Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/09 uku. 4-7
  • Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kipindi cha Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Siku Tatu za Kuburudishwa Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mfuate Kristo kwa Kuonyesha Heshima
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Mikusanyiko Yetu ya Wilaya—Inashuhudia Kabisa Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2009
km 4/09 uku. 4-7

Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?

1. Ni matayarisho gani yanayopaswa kufanywa kwa ajili ya karamu?

1 Karamu inaomba matayarisho mengi. Inaomba kupata chakula, kukitayarisha vizuri, na kisha kukitolea watu. Inaomba kufanya mipango kuhusu jinsi ya kugawa chakula. Pia, inaomba kutayarisha mahali pa kufanyia karamu. Waalikwa wanapaswa pia kujitayarisha, zaidi sana ikiwa watafanya safari ndefu ili kufika kwenye karamu. Ijapokuwa karamu inaomba kazi nyingi, kula chakula kitamu na chenye kujenga mwili pamoja na marafiki na watu wa jamaa kunaleta furaha. Karibuni Mashahidi wa Yehova duniani pote watakusanyika pamoja wakiwa vikundi vikubwa ao vidogo, ili kufurahia karamu ya kiroho waliyongojea sana, yaani Mkusanyiko wa Wilaya wenye kichwa ‘Mwendelee Kukesha!’ Kazi nyingi imekwisha kufanywa ili kutayarisha programu na mambo mengine. Sisi wote tumealikwa. Ili kuhuzuria mkusanyiko huo na kufaidika kabisa, kila mutu anapaswa kujitayarisha.—Met. 21:5.

2. Inaomba kufanya nini ili kuhuzuria kila sehemu ya karamu yetu ya kiroho?

2 Faidika Kabisa na Karamu Hiyo: Je, umekwisha kufanya mipango yote ili kuhuzuria kila sehemu ya karamu hiyo ya kiroho? Ikiwa ni lazima, zungumza na mkubwa wako wa kazi ili kumjulisha kwamba utahuzuria vipindi vyote vya mkusanyiko, kuanzia siku ya kwanza ya mkusanyiko. Je, umefanya mipango yote kwa ajili ya usafirishaji na mahali pa kupanga? Wazee wanapaswa kuchunguza ikiwa watu waliozeeka na wazaifu wameshugulikiwa, na pia wengine ambao labda wanahitaji msaada.—Yer. 23:4; Gal. 6:10.

3. Kwa nini hatupaswi kuhuzuria mkusanyiko wa kimataifa ambako hatukualikwa?

3 Katika maeneo fulani, kutakuwa mikusanyiko ya kimataifa. Kumbuka kwamba makutaniko fulani na wahuzuriaji watakaotokea katika inchi za kigeni wamealikwa kwenye mikusanyiko hiyo. Ili kutayarisha mikusanyiko hiyo, biro ya tawi imekadiria kwa uangalifu hesabu ya wale ambao wataalikwa kwa kufikiria hesabu ya viti mahali pa mkusanyiko na ya vyumba vya hoteli ambamo watapanga. Ikiwa wahubiri wanahuzuria mkusanyiko wa kimataifa ambako hawakualikwa, hilo linaweza kutokeza msongamano.

4. Ni mambo gani ya kukumbuka yatakayotusaidia tuwe tayari kila siku programu inapoanza?

4 Jitayarishe kufika mahali pa mkusanyiko mbele ya wakati kila siku ili kupata nafasi mbele ya programu kuanza. Tumia dakika chache ili kutupia jicho kwenye programu mbele mkusanyiko uanze. Hilo litakusaidia kutayarisha moyo wako kwa ajili ya habari zitakazotolewa. (Ezra 7:10) Mwenyekiti wa kipindi cha mkusanyiko anapojulisha kwamba muziki unataka kuanza, uusikilize kwa furaha na kisha uwe tayari kuimba wimbo wa kufungua na kusikiliza sala.

5. Namna gani familia yetu inaweza kufaidika kabisa na mkusanyiko?

5 Ikiwa watu wa familia wanakaa pamoja wakati wa mkusanyiko, itasaidia wazazi waone ikiwa watoto wanafuata programu kwa uangalifu. (Kum. 31:12) Sisi wote tunatiwa moyo kufuata usomaji wa maandiko katika Biblia zetu. Kuandika mambo machache kunaweza kukusaidia kufuata kwa uangalifu. Baada ya muda, mambo uliyoandika yatakusaidia kukumbuka mambo makuu ya hotuba. Epuka kuongeaongea ao kutembeatembea wakati wa programu. Ikiwa una telefone, usiruhusu ikukengeushe ao kukengeusha wengine wakati wa programu. Kila siku baada ya mkusanyiko, unaweza kuzungumza na wengine kuhusu mambo ya programu ambayo ulifurahia?

6. Mikusanyiko yetu ina nafasi gani ya pekee, na namna gani tunaweza kufaidika kabisa na nafasi hiyo?

6 Kwenye mkusanyiko wa wilaya, tuna nafasi ya kufurahia uhusiano wa karibu pamoja na ndugu na dada zetu, uhusiano ambao haupatikane kati ya watu wa ulimwengu. (Zab. 133:1-3; Marko 10:29, 30) Kwa nini usijikaze kufahamiana na wale wanaokaa karibu nawe na kuzungumza nao wakati wa mapumziko? Hiyo ni faida moja inayotokana na kuleta chakula chepesi na kubaki mahali pa mkusanyiko kuliko kwenda inje ili kutafuta chakula. Usikose nafasi kama hiyo ya kutiana moyo na wengine.—Rom. 1:11, 12.

7. Ni matayarisho gani tunayopaswa kufanya kuhusiana na jinsi tutakavyovalia kwenye mkusanyiko?

7 Namna ya Kuvalia: Ni jambo la maana kujua kwamba Yehova aliwaamuru Waisraeli kujifanyia upindo wenye nyuzinyuzi kwenye miisho ya nguo zao na kuweka uzi wa bluu kwenye upindo huo wenye nyuzinyuzi. (Hes. 15:37-41) Hilo liliwakumbusha kwamba walikuwa watu waliotengwa kwa ajili ya ibada ya Yehova. Leo, kuvalia kwa njia ya heshima na yenye kiasi tunapokuwa kwenye mkusanyiko kunatufanya kuwa tofauti na watu wa ulimwengu. Kunatolea wale wanaotutazama ushahidi wenye nguvu hata wakati tunapoenda kula chakula kwenye restaurant kisha mkusanyiko. Kwa hiyo, fikiria kwa uangalifu tangu sasa namna utakavyovalia.

8. Namna gani tunaweza kutolea wengine ushahidi tunapokuwa katika mji ambamo mkusanyiko utafanywa?

8 Toa Ushahidi: Tukifanya mpango mbele ya wakati, tunaweza kutolea watu ushahidi tunapokuwa katika mji ambamo mkusanyiko utafanywa. Ndugu mmoja aliyeenda kwenye restaurant fulani pamoja na muke wake kisha mkusanyiko, alionyesha tu kadi yake ya utambulisho na akauliza mtumishi wa restaurant hivi: “Je, umeona watu wengi wenye kuvaa kadi hizi?” Mtumishi wa restaurant alisema kwamba amewaona na alijiuliza kwa nini kila mutu anavaa kadi hiyo. Mazungumzo yalianzishwa, na ndugu alimwalika mtumishi huyo kwenye mkusanyiko.

9. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani kwa Yule mwenye kutualika, Yehova?

9 Hata ikiwa ni ndugu zetu watakaotoa hotuba mbalimbali, kufanya sehemu za kuuliza watu maulizo, na maonyesho, Yehova Baba yetu wa mbinguni ndiye Mtoaji mwenye upendo wa karamu hii ya kiroho inayofanywa kila mwaka. (Isa. 65:13, 14) Tunaonyesha shukrani kwa Yule mwenye kutualika kwa kuhuzuria kila siku ya mkusanyiko na kula kila sehemu ya chakula cha kiroho kinachotolewa. Je, umefanya matayarisho yote ili kufanya hivyo?

[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 6]

Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mkusanyiko wa Wilaya

◼ Wakati Kuhusu Programu: Siku zote tatu programu itaanza pa saa 3:20 asubuhi. Milango itafunguliwa pa saa 2:00 asubuhi. Wakati muziki wa kufungua utakapoanza, sisi wote tunapaswa kukaa ili programu iweze kuanza kwa utaratibu. Siku ya Tano na Siku ya Posho, programu itamalizika pa saa 10:55 magaribi na Siku ya Yenga, itamalizika pa saa 10:00 magaribi. Kuhusu mikusanyiko ya kimataifa, programu itaanza Siku ya Ine pa saa 7:20 kisha midi na kumalizika pa saa 10:55 magaribi.

◼ Kuchungia Wengine Viti: Munaweza kuchungia viti wale tu wanaosafiri nanyi katika gari moja ao wale munaoishi nao katika nyumba moja.

◼ Chakula cha Saa Sita: Inapendekezwa kwamba kila mutu alete kitu fulani cha kula kisicho kizito lakini cha kujenga mwili, kwa mfano: sandwichi (mikate ao keki), matunda (ndizi), kalanga, vitumbua ao ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa ao chai vinapaswa kutiwa katika vyombo visivyoweza kuvunjika ili kuepuka aksida. Hairuhusiwi kuleta pombe kwenye mkusanyiko. Ikiwa tunaleta chakula na kinywaji chetu, hatutahitaji kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje. Kuepuka kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje kunasaidia kuonyesha kwamba sisi ni watu safi. (Tafazali, jueni kwamba wale wanaouzisha chakula inje hawataruhusiwa kuingia katika eneo la mkusanyiko wakati wowote.—Yohana 2:13-17.)

◼ Michango: Tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya mipango ya mkusanyiko kwa kutoa michango ya kujipendea kwenye Jumba la Ufalme ao mahali pa mkusanyiko, ili kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote.

◼ Aksida na Mambo Yanayoomba Kutenda Haraka: Ndugu wanaohusika na mambo yanayoomba kutenda haraka wanaitwa sana kwa sababu ya mambo madogomadogo. Ikiwa kunatokea jambo linaloomba kutenda haraka kwenye mkusanyiko, tafazali, munaweza kumwelezea ndugu mkaribishaji aliye karibu, ambaye atajulisha bila kuchelewa ndugu wanaoshugulika na Matunzo ya Haraka ili waamue ikiwa hali inaomba kutoa msaada unaohitajiwa.

◼ Kunasa Sauti (Enregistrement): Vyombo vya aina yoyote vya kunasa sauti havipaswi kuunganishwa na singa zinazochukua umeme ao kuunganishwa na vifaa vya sauti vya mkusanyiko na vinapaswa kutumiwa tu katika njia ambayo haitasumbua wengine.

◼ Kukamata Picha: Ukikamata picha wakati wa mkusanyiko, tafazali, usitumie mwangaza (flash). Tafazali, usiite mahali pa mkusanyiko wale wanaofanya kazi ya kukamata picha. Ikiwa unawaona wakitafuta mutu wa kukamata picha, usikubali wakukamate picha.—Yohana 2:13-17.

◼ Telefone za Mkononi: Zinapaswa kutiwa katika hali ambayo haitakengeusha wasikilizaji.

◼ Usafi: Imeonekana kwamba mara nyingi, wale wanaonunua vyakula kutoka kwa wale wanaouzisha chakula inje, wanatupa chini makaratasi ya kufungia vyakula. Hivyo, eneo lote linajaa makaratasi, vifuko vya plastiki, vifuniko vya machupa ya vinywaji-sukari, nk. Ikiwa mutu anachagua kununua chakula kwa wale wanaouzisha chakula inje, (kwa mfano: bonbons, biskwiti, ndazi ao vitumbua, vipande vya samaki ao chakula kingine), ana daraka la kutupa makaratasi ya kufungia vyakula katika chombo cha kutupia uchafu kuliko kutupa chini. Tukiona mutu fulani ametupa kipande cha karatasi ao cha plastiki chini, tunapaswa kukiokota na kukitia katika chombo cha kutupia uchafu. Tafazali ndugu, acheni tujikaze sana kuhusu jambo hilo ili kulinda mahali petu pa mkusanyiko na eneo la kandokando vikiwa safi. Kila mutu anayehuzuria anapaswa kuhangaikia jambo hilo la usafi. Ikiwa kila mutu anatimiza sehemu yake, mwishoni mwa siku, mahali pa mkusanyiko pataachwa pakiwa safi. Tunapenda kuonyesha katika maisha yetu sifa za Mungu ambaye tunaabudu na ambaye ni mtakatifu.—1 Pet. 1:15, 16; Kut. 19:10; Kum. 23:14.

◼ Mahali Ambapo Tunapangishwa: (1) Usiwe na watu wengi zaidi katika chumba ao nyumba isivyoruhusiwa ao isivyokubaliwa na mutu aliyekukaribisha. (2) Ikiwa utavunja ombi lako la kupangishwa, fanya hivyo bila kukawia. (3) Mbele ya kupika chakula, uliza mwenye nyumba ao ndugu wanaoshugulika na upangishaji katika Jumba la Ufalme ili ujue kile kinachohitajiwa ili kuepuka hatari. (4) Usitumie vibaya vitu vyovyote vinavyotolewa kwa ajili ya wageni. Kanuni ya mwenendo ni kuwa mwenye kiasi na mwenye usawaziko. (5) Ili kumwogopa Mungu inafaa kuwa safi. Kila siku, acha mahali ulipopangishwa pakiwa na utaratibu, penye usafi. Hilo linahusu pia Jumba la Ufalme, ambalo linaweza kutumiwa kuwa mahali pa upangishaji kwa ajili ya ndugu waliotoka katika makutaniko ya mbali. (6) Onyesha matunda ya roho katika kushugulika na wengine, iwe ni mwenye nyumba ao ndugu wengine Wakristo ambao labda munapangishwa pamoja nao.—Gal. 5:22, 23.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine