwa uangalifu wa pekee ambao tunatoa kwa mambo ambayo tuna pendeleo la kusikiliza kwenye makusanyiko ya wilaya. Kupendezwa kwa pekee na uangalifu ambao tunatoa kwa kila sehemu ya kusanyiko kunategemea hali yetu ya kiroho ya sasa na pia matarajio yetu ya wakati ujao. Kwenye makusanyiko, tunafundishwa njia za Yehova, tunapokea maagizo juu ya namna ya kutimiza kazi inayookoa uhai. (1 Tim. 4:16) Wazia ikiwa wewe ni mashua juu ya bahari yenye msukosuko kutokana na upepo. Ahadi za Yehova zinafanana na nanga yenye nguvu ya tumaini. Ikiwa mtu si mwenye makini wakati wa makusanyiko ya Kikristo na kwamba anaacha akili yake kutanga-tanga huku na huku, labda atapita pembeni ya mashauri au fundisho ambalo mawazo makuu yangeweza kumlinda kuzama kiroho.—Ebr. 2:1; 6:19.
9 Katika mahali pengi ulimwenguni, ndugu zetu wanafanya bidii kubwa kimwili ili kuhudhuria kwenye mikutano. Ni jambo lenye kugusa moyo kuona uangalifu wenye kukazwa walio nao wakati wa makusanyiko. Mahali pengine, hata hivyo, wengine wanapumbazisha wahudhuriaji kwa kutembea-tembea mahali pa kusanyiko wakati wa vipindi. Wengine wanafika nyuma. Wakati wa makusanyiko fulani, ilikuwa vigumu kusikia dakika za kwanza kwanza za programu kwa kuwa watu wengi walikuwa wakitembea-tembea katika vinjia na nyuma ya wasikilizaji. Kwa kawaida sio ndugu wafanyakazi ya kujipendea katika idara fulani, wala mama wanaoshughulikia watoto wao wachanga. Mara nyingi, fujo inatokezwa na watu ambao wapo tu wanapiga mdomo (kuzungumza). Mwaka huu, idara ya ukaribishaji itakuwa yenye makini sana kwa tatizo hilo, na tunatumaini kwamba kila mtu atakaa wakati msimamizi atakapowaalika wasikilizaji kufanya hivyo. Tutawashukuru sana kwa ushirikiano wenu kwa upande huo.
10 Ni mashauri gani yenye kutenda kazi yatakayotusaidia kuwa zaidi wenye makini kwenye kusanyiko na kuchunguza zaidi mawazo yatakayotolewa? Yale tuliyosema miaka iliyotangulia yanabaki yenye thamani: (a) Kaza fikira kikiki juu ya sababu kubwa iliyokufanya uje katika mji ambamo kusanyiko linafanyika. Haukuja kwa sababu ya kujiburudisha, lakini kwa ajili ya kusikiliza na kujifunza. (Kumb. 31:12) Jikaze vya kutosha kupumzika kila usiku. Ikiwa wewe ni mwenye kuchoka sana unapokuja kwenye kusanyiko, utakuwa na magumu ya kukaza fikira kikiki. (b) Kuja mapema zaidi ili kuwa na wakati wa kuegesha gari lako na kukaa kabla ya mwanzo wa programu. Ikiwa unakimbilia kukaa kwenye dakika ya mwisho-mwisho, kuna uwezekano mkubwa wewe kukosa mwanzo wa programu. (c) Andika kwa kifupi mambo makuu. Ikiwa unaandika mambo mengi, hilo litakuzuia kusikiliza kwa makini. Katika kuandika, uwe hakika kwamba haukosi mawazo mengine kwa kuwa unakaza fikira juu ya maandishi yako. (d) Wakati sehemu moja ya kusanyiko inapotangazwa, uwe tayari kuisikiliza kwa kupendezwa kwingi. Ujiulize: ‘Ninaweza kujifunza nini kutokana na sehemu hii ili kuongeza shukrani yangu na upendo wangu kwa Yehova? Jinsi gani habari hizi zinaweza kunisaidia kuonyesha kikamilifu zaidi utu mpya? Jinsi gani hilo litanisaidia kujiboresha katika huduma?’
11 Mwenendo Unaopamba Huduma Yetu: Paulo alimtia Tito moyo kuwa “kielelezo cha kazi zilizo nzuri.” Kwa kuonyesha uaminifu-mshikamanifu katika mafundisho yake, Tito angewasaidia wengine “kulipamba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu katika mambo yote.” (Tito 2:7, 10) Kila mwaka, tunapokea vikumbusho vyenye urafiki vikituonyesha kwa nini ni jambo la lazima kuwa na mwenendo unaopatana na mapenzi ya Mungu katika safari kuelekea kusanyiko, nafasi ambako tunapangishwa, na pia mahali pa kusanyiko.
12 Msimamizi wa hoteli fulani alisema: “Sikuzote ni furaha ya kuwa na Mashahidi kwa kuwa wao ni wavumilivu, wenye ushirikiano na wanalinda kwa ukaribu sana watoto wao.” Mpokeaji wageni wa hoteli alisema kwamba kazi yake “inarahisishwa sana wakati Mashahidi wanajiandikisha wanapofika au wanapoondoka toka hoteli kwani, hata ikiwa inawapasa kufuatana kwenye mstari, wao sikuzote ni wenye adabu, wavumilivu na wasikivu.” Katika Nouvelle-Angleterre, katika Shirikisho ya Amerika, mwanamke mmoja alishangazwa sana na mwenendo wa vijana Mashahidi aliyokuwa nao katika nyumba za kupangisha; aliomba hivyo vichapo vinavyozungumzia tengenezo letu.
13 Tofauti na hilo, tunaweza kujiboresha katika hali fulani. Tungependa kuwajulisha hapa mawazo fulani yaliyotumwa kwenye Sosaiti. Mwangalizi mmoja msafiri alitufanyia ripoti kwamba watoto wa Mashahidi wa Yehova wanapaswa kulindwa zaidi. Tunawaona wakikimbia-kimbia katika njia, wakifanya fujo nyingi. Imetupasa kuelewesha watoto wetu kwamba mwenendo wa Kikristo hausimamii tu kwa saa fulani mchana. Haumaliziki tunapotoka mahali pa kusanyiko. Sisi ni Wakristo saa 24 kwa 24. Mwenendo wetu nyumbani na barabarani unapaswa pia kuwa wenye kuheshimika tunapokaa pamoja na ndugu zetu wakati wa programu, tunapopokea mafundisho ya Yehova.—Is. 54:13; 1 Pt. 2:12.
14 Ijapokuwa hakuna tena utumishi wa chakula kwenye makusanyiko, gharama kubwa zingali bado zinafanywa ili kukodisha majengo, kutayarisha nafasi za kuegesha magari na kutimiza mambo mengine mengi. Michango yetu ya kujipendea inawezesha kulipia gharama hizo. Dada mmoja ambaye watoto ni matineja alikuja kwenye kusanyiko akiwa na fedha ndogo. Hata hivyo, watoto wake na yeye mwenyewe walileta msaada wao kwa ajili ya mchango mdogo. Kile kila mmoja anaamua kufanya katika upande huo ni swala la kibinafsi, lakini tunajua kwamba mnaelewa vikumbusho hivyo.—Mdo. 20:35; 2 Kor. 9:7.
15 Tunajitambulisha kwa Namna Tunavyovaa: Namna tunavyovaa inasema mengi juu yetu na juu ya hisia za wengine. Vijana matineja walio wengi na watu wazima wengi wanakutana shuleni au kazini na watu wengi wenye kuvalia mavazi ya mtindo wa kisasa na ya ovyoovyo. Mwaka baada ya mwaka, mitindo ya mavazi inakuwa yenye kupita kiasi, na hata yenye kuchukiza. Ikiwa sisi si waangalifu, tunaweza kwa vyepesi kujiacha kushawishwa na watu wa ulimwengu walio katika ujirani wetu, na kuanza kuvaa kama wao. Mitindo mingi ya mavazi haifai kwa mikutano ya ibada. Kutokana na kusanyiko moja la mwaka jana, tulipokea barua moja ya shukrani, lakini iliongeza hivi: “Ninajiuliza kwa nini wasichana wengi walikuwa wamevalia kanzu fupi na mavazi yenye kuacha mgongo na shingo wazi na yenye kupasuliwa na kuacha mapaja wazi kabisa.’ Hakuna shaka kwamba tunatamani sote kuvaa kwa namna inayostahili wahuduma wa Kikristo, iwe kwenye kusanyiko kama vile wakati tunapojiburudisha kisha kusanyiko. Ni vizuri kutafakari kwa wakati wote juu ya shauri la mtume Paulo la kujipamba katika “mavazi yenye mpangalio mzuri, pamoja na kiasi na utimamu wa akili.”—1 Tim. 2:9, NW.
16 Nani anapaswa kujua ni nini humaanisha mavazi “yenye mpangalio mzuri” na yenye kiasi? Kuwa mwenye kiasi humaanisha kuwa na “hali isiyozidi wala kupungua, hali ya wastani katika yale tuliyo na uwezo wa kufanya.” Kamusi humwita mtu mwenye kiasi kuwa mtu “asiyejitanguliza kimbele-mbele.” Wala Sosaiti wala wazee hawapaswi kuweka kanuni kuhusu mvalio au kunyolewa. Hata hivyo, Mkristo ambaye mtindo wa mavazi sio wa kiasi wala wenye adabu je! hangepaswa kuitikia? (Ona Wafilipi 1:10.) Mavazi yetu na kunyolewa kwetu hakungepaswa kuvutia uangalifu kupita kiasi. Hali yetu ya nje inapaswa kuwa nzuri, lakini isiyofanana na ulimwengu au kuwa yenye kuchukiza. Kwa kuwa tupo wahudumu wa habari njema, tutamheshimu Yehova na tutatoa picha nzuri ya tengenezo kwa kuwa na mvalio na kunyolewa kunakofaa muda wa wakati tunaopatikana katika mji wa kusanyiko la wilaya. Hivyo, wazazi wataonyesha kielelezo (mfano) na watahakikisha kwamba watoto wao wanavaa vizuri kwa ajili ya tukio hilo. Wazee watapaswa kutoa kielelezo kizuri na watakuwa tayari kushauri kwa kirafiki ikiwa hilo linaonekana kuwa la lazima.
17 Kamera, Kameskopi na Redio Kaseti: Inawezekana kutumia kamera na vyombo vingine vya kurekodi, ikiwa tu tunawafikiria kwa adabu wahudhuriaji wengine. Ikiwa tunazunguka ili kuchukua picha wakati wa programu, si tu tutawapumbazisha wale wanaojikaza kusikiliza, lakini tutakosa pia sehemu ya kusanyiko. Kwa kawaida, tunafaidika zaidi na yale yanayosemwa kwa kuwa wenye makini sana kwa wasemaji na kuandika yanayosemwa kwa kifupi. Labda tunarekodi vipindi vya kusanyiko kwa ajili ya ndugu au dada aliyemgonjwa nyumbani kwake; hata hivyo, ikiwa ni kwa ajili ya matumizi yetu wenyewe, tutakaporudi nyumbani kwetu tutajikuta kwamba baada ya kupitisha saa nyinyi kurekodi vipindi vya kusanyiko, hatutakuwa hata na wakati wa kusikiliza au kuchunguza upya yale tuliyorekodi. Chombo chochote cha kurekodi, hata kiwe namna gani, hakipaswi kuchomekwa kwenye mkondo wa umeme au mkondo wa vikuza-sauti vya kusanyiko, wala kuzuia njia au ukumbi au kuwazuia wahudhuriaji wengine kuona.
18 Nafasi za Kukaa: Tunaendelea kuona marekebisho kuhusu kuchungiana nafasi. Mwaka jana, wahudhuriaji walio wengi walifuata agizo hili: HATUNGEPASWA KUCHUNGA VITI ISIPOKUWA TU KWA AJILI YA FAMILIA YETU YA KARIBU NA KWA WALE AMBAO TUMESAFIRI PAMOJA NAO KATIKA MOTOKAA. Kwa kuwa wengi waliitikia hivyo, uliweza labda kujisikia mwenye starehe zaidi. Jambo la lazima tena zaidi, ushirikiano wako ulimfurahisha Yehova na “mtumwa mwaminifu,” anayetoa chakula cha kiroho.—Mt. 24:45.
19 Ndugu zaidi na zaidi wana afya ambayo inaomba matunzo ya pekee. Wamoja wanakuja kwenye kusanyiko katika viti vya kusukumwa na wanahitaji wasaidiwe na washiriki wa familia zao. Wengine wanaendelea kutumia dawa za magonjwa yasiyokoma, matatizo ya moyo kwa mfano. Kwa kweli ni jambo lenye kusisimua kuona ndugu na dada hao tunaowapenda wakiwako kwenye kusanyiko, wenye kuazimia kutokosa kwa vyovyote chakula cha kiroho. Hata hivyo, ilifikia kwamba watu waligonjwa kwenye kusanyiko, wakati mshiriki mmoja wa familia yao au wa kutaniko lao hakuwapo ili kuwasaidia. Katika hali fulani, usimamizi wa kusanyiko uliweza kuita haraka utumishi wa matibabu ili kumpeleka ndugu au dada hospitalini. Daraka la kutunza wale wanaoteseka na ugonjwa fulani kwanza ni la familia yake na washiriki wa jamaa ya karibu. Utumishi wa matunzo ya msingi ya kusanyiko hauna uwezo wa kutunza wagonjwa wenye magonjwa yasiyopona. Ikiwa mshiriki wa familia yenu anahitaji matunzo ya pekee, hakikisheni kwamba hayupo peke yake, wakati hali ya dharura (haraka) ingeweza kujitokeza. Kwa upande mwingine, kwenye kusanyiko hakutatayarishwa vitambulisho vya pekee kwa ajili ya wale ambao miili yao haitikii dawa fulani zinazowazuia kukaa kwenye nafasi za kawaida. Wazee wataweza kuwa wenye makini kwa wale wote ambao, katika kutaniko lao, wanahitaji matunzo ya pekee na wataangalia kwamba mipango mizito ichukuliwe kimbele ili kuwasaidia.
20 Chakula: Kama tulivyojulishwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili, hakutakuwa na chakula kitakachohudumiwa wakati wa kusanyiko la wilaya, wala kwenye makusanyiko ya mzunguko na kwenye makusanyiko ya siku moja yatakayofuata. Mpango huo mpya ulitokeza maelezo mengi yenye kupendeza kuhusu faida zinazotokana na kila mtu kujiletea chakula chake mwenyewe. Ndugu mmoja aliandika: “Ninaona waziwazi katika mpango huo faida nyingi kwa upande wa kiroho. Wakati wote huo na nguvu zote hizo zinaweza sasa kutumiwa kwa mambo ya kiroho. Sikusikia hata elezo moja lisilofaa.” Dada mmoja alisema: “Kwa mfano, ndugu wapendwa, mnamtia moyo kila Mkristo kujichunguza na kuona jinsi ya kurekebisha maisha yake na kuongeza utendaji wake wa kitheokrasi.” Mwangalizi mmoja msafiri aliandika kuhusu utumishi wa zamani wa chakula: “Kufuatana na mpango wa zamani, hesabu kubwa ya ndugu walikuwa wakikosa kusanyiko lote.” Akisema juu ya chakula ambacho ndugu walinunua, mzee moja aliandika: “Walikuwa hasahasa na kile walichohitaji bila ya kusimama kwenye mstari.” Hatimaye, dada mwingine aliandika: “Kisha vipindi, kila mtu alikuwa mwenye kutulia na mwenye amani, na alikuwa akipumua hali nzuri.” Hakika, kila mtu angepaswa kuleta chakula cha kutosha ili kujipatia nguvu mpya kisha mchana. Wengi walionyesha kwamba walikuwa na wakati mwingi zaidi ili kuwaona marafiki.
21 Kwenye makusanyiko ya wilaya mwaka huu, hakutakuwa na utumishi wa chakula. Unaweza kuchukua dakika chache ili kuchunguza tena nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1996, fungu 8 pia kwenye mwisho wa makala, ambako tunatoa madokezo kuhusu vyakula vyenye kujenga mwili ambavyo ni rahisi kuleta kwenye kusanyiko. Kumbukeni kwamba haifai kuja na vyombo vikubwa vya barafu wala vinywaji vya kulevya. Ikiwa una lazima ya chombo kidogo cha kufanya vinywaji viwe baridi, kinapaswa kuenea chini ya kiti chako. Usisahau kwamba una wakati mwingi wa pumziko pa saa sita ili kula na kunywa kile ulichotayarisha. Kama vile kwenye mikutano ya Jumba la Ufalme, kamwe hatuli wakati wa vipindi vya kusanyiko. Tunaonyesha hivyo heshima yetu kwa mipango inayochukuliwa kwa ajili ya ibada na chakula cha kiroho tunachopokea.
22 Makusanyiko ya kwanza ya wilaya “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” yameanza sasa katika nchi fulani. Je! umechukua mipango ili kuhudhuria kwa lile la kwenu, na je! sasa wewe ni tayari kufaidika na siku hizo tatu pamoja na mashirika mazuri muda wa hizo tutapokea mambo mazuri kwa upande wa kiroho? Tunamwomba kwelikweli Yehova ili kwamba abariki bidii yako ili kuhudhuria kwenye kusanyiko wa mwaka huu.
[Box on page 6]
Kusanyiko la Wilaya—Vikumbusho
Ubatizo: Wanaojitayarisha kwa ajili ya ubatizo watakaa katika nafasi za kwanza-kwanza zinazotayarishwa kabla ya mwanzo wa programu ya Siku ya Posho asubuhi. Ilionwa kwamba wengine wana mavazi yasiyo ya heshima na yanayodharaulisha uzito wa ubatizo. Kila mwenye kujitayarisha kwa ajili ya ubatizo ataleta mavazi ya kuoga nayo yenye kustahili na taulo (nguo ya kujipanguza baada ya kuoga) Wazee watakaochunguza maulizo yanayopatikana katika kitabu Huduma Yetu pamoja na wale wanaojitayarisha kwa ajili ya ubatizo watahakikisha kwamba kila mmoja wao anaelewa vizuri nukta hizo. Msemaji atakapomaliza kutoa hotuba ya ubatizo na sala, msimamizi wa programu atatoa maagizo mafupi kwa wanaojitayarisha kubatizwa, kisha ataimbisha wimbo. Kisha kifungu cha mwisho cha wimbo, wanamemba wa idara ya ukaribishaji watawaongoza wale watakaobatizwa kwenye nafasi ya ubatizo. Kwa kuwa ubatizo ni kielelezo cha wakfu wetu ni swali la kibinafsi kati ya mtu mwenyewe na Yehova, haikusudiwi kufanya “ubatizo wa vikundi” vya watakaobatizwa wawili wawili au zaidi ambao wangeshikana mikononi mmoja na mwingine au ambao wangeshikana mkono wakati wa ubatizo.
Alama: Tafadhali vaa alama kwa ajili ya 1996 iwe kwenye kusanyiko kama vile katika safari ya kwenda na kurudi. Hilo linawezesha mara nyingi kutoa ushuhuda bora. Utajipatia alama kwa njia ya kutaniko lenu, kwani hazitapatikana kwenye kusanyiko. Usingoje siku zinazotangulia kusanyiko ili kuomba alama kwa ajili yako na familia yako. Usisahau kuwa na kadi yako “Instructions médicales — Pas de sang.”
Utumishi wa Wenye Kujipendea: Kwa kuwa sasa hakuna utumishi wa chakula, wengi waliokuwa wafanyakazi wa kujipendea katika utumishi huo watatamani labda kuwa wenye manufaa mahali pengine. Je! unaweza kuweka wakati mdogo muda wa kusanyiko ili kutoa msaada wako katika mojawapo ya utumishi kadha? Tunapaswa kuwa wenye manufaa sana na kujipatia uradhi mwingi tunapotumikia ndugu zetu, haidhuru saa chache tu. Ikiwa unaweza kutoa msaada wako, tafadhali fika kwenye utumsihi wa wafanyakazi wa kujipendea wa kusanyiko. Watoto wa chini ya umri wa miaka 16 wanaweza kutimiza sehemu yao kwa namna iliyo bora kwa kutumika chini ya uongozi wa baba zao, wa mama zao au wa mtu mzima mwingine.
Angalisho: Tuwe wepesi kutambua iwezekanavyo magumu ili kuepuka matatizo yasiyofaa. Mara nyingi, wale ambao hawapatikani katika mazingira (mahali) yao ya asili ndio wanaoshambuliwa na wevi na watu wengine wasio na dhamiri. Tafadhali funga sikuzote vizuri milango ya motokaa yako na kutoacha kamwe kitu chochote waziwazi kinachoweza kushawishi macho. Wevi na wachomoaji vitu mifukoni wanavutiwa na makusanyiko makubwa. Halingekuwa jambo la hekima kuacha kitu cha thamani juu ya kiti chako. Hauwezi kuwa hakika kwamba wote wanaokuzunguka ni Wakristo. Kwa nini kumtia mtu mwingine katika jaribu? Tulipokea ripoti zinazoonyesha kwamba watu wasiojulikana walijaribu kuvuta watoto nje. USISAHAU KAMWE WATOTO WAKO.