Mfuate Kristo kwa Kuonyesha Heshima
1 Biblia inaeleza kwamba Yehova Mwenye Enzi Kuu ni mwenye kuvaa heshima. (Zab. 104:1) Wakati wote, Yesu alisema na kutenda katika njia ambayo ilimheshimisha Baba yake na kuletea mipango ya Baba yake heshima. (Yoh. 17:4) Kila mmoja wetu atakuwa na nafasi za kumwiga Yesu na kumletea Yehova utukufu wakati wa Mikusanyiko yetu ya Wilaya inayokuja yenye kichwa “Mfuate Kristo!”
2 Kuonyesha Heshima Kuhusu Ibada: Tunaweza kumheshimu Yehova kwa kuchukua mipango ili tuwe kwenye karamu hiyo ya kiroho ambayo ametayarisha kwa ajili yetu. Je, umezungumza na mkubwa wako wa kazi na kupanga mambo yako ili kuhuzuria kila siku ya mkusanyiko, na pia Siku ya Tano? Je, umepanga kufika mbele vya kutosha ili kupata mahali utakapokaa na kushiriki wimbo na sala ya mwanzo? Je, umechukua mipango kuhusu chakula chako cha saa sita ili uweze kula mahali pa mkusanyiko? Mwanzoni mwa kila kipindi wakati mwenyekiti anatualika kwa upendo ili tukae mbele ya muziki kuanza, tunapaswa mara moja kumaliza mazungumzo yetu na kukaa ili kungojea mwanzo wa programu.
3 Kusikiliza kwa uangalifu sana wakati wa programu kunamletea pia Baba yetu wa mbinguni heshima. Kisha kutazama mkusanyiko wa wilaya mmoja uliofanyika kwao, mpashaji habari mmoja aliandika kwamba watazamaji walishangazwa na “mwenendo mzuri wa watu wanaohuzuria, jinsi wanavyofuata kwa adabu na ukimya na wakiwa wenye kuvutiwa sana na mambo ya kiroho.” Alitoa pia maelezo kuhusu “hesabu kubwa ya watoto . . . , kwa kushangaza wote wakiwa wenye kujiendesha vizuri au wakiwa wenye kutafuta maandiko katika Biblia Takatifu.” Programu inapoendeshwa si wakati wa kuzungumza mambo yasiyo ya lazima, kutumiana ujumbe katika telefone, kula, au kutembeatembea. Watoto wanapaswa kuwa wenye kukaa pamoja na wazazi wao ili wazazi wao waweze kuwasaidia kufaidika na programu. (Kum. 31:12; Met. 29:15) Tunapojikaza kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tunaheshimu wengine na kwamba sisi ni wenye shukrani kwa ajili ya chakula cha kiroho cha maana ambacho tunatolewa.
4 Kuvalia na Kujipamba kwa Heshima: Watu wengi walifurahia sana vikumbusho vya Yehova kwenye mkusanyiko wa wilaya wa mwaka jana katika hotuba yenye kichwa “Nyakati Zote, Onyesheni Heshima Inayofaa Mnapomwabudu Yehova,” hotuba hiyo ilionyesha kwamba watumishi wa Mungu wanapaswa kujikaza ili kuonyesha heshima ya Kikristo katika kuvaa na kujipamba kwao. Mwaka huu tunapaswa tena kuchukua jambo hili kwa uzito. Kuvalia na kujipamba kwetu kunapaswa kuonyesha jinsi tunavyomuona Yehova na jinsi tunavyoliona pendeleo la kuwa Mashahidi wake. Wakati wote tunapaswa kuvalia kama wale “wanaodai kumheshimu Mungu.”—1 Tim. 2:9, 10.
5 Je, tunapaswa kuvalia na kujipamba kwa heshima wakati wa programu tu? Kumbuka kwamba wengi watatuona tukiwa wenye kuvalia kadi za vitambulisho katika mji wa mkusanyiko. Namna yetu ya kuvaa na kujipamba inapaswa kutufanya tuwe tofauti na watu wengine wote. Kwa hiyo, hata wakati wa kuvuta hewa, kama vile wakati wa kwenda kula chakula kwenye hoteli (au restaurant) kisha programu, tunapaswa kuvalia kama inavyostahili watumishi ambao wanapatikana katika mji kwa kusudi la kuhuzuria mkusanyiko wa Kikristo, na hivyo hatupaswi kuvalia mavazi kama vile jeans, kaputula, Ti-sheti au Polo. Mavazi yenye kiasi, si ya bei sana, lakini ni yale yaliyo safi, yanayoonyesha heshima na yasiyo ya ovyoovyo. Kuvalia kwa heshima kutatolea watu ushahidi kabisa! Yehova anapendezwa wakati kuvalia na kujipamba kwetu kunaonyesha kwamba sisi tuna daraka la kuhubiri.
6 Matokeo Yenye Kupendeza: Kuonyesha heshima ya Kikristo kwenye mikusanyiko yetu ya wilaya kunatutolea nafasi mbalimbali za kutolea watu ushahidi ijapokuwa hatukupangilia kufanya hivyo na kufanya wale wenye kutuangalia wawe na maoni mazuri juu yetu. Mwishoni mwa mkusanyiko mmoja wa wilaya, mkubwa mmoja wa serikali alisema: “Hatujaona kamwe watu wenye kujiendesha vizuri kama ninyi. Ninyi munaishi jinsi Mungu anavyopenda tuishi.” Kuonyesha heshima ni alama ya adabu na upendo kwa mmoja na mwenzake na kunamtukuza Yehova. (1 Pet. 2:12) Kunaonyesha kwamba tunamwogopa Mungu na kwamba tunaonyesha shukrani kwa pendeleo la kufundishwa na Baba yetu. (Ebr. 12:28) Na tujikaze kuonyesha heshima tunapongojea Mkusanyiko wa Wilaya wenye kichwa “Mfuate Kristo!”
[Maulizo ya Funzo]
1. Namna gani kichwa cha mkusanyiko wa wilaya mwaka huu kinapatana na jambo la kuonyesha heshima?
2. Tunapojitayarisha ili kuwa kwenye kila kipindi cha mkusanyiko wa wilaya, hilo linamletea Yehova heshima namna gani?
3. Namna gani kusikiliza programu kwa uangalifu sana ni jambo lenye kuonyesha kwamba tunaiheshimu ibada yetu?
4. Kwa nini tunapaswa kuvalia na kujipamba kwa heshima kwenye mkusanyiko wa wilaya?
5. Namna gani tunaweza kuendelea kuvalia na kujipamba kwa heshima wakati wa kuvuta hewa katika mji wa mkusanyiko wa wilaya?
6. Kuonyesha heshima ya Kikristo kuna matokeo gani mazuri?