“Imani Katika Neno La Mungu” —Kusanyiko La Wilaya 1997
1 Mtume Paulo alimkumbusha Timotheo kwamba “andiko lote limepuliziwa na Mungu.” (2 Tim. 3:16, TUM) Neno la Mungu likiwa lenye kupuliziwa (kuongozwa), tunazo sababu zote za kujizoeza imani ndani yalo. Mwaka huu, kusanyiko la wilaya litakuwa na kichwa cha habari “Imani Katika Neno la Mungu.” Iwe tumeujua ukweli tangu miaka mingi au kwamba ni karibuni tu tumekuja kwenye tengenezo la Yehova, programu itajenga imani yetu katika Biblia. Kila mmoja wetu angepaswa kupanga mambo yake ili kuhudhuria kwenye kusanyiko lote. Lingekuwa jambo lenye kutia moyo kama nini kwamba watu wanaoonyesha kupendezwa tangu hivi karibuni wawepo pamoja nasi, hasa wale tunaojifunza nao Biblia!
2 Kusanyiko la Siku Tatu: Mwaka huu, kusanyiko la wilaya la siku tatu lilipangwa kwa faida yetu. Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 1997 inatoa orodha ya makusanyiko 53 ambayo yatafanyika Burundi, Congo na katika Zaïre. Kwa sasa, unajua kusanyiko ambalo kutaniko lenu linaalikwa kwalo na ungepaswa kuwa umekwisha kuchukua mipango kamili ili kuwako muda wa siku tatu. Je! umemuomba bwana wako wa kazi likizo ya kutosha? Ikiwa una watoto wa umri wa kwenda shule, je! umewajulisha kwa heshima walimu wao kwamba hawatakuwapo Siku ya Tano kwa sababu ya tukio la maana katika mazoezi yao ya kidini?—Kumb. 31:12.
3 Kila siku, kusanyiko litaanza pa saa 3:30. Milango itafunguliwa saa 2:00. Ni wale peke yao walio na kazi ya kutimiza wataruhusiwa kuingia mapema zaidi, lakini si kuchungiana nafasi kabla ya kufunguliwa kwa mahali kwa watu wote.—Flp. 2:4.
4 Tunafanya Vema Kukazia Uangalifu: Katika karne ya kwanza, mtume Petro aliwakumbusha Wakristo kwamba wangefanya vema kukazia uangalifu neno la unabii kama vile kwa taa yenye kung’aa katika mahali penye giza. (2 Pt. 1:19) Hilo ni kweli pia kwetu. Tukiwa wenye kuishi katika ulimwengu ulio chini ya uwezo wa Shetani, tupo kama vile katika mahali penye giza. Sisi ni wenye shukrani kuweza kuitwa kutoka giza la kiroho. (Kol. 1:13; 1 Pt. 2:9; 1 Yn. 5:19) Ili kubaki katika nuru, imetupasa kulinda imani yenye nguvu kwa kukazia uangalifu kwenye Neno lililopuliziwa na Yehova. Ni hilo hasa jambo ambalo kusanyiko letu la wilaya lijalo litatuchochea kwalo.
5 Ikiwa tunataka kukaza akili kikiki juu ya kusanyiko, itatupasa labda kufanya bidii, lakini bila shaka yoyote tutabarikiwa ikiwa tunafanya hivyo. Tuangalie ili kwamba tupumzike vizuri, jambo ambalo litatuwezesha kusikiliza kwa makini sehemu mbalimbali za programu. Tuweke kila siku wakati wa kutosha ili kujielekeza kwenye kusanyiko hivi kwamba tuweza kukaa kabla ya programu kuanza. Kisha tushiriki wimbo wa kufungua na tufaidike na sala. Watu wazima wangepaswa kutoa kielelezo, na wazazi wangepaswa kutayarisha watoto wao juu ya kusanyiko.—Efe. 6:4.
6 Ikiwa tunachunguza mapema programu ya hotuba za siku, tunaweza kujaribu kufikiria labda mawazo hayatakayokaziwa. Hilo litaongeza kupendezwa kwetu wakati ambapo mawazo hayo yatatolewa. Tunaweza kuwa chonjo juu ya nukta zitakazotolewa kufasiria kwa jirani sababu zinazotufanya tuamini katika Mungu na katika ahadi yake iliyo hakika ya kuwadhawabisha wale wanaomtafuta kwelikweli. (Ebr. 11:1, 6) Tunaombwa kuandika mambo makuu ya kusanyiko kwa kifupi. Ikiwa tungeandika mambo mengi sana, kungekuwa hatari ya sisi kupitwa na mambo makuu, huku tukiwa wenye kushughulika sana kuandika mambo.
7 Mwaka wa nyuma, tuliona wakati programu ilipokuwa ikiendeshwa hesabu ya kutosha ya watu wazima na vijana wakitembea-tembea kwa uzembe katika njia ndogo, wakizurura-zurura nje na kuzungumza-zungumza na watu wengine, badala ya kusikiliza yale “mtumwa mwaminifu na mwenye akili” alitayarisha kwa faida yetu. Yesu aliahidi kututolea chakula cha kiroho kwa wakati ufaao. (Mt. 24:45-47) Kwa hiyo, tungepaswa kuwapo ili kufaidika zaidi na chakula hicho, na si kukosa shukrani. (2 Kor. 6:1) Inaonekana pia kwamba watoto wanakosa uvumilivu na wanaomba kwenda kila mara chooni, wakiwa hivyo na kisababu ili kusimama na kutembea-tembea. Malezi yanayofaa yanayotolewa nyumbani yatawezesha kwa ujumla kuepuka kwenda mara kwa mara chooni na kusinzia wakati wa programu. Mara nyingi, matineja wanakaa kikundi wakijitenga kidogo, wanazungumza-zungumza, wananong’ona-nong’ona na kuandikiana maneno madogo wanayopeana. Katika siku zetu, vijana wetu wanapatwa na mavutano na wanahitaji kukaza akili kikiki juu ya mafundisho wanayotolewa, bila kufanya mambo mengine wakati programu inapoendeshwa. Inawapasa kutupilia mbali tamaa zenye kutukia hasa ujanani zisizolingana na kanuni za Biblia. (Ona 2 Timotheo 2:22.) Uangalifu wa wote, watu wazima na walio vijana zaidi, utamheshimisha Yehova na kumfurahisha.
8 Ikiwa ingeonekana kuwa lazima kwamba mwanamemba mmoja wa idara ya ukaribishaji amtolee mtu fulani shauri juu ya hilo, ingefaa kuliona kama alama ya upendo unaotoka kwa Yehova. (Gal. 6:1) Kila mmoja anapaswa kukumbuka kwamba ikiwa anafanya bidii ili kuhudhuria kwenye kusanyiko, ni ili ‘kusikiliza na kujifunza.’ (Kumb. 31:12) Zaidi ya hilo, “mwenye hekima [husikia] na kuongezewa elimu.” (Mez. 1:5) Tangu sasa na kufikia kwenye kusanyiko, tuzungumze katika familia juu ya ulazima wa kukaa pamoja, wa kubaki pa nafasi yetu wakati wa kuendeshwa kwa programu na kuwa wenye makini sana katika kusudi la kufaidika kikamilifu na programu.
9 Mvalio Unaompendeza Yehova: Wale wanaounda taifa la watu wa Yehova wanawekwa hadharani wakitazamwa na ulimwengu mzima. (1 Kor. 4:9) Kwa ujumla, tunajulikana kwa namna yetu nzuri ya kuvaa na kunyolewa. Wengi wa wale wanaotumikisha kanuni za Maandiko zinazotajwa katika 1 Timotheo 2:9, 10 na katika 1 Petro 3:3, 4 waliona utu wao wa nje umebadilika kabisa kabisa wakilinganisha na wakati walipoanza kushirikiana na kutaniko la Kikristo. Hilo linaonyesha tofauti iliyo wazi na upotovu wenye kuendelea ambao tunaona katika namna ya kuvaa na kunyolewa ya ulimwengu. Tunataka kubaki chonjo (waangalifu) ili kutofanana na ulimwengu kwa kuvalia mavazi ya ajabu-ajabu, kwa kutegemeza mtindo fulani kwa kunyolewa kwetu au kwa kuwa na mavazi yanayokosa kiasi. Mavazi yetu na kunyolewa kwetu kungepaswa kuwa kielelezo ili kuwasaidia wapya wanaohudhuria kwenye kusanyiko kuelewa jinsi mavazi ya Wakristo yanapaswa kuwa.
10 Maoni kwa ujumla yaliyoachwa mwaka wa nyuma kwenye makusanyiko yalikuwa mazuri kabisa; hata hivyo, akina ndugu na dada fulani bado wana mavazi na namna ya kunyolewa ambayo ni ya ulimwengu kabisa, na hasa wakati wa vipindi vyao vya vidumbwizo. Tunapofanya miradi ili kuhudhuria kwenye kusanyiko, tungepeswa kuchunguza mavazi yetu na kunyolewa kwetu. Enyi wazazi, chagueni kwa hekima kile watoto wenu wenye umri wa chini au matineja watavaa. Hakikisheni kwamba haturuhusu mitindo pekee ya ulimwengu au shauku yake yenye wazimu kuwa na uvutano mbaya juu ya utu wetu wa nje wa Kikristo.
11 Tudumishe Mwenendo Bora: Mwenendo bora ni alama ya Wakristo wa kweli. (1 Pt. 2:12) Haidhuru tuwe mahali gani, kwenye kusanyiko, kwenye mkahawa, kwenye hoteli na wakati wa matembezi yetu, mwenendo wetu unaweza kutoa ushuhuda na kuwasaidia watu kuona yale imani katika Mungu na katika Neno lake inaweza kutokeza. Hilo linaweza kuwaongoza wamoja kutamani kumjua Yehova. (Ona 1 Petro 3:1, 2.) Tunalo pendeleo la kumtukuza Yehova kwa mwenendo wetu.
12 Tunakumbushwa mara kwa mara kuangalia mwenendo wa watoto wetu, kutokuwaacha bila uangalizi wala kukimbia-kimbia mahali pote katika mahoteli (au mahali ambapo tunapangishwa), jambo ambalo linavuruga wageni wengine. Kila mwaka, Sosaiti inapokea habari kwamba wamoja wa watoto wetu wako pasipo uangalizi. Hata ikiwa kusanyiko linatutolea nafasi ya kuwaona ndugu zetu na kukusanyika pamoja nao, wazazi hawapaswi hata hivyo kusahau mapaswa yao ya kuangalia watoto wao kila wakati. Ni daraka ambalo Yehova amekabizi kila baba na mama. (Mez. 1:8; Efe. 6:4) Matendo yanayofanywa na watoto wanaoachwa pasipo uangalizi yanaweza kuharibu sifa nzuri ambayo Mashahidi wa Yehova wengine walijifanyia kwa bidii yao nyingi.—Mez. 29:15.
13 Tulipie Gharama Zinazofanywa kwa Ajili ya Kusanyiko: Tunagharimu sote fedha ili kuhudhuria kwenye makusanyiko. Kuna gharama nyingine ambazo tungefanya vema kufikiria. Majengo yanayotumiwa kwa ajili ya makusanyiko yanakodiwa kwa bei ghali. Kuna pia gharama nyingine za kutimiza. Michango karimu ya kujipendea ambayo mnafanya wakati wa makusanyiko ni yenye kuthaminiwa sana.—Mdo. 20:35; 2 Kor. 9:7, 11, 13.
14 Nafasi za Kukaa: Maagizo yaliyotolewa muda wa miaka ya nyuma ni sikuzote halali: HATUNGEPASWA KUCHUNGIANA VITI ISIPOKUWA TU KWA AJILI YA FAMILIA YETU YA KARIBU NA KWA WALE AMBAO TUNASAFIRI NAO KATIKA MOTOKAA. Ni jambo lenye kufurahisha kuona kwamba, miaka hii ya nyuma, wahudhuriaji zaidi na zaidi wanaheshimu mwongozo huo, jambo ambalo linainua mazingira yenye kujaa upendo yanayotawala katika makusanyiko yetu. Katika mahali pengi ambako kunafanyika makusanyiko, ni rahisi zaidi kufika nafasi fulani za kukaa kuliko nyingine. Tafadhali iweni wenye huruma kwa kuacha nafasi nzuri zaidi kwa wale ambao hali yao inaruhusu hivyo.
15 Vyombo vya Kupiga Picha, Kameskopi na Redio Kaseti: Inawezekana kutumia vyombo vya kupiga picha na vyombo vingine vya kunasa sauti. Hata hivyo, hatupaswi kupumbaza wahudhuriaji wengine tunapovitumia. Hatungepaswa kutembea-tembea wakati programu inapoendeshwa ili kupiga picha, kwani kuna hatari kuvuruga wengine wanaojikaza kusikiliza. Hakuna chombo chochote cha kunasa sauti, haidhuru kiwe ni gani, kinachopaswa kuchomekwa kwenye singa za umeme au kwenye mtambo wa vikusa-sauti wa kusanyiko, wala kuzuia njia au mapitio (ukumbi) au kwenye eneo la kuona la wahudhuriaji wengine.
16 Matibabu ya Kwanza: Idara ya matibabu ya kwanza inatumika tu katika hali ya dharura. Haina uwezo wa kutunza watu wanaopatwa na magonjwa yasiyopona. Ni kwa sababu hiyo ungepaswa kufikiria mbele ya wakati matibabu yanayohitajiwa na afya yako na ile ya washiriki wa familia yako. Tafadhali chukua asprini yako, dawa zako za kusafisha tumbo, vitambaa vyako vya vidonda, pini zako za watoto na mambo mengine kama hayo yasiyopatikana pa nafasi ya kusanyiko. Wale wote walio na matatizo ya ugonjwa wa moyo, ambao kuna hatari wapatwe na mshtuko wa insilini, n.k., wanapaswa kwa kadiri yote iwezekanayo kuchukua mipango ya kujilinda mbele ya wakati. Wangepaswa kuwa na dawa za lazima, na mshiriki mmoja wa familia yao au wa kutaniko lao anayejua hali yao angepaswa kuwa pamoja nao ili kuwasaidia wakati wa uhitaji. Ilifikia kwamba kwenye makusanyiko watu wenye magonjwa yasiyopona walioachwa wenyewe walipatwa na mshtuko wa ghafula, jambo ambalo lilitokeza matatizo. Idara ya usimamizi ililazimika kuita idara ya dharura (usaidizi wa haraka) ili kuwapeleka kwenye hospitali. Ikiwa mtu anahitaji matibabu ya pekee na kwamba hakuna mshiriki wowote wa familia yake anayeweza kushughulika naye, wazee wa kutaniko lake watapaswa kujulishwa juu ya hali na watapaswa kuchukua mipango ya lazima ili kumsaidia. Hakutatayarishwa vyumba vya pekee kwa ajili ya wale ambao miili yao haitikii hali au dawa fulani.
17 Chakula: Kuondolewa kwa idara ya chakula kunawezesha kukaza akili kikiki zaidi juu ya chakula cha kiroho wakati wa kuendeshwa kwa programu. Tangu hapo, tumepokea wonyesho wa shukrani nyingi kwa ajili ya marekebisho hayo. Kila mmoja angepaswa kutayarisha vyakula vyenye kujenga mwili ambavyo inawezekana kuvichukua kwa ajili ya pumziko la saa sita. Hatutaingia ndani ya mahali patakapofanyika kusanyiko pamoja na machupa ya bilauri wala pamoja na vinywaji vya kulevya. Vyombo vikubwa vya kulinda barafu vinapaswa kuwa vidogo sana ili kuweza kuingia chini ya kiti chako. Wahudhuriaji walionekana wakila chakula wakati programu inapoendeshwa. Huko ni kukosa heshima. Kwenye makusanyiko mengine, ndani ya majengo au nje kulikuwako nafasi za wachuuzi wa rejareja (mambo madogo-madogo), na ilionekana kwamba ndugu walikuwa wakienda huko ili kununua vyakula wakati programu inapoendeshwa. Hilo halifai.
18 Tunathamini sana sikukuu yetu ya kiroho na hali ya starehe na ya amani ya undugu wakati wa mapumziko ya saa sita. Kupatana na kusudi hilo la mpango huo, tafadhali leta chakula chako mwenyewe, badala ya kutoka mahali pa kusanyiko ili kwenda kununua chakula. Utakuwa hivyo na wakati zaidi ili kufurahia ushirika wa ndugu na dada zako.
19 Tunashangilia kama nini kwa kufikiria kusanyiko la wilaya “Imani Katika Neno la Mungu” linalokaribia sasa! Sisi sote tunataka kuwa hakika kwamba tulichukua mipango ili kuhudhuria kwenye programu yote, ili kufaidika na karamu nono ya kiroho ambayo Yehova alitutayarishia kupitia tengenezo lake. Hilo litatuwezesha kuwa wenye ‘kuandaliwa vifaa kikamili kwa ajili ya kila kazi njema’ katika siku zijazo.—2 Tim. 3:17, TUM.
[Box on page 6]
Kusanyiko la Wilaya—Vikumbusho
Ubatizo: Wanaojitayarisha kwa ajili ya ubatizo watakaa katika nafasi za kwanza-kwanza wanazotayarishiwa kabla ya mwanzo wa programu ya Siku ya Posho asubuhi. Kila mwenye kujitayarisha kwa ajili ya ubatizo ataleta mavazi ya kuoga nayo yenye kustahili na taulo (nguo ya kujipanguza baada ya kuoga). Wakati wa nyuma, wamoja walikuja na mavazi yasiyo ya heshima na yaliyoharibu sifa ya uzito wa tukio hilo. Wazee watakaochunguza maulizo yanayopatikana katika kitabu Huduma Yetu pamoja na wale wanaojitayarisha kwa ajili ya ubatizo watahakikisha kwamba kila mmoja wao anaelewa vizuri nukta hizo. Msemaji atakapomaliza kutoa hotuba ya ubatizo na sala, msimamizi wa programu atatoa maagizo mafupi kwa wanaojitayarisha kubatizwa, kisha ataimbisha wimbo. Kisha kifungu cha mwisho cha wimbo, wanamemba wa idara ya ukaribishaji watawaongoza wale watakaobatizwa kwenye nafasi ya ubatizo. Ubatizo kama vile wonyesho wa wakfu wetu ni ulizo la kibinafsi kati ya mtu na Yehova. Haikusudiwi hivyo kufanya “ubatizo wa vikundi” vya wawili pamoja au zaidi vya watakaobatizwa ambao wangeshikana mikono wakati wa ubatizo.
Alama: Tafadhali vaeni alama kwa ajili ya mwaka 1997 iwe kwenye kusanyiko kama vile katika safari ya kwenda na kurudi. Hilo linawezesha mara nyingi kutoa ushuhuda bora. Mtajipatia alama na mifuko yake kupitia kutaniko lenu, kwani hazitapatikana kwenye kusanyiko. Usingoje siku zinazotangulia kusanyiko ili kuomba alama kwa ajili yako na familia yako. Usisahau kuwa na kadi yako “Instructions médicales — Pas de sang”.
Upangishaji: Tunaomba kwa wote ushirikiano kwa kutumia TU orodha ya nafasi za kupangishwa inayotolewa na Afisi ya kusanyiko. Ikiwa ndugu wa mahali wanatupangisha, hatungepaswa kutumia vibaya ukarimu wao kwa kubaki kwao muda mrefu kisha kusanyiko. Hata wakati kusanyiko linapoendeshwa, hakuna yeyote angepaswa kufikiri kwamba wale wanaotukaribisha ndio watatutolea chakula. Wamoja hawana uwezo wa kufanya hivyo. Tuweze kwa hiyo kujitayarisha tangu sasa ili kubeba kile tutakachokula wakati wa kusanyiko. Mwandishi wa kutaniko ataangalia kwamba Maombi ya chumba kwa watu pekee yatumwe haraka kwa anwani ya kusanyiko linalohusika. Ikiwa inawapasa kufuta mpango wa kuchungia mtu fulani chumba cha pekee, julisha hilo mapema kwa yule anayeshughulika na kupangisha watu au kwenye hoteli na pia kwenye idara ya upangishaji ya kusanyiko, hivyo kwamba chumba kiweze kutolewa kwa mtu mwingine.
Viti vya Kusukumwa na vya Kukunjwa: Katika mahali pengi, inakatazwa kutumia viti vya kusukumwa wakati wa makusanyiko ya peupe. Kanuni za ulinzi haziruhusu kwamba viti hivyo viachwe katika kumbi, katika vinjia au kati ya misafara ya viti. Kwa kuwa umati mkubwa unaweza kutokeza misongamano, viti vya kusukumwa vinakuwa hatari iwe kwa watoto kama vile kwa wale watakaoweza kujikwaa kwavyo. Tafadhali msiweze hivyo kuvileta kwenye mahali pa kusanyiko. Hata hivyo, viti vya watoto au viti vya motokaa vinaruhusiwa, kwani wazazi wanaweza kuvichomeka kwenye kiti pembeni yao. Tafadhali msilete pia viti vya kukunjwa. Vinaweza kuwa hatari na hairuhusiwi kuvitumia wakati wa makusanyiko makubwa ya peupe. Ushirikiano wenu katika mambo hayo mawili ni wa lazima na unathaminiwa.
Utumishi wa Wenye Kujipendea: Je! unaweza kujiwekea muda mchache wakati wa kusanyiko ili kutoa msaada wako katika mojawapo ya idara mbalimbali? Tunaweza kuwa wenye thamani sana na kujipatia uradhi mkubwa ikiwa tunahudumia ndugu zetu, hata tu kwa muda wa saa chache. Ikiwa unaweza kutoa msaada wako, tafadhali kwenda kujionyesha kwenye idara ya wafanyakazi wa kujipendea ya kusanyiko. Watoto wa chini ya miaka 16 wanaweza pia kushiriki kwa namna iliyo nzuri kabisa kwa kutumika chini ya uongozi wa baba zao, wa mama zao au wa mtu mzima mwingine mwenye madaraka.
Angalisho: Tuwe wepesi kutambua iwezekanavyo magumu ili kuepuka matatizo yasiyofaa. Mara nyingi, wale ambao hawapatikani katika mazingira yao ya asili ndio wanaoshambuliwa na wevi na watu wengine wasio na dhamiri. Hakikisha sikuzote kwamba milango ya motokaa yako inafungwa kwa ufunguo na usiache kamwe kitu chochote waziwazi kinachoweza kushawishi macho. Wevi na wachomoaji vitu mifukoni wanavutiwa na makusanyiko makubwa. Halingekuwa jambo la hekima kuacha kitu cha thamani juu ya kiti chako. Hauwezi kuwa hakika kwamba wote wanaokuzunguka ni Wakristo. Kwa nini kumtia mtu mwingine katika jaribu? Tulipokea pia ripoti kwamba watu wasiojulikana walijaribu kuvuta watoto nje. USISAHAU KAMWE WATOTO WAKO.
Itafaa pia kuangalia ili kwamba misiba iepukike. Wakati wa nyuma, akina ndugu walipandia motokaa kwa uwingi au mitumbwi bila kujali uwezo wa vyombo hivyo. Kulitokea misiba mikubwa. Kwa kuwa uhai ni mtakatifu, tunataka kuwa waangalifu kwa kuepuka kujitwika deni ya damu. Kwa kuvuka barabara, inafaa kuwa hakika kwamba hakuna gari linaloweza kutugonga sisi wenyewe au watoto wetu.
Ni Julai 11, 1997 ndipo linaanza kusanyiko la wilaya la kwanza “Imani Katika Neno la Mungu.” Tunamuomba Yehova kwa unyofu wa moyo kubariki bidii yetu ili kuhudhuria mfululizo huo wa makusanyiko ya wilaya na kulishwa mambo mazuri kwenye meza Yake.