Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/99 uku. 3-6
  • Makusanyiko ya Wilaya 1999 “Neno la Unabii la Mungu”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Makusanyiko ya Wilaya 1999 “Neno la Unabii la Mungu”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kabla ya Kusanyiko
  • Wakati wa Kusanyiko
  • “Njia Ya Mungu Huongoza Kwenye Uzima”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • “Imani Katika Neno La Mungu” —Kusanyiko La Wilaya 1997
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • “Wajumbe wa Amani ya Kimungu”—Kusanyiko la Wilaya 1996
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kipindi cha Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 5/99 uku. 3-6

Makusanyiko ya Wilaya 1999 “Neno la Unabii la Mungu”

1 Waisraeli walipokuwa karibu kuingia katika Bara Lililoahidiwa, Musa aliwasihi wathamini maagizo ya Mungu. Aliwaambia: “Si kitu bule kwenu; maana ni maisha yenu.” (Kum. 32:45-​47) Je! sisi si wenye shukrani kwa Yehova kuona kwamba uhai wetu ni wenye thamani kwake hivi kwamba anaendelea kutuongoza kupitia Neno lake lenye thamani sana? Kwa hiyo, tunatazamia kwa hamu lile Kusanyiko la Wilaya la siku tatu “Neno la Unabii la Mungu” na yale ambayo Yehova anatuwekea.

2 Mwaka huu, makusanyiko ya wilaya yanapangwa ifaavyo katika miji 59 kuzunguka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Programu ya kusanyiko itaongozwa katika Kifaransa, Kiluba, Kiswahili, Lingala, Monokutuba, Otetela, Tshiluba na Uruund. Kutakuwako pia programu katika Lugha ya Ishara kwa ajili ya viziwi katika mji wa Kinshasa.

3 Bila shaka umekwisha kufanya mipango ili uhudhurie kila siku ya kusanyiko kwa kuwa unasadiki kwamba Yehova atazamia uhudhurie. Uwe hakika kwamba yeye aona jitihada na kujinyima wanavyofanya watumishi wake ili wahudhurie, na anawakumbuka wale walio wenye shukrani. (Ebr. 6:​10) Kwa kuhudhuria kila siku ya kusanyiko, kutoka wimbo wa kwanza hadi sala ya mwisho, tunamwonyesha Yehova kwamba tunathamini maneno yake kwetu. (Kum. 4:​10) Tunaonyesha pia uthamini kwa kazi ngumu ya ndugu zetu wengi wanaohusika na kutayarisha kusanyiko.

4 Kufanya mipango ili maelfu ya watu wa Mungu wakusanyike mahali pa kusanyiko kwaomba matayarisho ya kimbele na upangaji-mambo mzuri. Kujua kwamba mipango kwa ajili ya kusanyiko imefanywa kwa upendo kwa ajili yetu kwatusukuma tushirikiane, ili “mambo yote yatukie kwa adabu na kwa mpango.” (1 Kor. 14:40) Habari na vikumbusho vifuatavyo vinaandaliwa ili ufike kwenye kusanyiko lako ukiwa mwenye kujitayarisha kikamili ili kufurahia chakula cha kiroho na ushirika wa Kikristo.

Kabla ya Kusanyiko

5 Je! wale unaojifunza Biblia pamoja nao na wengine wenye kupendezwa wanahitaji msaada ili kufanya matayarisho ya binafsi kwa ajili ya kuhudhuria? Yale wanayoyaona na kusikia yanaweza kuwachochea wawe waabudu wa Yehova. (1 Kor. 14:25) Wazee wangepaswa kujua mtu yeyote anayehitaji msaada kuhusiana na upangishaji au usafirishaji, zaidi sana washiriki wazee-wazee wa kutaniko, na kuangalia kwa upendo kwamba mahitaji yao yatimizwe.​—Gal. 6:​10.

6 Je! mipango yako kwa ajili ya kupata makao imekamilishwa? Ikiwa uliazimia kukaa pamoja na akina ndugu muda wa kusanyiko, je! umejaza fomu ili kupewa chumba? Je! umeonyesha hesabu ya watoto watakaokusindikiza, ikiwa unao? Mwandishi angepaswa kutuma, haraka iwezekanavyo, kwenye mji wa kusanyiko maombi yote yenye kukubaliwa na Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Ni jambo la maana kwamba akina ndugu watakaotoa ukaribishaji wao wajulishwe mapema ili wajitayarishe kupokea wageni wao.​—1 Kor. 14:40.

7 Kwa kuwa Idara ya Msaada wa Kwanza kwenye kusanyiko imewekwa ili kushughulikia hali za dharura tu, tunapendekeza kwamba mlete kwenye kusanyiko vidonge vyenu wenyewe vya aspirini, bendeji, vyombo vya kusaidia kupisha dawa puani au kooni, madawa ya kutuliza tumbo, na vifaa vingine kama hivyo ikiwa mwafikiri kwamba vyaweza kuhitajiwa. Ikiwa wewe au mpendwa anayo hali ngumu yenye kuendelea, kama vile tatizo la moyo, ugonjwa wa kisukari, hatari ya kuzimia, tafadhali leta kwenye kusanyiko dawa inayohitajiwa ili kushughulikia mahitaji hayo. Lingekuwa jambo lenye hekima kwamba mshiriki wa familia au rafiki wa karibu anayeelewa hali abaki na mtu yule kila wakati, kwa kuwa yeye angeweza kuwa katika hali inayofaa zaidi ili kutoa msaada wenye kuhitajiwa.

8 Nafasi za kutoa ushahidi wa vivi hivi huenda zitajitokeza unaposafiri kwenda au kurudi kutoka kwenye kusanyiko. Je! utakuwa mwenye kujitayarisha ili kushiriki kweli na wengine? Sisi sote, kutia ndani watoto wadogo, twaweza kuhusika kwa kutoa trakti kwa watu tunaowakuta wakati wa kusafiri kwa mguu, kwa mashua, kwa gari au kwa gari-moshi. Njiani, tunaposimama kwenye soko, tunaweza pia kutoa ujumbe kupitia vichapo. Kutakuwako nafasi za kuacha magazeti, broshua au vichapo vingine kwa watu wenye kupendezwa. Uwe tayari kutoa ushahidi wa vivi hivi kwa watu ambao huenda hawapatikani tunapotumia njia nyinginezo za mahubiri. Ikiwa unavaa alama-kitambulisho yako unapokwenda kwenye kusanyiko, jambo hilo litakupa nafasi nyingi za kutoa ushahidi.

Wakati wa Kusanyiko

9 Kila siku, milango itafunguliwa kwenye nafasi ya kusanyiko pa saa 2:00 asubuhi. Unaweza kuchunga viti kwa ajili ya familia yako ya karibu tu au kwa ajili ya wale wanaosafiri katika gari lako. Viti vyenye kufaa vitawekwa kwa ajili ya ndugu na dada wazee-wazee, na mahali patawekwa kando kwa ajili ya wale wasiojiweza au wale wanaoomba mahali pa kufikiwa na viti vya magurudumu. Tunataka kuwaonyesha staha na wema. Kila siku, utakapoondoka kwenye kiti chako, tafadhali angalia ili uhakikishe kwamba unavyo vitu vyako vyote.

10 Je! utabatizwa kwenye kusanyiko la wilaya? Kwa ajili ya kipindi cha kusanyiko cha Siku ya Posho asubuhi, sehemu fulani ya viti itawekwa kwa ajili ya wale wanaotaka kubatizwa, na wahudumu watakuongoza mahali hapo. Ikiwa kwa vyovyote inawezekana, tafadhali uwe mwenye kukaa hapo kabla ya kipindi cha kusanyiko kuanza. Leta Biblia yako, kitabu chako cha nyimbo, kitambaa cha kupangusa maji, na nguo ya kuoga nayo yenye kufaa. Kaputula zilizofanywa kwa kukata suruali za jini (jean), mipira yenye maneno ya kuvumisha biashara, na mavazi yenye kufanana na hayo si yenye kufaa kwa ajili ya tukio hilo lenye kutukuka. Wazee watakaorudilia maulizo katika kitabu Huduma Yetu pamoja na wale wanaotaka kubatizwa wanapaswa kuhakikisha kwamba kila mmoja aelewa mambo hayo. Kwa kuwa ubatizo ni alama ya wakfu wa mtu binafsi kwa Yehova Mungu, halingekuwa jambo lenye kufaa kwa wale wanaotaka kubatizwa kushikana mikono watakapokuwa wakibatizwa.

11 Kwenye kusanyiko, mnaweza kutumia kamera, kameskopi, na vyombo vya kurekodi kwenye kaseti za kusikiliza. Hata hivyo, vyombo hivyo havingepaswa kuwekwa kwa namna ya kufunga vipito, kuzuia wengine wasione, au kupotosha uangalifu wa wengine wasifuate programu. Havipaswi kuunganishwa na mfumo wa umeme au wa sauti.

12 Ili kukomboa wakati na kurahisisha mambo, Sosaiti imetuomba tulete chakula chetu wenyewe chepesi kila siku kwenye kusanyiko. Akina ndugu wengi wamefuata mwongozo huo na wameona kwamba, baada ya kutawanyika kwa ajili ya pumziko la saa sita, wanaweza kukaa pamoja na familia zao na kula kile walicholeta kwa ajili ya siku ile. Wamesema kwamba nafasi ya kujiburudisha muda wa pumziko la saa sita na kupitisha wakati wa ziada pamoja na ndugu na dada zao umekuwa wenye kufurahisha. Jambo hilo laomba kununua vyakula na vinywaji mbele ya wakati na kuvipakiza katika kitu kidogo au chombo cha kutia vyakula baridi ambacho kinaweza kuenea chini ya kiti. Tunaomba wahudhuriaji wote wafuate mwongozo huo. Hivi karibuni, wachuuzi wa vyakula katika makao ambako makusanyiko yetu hufanyika wameona ndugu fulani wakiondoka mahali wasikilizaji walipokaa ili kununua chakula katika nyumba za karibu ambako vyakula huuzwa. Sasa, baadhi ya wachuuzi wa vyakula katika makao ya kusanyiko yaliyotumiwa ni wenye kuomba waruhusiwe kufungua mahali pa kuuzia vyakula na kuhudumia wajumbe wanaohudhuria makusanyiko yetu. Ikiwa jambo hilo lingeruhusiwa, watu wengi wa ulimwengu wangechanganyika katika ushirika pamoja nasi muda wa siku. Pia, songamano na mistari mirefu mahali palipo vitu vya kuuza vingerudia, vikivuruga hali yenye kuburudisha ya makusanyiko yetu. Kwa hiyo, tunaomba kila mtu ajitahidi kuleta chakula na kinywaji chake mwenyewe kwenye kusanyiko kila siku. Wale wenye kupendezwa wanaokusindikiza kwenye kusanyiko wangepaswa pia kuleta chakula chao wenyewe. Vyombo vya kuwekea bilauri na vinywaji vya alkoholi haviruhusiwi katika makao ya kusanyiko.

13 Je! unaweza kujitolea kwa kujitakia ili kusaidia kusafisha makao baada ya vipindi vya kusanyiko kila siku? Au je! ungeweza kutumika katika moja ya idara zile nyingine? Ikiwa waweza kusaidia, tafadhali kuja kwenye Idara ya Wenye Kujitakia kwenye kusanyiko. Watoto walio na umri cha chini ya miaka 16 wakaribishwa kutumika pamoja na mzazi au mtu mwingine mwenye umri mkubwa. Bila shaka, kila mmoja anaweza kusaidia kusafisha makao kwa kuangalia kwamba kila takataka iokotwe na kutiwa mahali panapofaa.

14 Tumepata mielekezo mizuri kuhusu mavazi na kujipamba vyenye kufaa kwenye makusanyiko. Kwa mfano: tunao mwongozo kuhusu mambo hayo katika nyongeza za Huduma Yetu ya Ufalme, tunavyo vielezi na picha katika vichapo vyetu, na zaidi ya yote, tunayo yale ambayo Yehova asema katika Biblia. (Rom. 12:2; 1 Tim. 2:​9, 10) Watu wanajua sisi ni nani na kwa nini tumekusanyika katika mji wao. Hivyo, mavazi na kujipamba kwetu vyenyewe ni ushahidi wenye nguvu. Wengi wa watu wa Yehova hutoa kielelezo chema upande huo. Hata hivyo, mara kwa mara, tunaona roho ya ulimwengu ikionyeshwa katika mavazi na kujipamba kwa baadhi ya wale wanaohudhuria makusanyiko yetu. Mavazi ya aina yoyote yenye kuonyesha viungo vya mwili hutia mashakani dai la kuwa mtu wa kiroho. Utu wa nje wenye kiasi, ulio safi na ulio nadhifu ndio wenye kupendeza zaidi. Kwa hiyo, vichwa vya familia wangepaswa kuchunguza kwa uangalifu mavazi wanayovaa washiriki wa familia yao. Jambo hilo lingepaswa pia kutumika tunapokuwa nje ya mahali pa kusanyiko. Kuvaa alama-vitambulisho zetu kabla na baada ya vipindi vya kusanyiko vya siku hutufungamanisha zaidi na Yehova na watu wake safi.​—Linganisha Marko 8:​38.

15 Mfalme mwenye hekima Solomono alipuliziwa kusema kwamba “ujinga umefungwa moyoni mwa mutoto” na kwamba “mutoto anayeachwa kwa yeye mwenyewe anapatia mama yake haya.” (Mez. 22:15; 29:15) Muda wa vipindi vya kusanyiko, Mashahidi vijana wasioangaliwa wamevuruga akina ndugu na dada waliojaribu kufaidika na programu. Muda wa siku ya mwisho ya kusanyiko, vijana fulani walikuwa wakikaa katika sehemu za juu za viti na walikuwa wakizungusha vionyeshi vilivyo kama fimbo, ambavyo hutokeza nuru, kuzunguka wasikilizaji. Nuru kutoka vionyeshi hivyo ni kubwa na inaweza kuharibu macho ya wengine, hata kwa kadiri kubwa. Ni wazi kwamba vijana hao hawakuwa wakifaidika na programu ya kiroho ambayo ilikuwa imetayarishwa kwa kuwafikiria. Kwa kuwa wazazi watatoa hesabu kwa Yehova kwa sababu ya mwenendo wa watoto wao, mama au baba anaweza kuwa hakika kwamba watato ni wenye kujiendesha vizuri na wenye kusikiliza maagizo ya Yehova ikiwa tu wanakaa pamoja na wazazi. Wahudumu watakaribia mtu yeyote anayekengeusha wengine na kumwomba aache kufanya hivyo, huku wakimkumbusha kwa wema afuate programu kwa uangalifu.

16 Kwa kuwa twaalika watu wote kwenye makusanyiko yetu, ni jambo la hekima kujihadhari kuhusiana na watoto na mali yetu binafsi. Watoto wetu ni zawadi yenye thamani kutoka kwa Yehova. Lakini tunajua kwamba ulimwengu unaonyesha utu wa Shetani wa kuteka watu. Kwa hiyo, jueni mahali watoto wenu walipo nyakati zote. Ungepaswa kuchukua nyakati zote pamoja nawe kamera, mfuko wa kuwekea fedha, na mambo mengine ya thamani; haifai kuyaacha kwenye kiti chako. Hakikisha kwamba gari lako limefungwa, na uweke mali yako binafsi katika sehemu ya gari ya kuwekea mizigo au uyachukue pamoja nawe. Jambo hilo hupunguza jaribio la kuvunja na kuingia ndani ya gari.

17 Ni jambo lenye kutia moyo kuona ndugu na dada wakiandika muda wa vipindi vya kusanyiko. Maandishi mafupi yatakusaidia ukaze fikira na kukumbuka nukta za maana. Kurudilia maandishi yako baadaye pamoja na familia au marafiki kutakuwezesha utafakari juu ya mambo makuu ya kusanyiko ili yasisahauliwe.

18 Watu wa Yehova wamekuwa sikuzote wenye ukarimu katika kutoa michango kwa ajili ya faida za kitheokrasi. (Kut. 36:​5-7; 2 Sik. 31:10; Rom. 15:26, 27) Michango yenu ya kujitakia kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni hutumiwa ili kulipia gharama zinazohusiana na kukodi yale makao makubwa ambayo katika hiyo makusanyiko hufanyika.

19 Kama inavyoandikwa kwenye Amosi 3:7, Yehova alisema kwamba ‘hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.’ Akiwa ‘Mfunuaji wa siri,’ Yehova ameandikisha katika Biblia mamia ya unabii mbalimbali uliotimizwa kwa usahihi na kikamili. (Dan. 2:​28, 47) Ahadi tukufu zingali zitatimizwa. Makusanyiko ya wilaya 1999 “Neno la Unabii la Mungu” yatatia nguvu imani yako katika ahadi za Mungu. Sikiliza kwa ukaribu anayokuambia Yehova. Tumia yale utakayoona na kusikia​—katika huduma, katika kutaniko na katika maisha yako binafsi. Tunaomba Yehova abariki mipango yako yote ili uhudhurie kila siku ya karamu hiyo tamu ya kiroho!

[Caption on page 3]

Panga kuhudhuria mchana wote Siku ya Tano, Siku ya Posho na Siku ya Yenga!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine