Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/08 uku. 5
  • Kipindi cha Kulishwa Kiroho na Kushangilia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kipindi cha Kulishwa Kiroho na Kushangilia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Mfuate Kristo kwa Kuonyesha Heshima
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Endelea Kumtarajia Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Mikusanyiko Yetu ya Wilaya—Inashuhudia Kabisa Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 4/08 uku. 5

Kipindi cha Kulishwa Kiroho na Kushangilia

1 Yehova anahangaikia kwa upendo mahitaji ya kiroho ya watumishi wake. Wakati ambapo ulimwengu kwa ujumla unapatwa na njaa ya kiroho, sisi tunalishwa vizuri kabisa. (Isa. 65:13) Mikusanyiko yetu ya wilaya ya kila mwaka ni njia moja ambayo Yehova anatumia ili kutulisha kiroho. Je, umeanza kujitayarisha ili kuhuzuria vipindi vyote vya Mkusanyiko wa Wilaya wa wakati ujao wenye kichwa “Kuongozwa na Roho ya Mungu”? Karamu ya chakula cha kiroho chenye kujenga imetayarishwa.

2 Jitayarishe Mbele ya Wakati: “Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta faida.” (Met. 21:5) Kwa hiyo, ili kuhakikisha kwamba umemaliza mipango yote ili kuhuzuria siku zote tatu za mkusanyiko, usikose kumjulisha mkubwa wako wa kazi ikiwa unahitaji wakati wa mapumziko. Ikiwa utataka kupangishwa, je, umefanya mipango mbele ya wakati? Utatayarisha pia chakula cha kutumia wakati wa mapumziko ili kuchangia pamoja na ndugu zako kwenye mahali pa mkusanyiko. Fanya mipango ili kufika pa wakati kila siku ili kupata nafasi ya kukaa na kuimba na kufuata sala ya kufungua.

3 Tunataka kuhakikisha kwamba mavazi tutakayovaa ni yenye kiasi na yenye mpangilio mzuri. (1 Tim. 2:9, 10) Mikusanyiko ya wilaya inatutolea nafasi nzuri zaidi ya kutolea watu ushahidi. Kuvaa kwa njia ya heshima kwenye mkusanyiko wa wilaya na kuvaa kadi zetu za utambulisho kunatufanya kuwa tofauti na watu wasioamini na kunafanya wale wanaotuangalia wawe na maoni mazuri juu yetu.

4 Sikiliza kwa Uangalifu: Kwa kweli, hatutaki kukosa habari yoyote itakayotolewa kwenye karamu hii ya kiroho! (Met. 22:17, 18) Kufuata usomaji wa maandiko katika Biblia zetu na kuandika mambo ya maana kutatusaidia kufuata programu kwa uangalifu na bila kukengeushwa. Kwa hiyo, wakati wa mangaribi, tunaweza kuzungumzia pamoja na wengine mambo ambayo tuliandika. Miaka iliyopita, ilionekana kwamba vijana fulani walikaa pamoja kwenye mkusanyiko wakizungumza wakati wa programu ao kuandikiana habari kwa njia ya telefone. Ikiwa una watoto wadogo na vijana, itakuwa vizuri kukaa pamoja nao na kufuata programu mukiwa familia badala ya kuachilia vijana kukaa pamoja na vijana wengine, mbali nanyi.

5 Chukua Nafasi ya Kuzungumza na Ndugu na Dada: Kuchangia chakula kitamu pamoja na marafiki kunafurahisha zaidi. (Met. 15:17) Vivyo hivyo, kuzungumza na ndugu na dada kunaongeza furaha yetu kwenye mkusanyiko. Kwa hiyo, mbele na kisha programu na pia wakati wa mapumziko, ni jambo lenye kupendeza kuchukua nafasi ya kukutana na wahuzuriaji wengine na kuzungumza nao. (Zab. 133:1) Mbele ya muziki kuanza, mwenyekiti anapotualika kwa uchangamfu tukae, tunapaswa kubaki kimya na kukaa mpaka wakati programu inapoanza.

6 Tumia Kila Nafasi ili Kutoa Ushahidi: Mara nyingi, mikusanyiko inatutolea nafasi nzuri zaidi ili kutolea wengine ushahidi. Wahuzuriaji wengi wanaoenda kwenye restaurant kisha mkusanyiko wanaulizwa na watu wanaogawa chakula kuhusu kichwa cha mkusanyiko kinachoonyeshwa kwenye kadi ya utambulisho. Hilo limesaidia kuanzisha mazungumzo na kutoa ushahidi juu ya kweli. Watu fulani waliouliza kuhusu kichwa cha mkusanyiko walialikwa kwenye mkusanyiko na walikuja kuhuzuria.

7 Saa nyingi sana zimetumiwa ili kutayarisha mkusanyiko, kutayarisha mahali pa kuufanyia, kupanga idara mbalimbali na kutayarisha hotuba zote. Kazi zote zilizofanywa kwa upendo ili kutayarisha karamu hiyo ya kiroho zinaonyesha kwamba Yehova anawahangaikia watu wake kwa upendo. Sisi wote na tuwe hapo na kujifunza mengi zaidi iwezekanavyo! Tofauti na ulimwengu, ‘tutapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya hali nzuri ya moyo.’—Isa. 65:14.

[Maulizo ya Funzo]

1. Jinsi gani Yehova anahangaikia mahitaji ya kiroho ya watumishi wake?

2. Unapaswa kufanya nini ili kujitayarisha mbele ya wakati kwa ajili ya mkusanyiko?

3. Ni mavazi ya aina gani ambayo tutapanga kuvaa?

4. Ni nini kitatusaidia kufaidika sana na programu sisi na familia zetu?

5. Tunaweza kufanya nini ili kuongeza furaha yetu kwenye mkusanyiko?

6. Eleza jambo ulilojionea linaloonyesha namna tunavyoweza kuhubiria watu katika mji ambamo mkusanyiko unafanywa.

7. Kwa nini tunapaswa kuhuzuria mkusanyiko wa wilaya unaokuja?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine