Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/06 uku. 4-5
  • Endelea Kumtarajia Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Endelea Kumtarajia Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kipindi cha Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Mfuate Kristo kwa Kuonyesha Heshima
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 4/06 uku. 4-5

Endelea Kumtarajia Yehova

1 “Yehova ni Mungu wa hukumu,” aliandika Isaya. “Wenye furaha ni wale wote wanaoendelea kumtarajia.” (Isa. 30:18b) Kuna masimulizi mengi ya Biblia yanayohusu hukumu ya Mungu juu ya adui zake na wokovu wa watumishi wake waaminifu. Masimulizi hayo yanatolea waabudu wa Yehova mafundisho gani leo? Tunaweza kufanya nini ili kujitayarisha kwa ajili ya “ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kuogopesha”? (Yoe. 2:31, 32) Mkusanyiko wetu wa Wilaya unaokuja “Ukombozi Unakaribia!” utatuchochea kutafakari kuhusu maulizo hayo na kufanya uchunguzi wa kibinafsi. Utatusaidia kuendelea kumtarajia Yehova.

2 Je, umefanya mipango ili kufaidika na siku zote tatu za mkusanyiko? Kwa mfano, je, umezungumza na bwana wako wa kazi ili kupata siku za mapumziko zitakazokuruhusu uhudhurie? Usifikiri kwamba utapata ruhusa bila kufanya jitihada fulani. Sali kuhusu jambo hilo. Baadaye fanya ombi lako. (Neh. 2:4, 5) Pia, hatupaswi kupangia kwenye dakika za mwishomwisho mambo yetu kuhusu usafirishaji, makao, na mambo mengine ya maana. Kupangia vizuri mambo kimbele kunaonyesha kwamba tunathamini kwa uzito meza ya kiroho ya Yehova. Wazee wanapaswa kuwa macho ili kusaidia wale wanaohitaji msaada kuhusiana na mipango ya mkusanyiko, hasa wazeewazee katika kutaniko.—Gal. 6:10.

3 Mwenendo Bora Unamletea Mungu Heshima: Tunapokusanyika watu wengi kwenye mikusanyiko, mwenendo wetu bora unakuwa ushuhuda kwa majirani. Hilo linaomba nini kwa upande wetu? Katika eneo ambamo mkusanyiko unafanywa, wale tunaokutana nao wanapaswa kuvutiwa na sifa zetu za Kikristo, kama vile ustahimilivu, upole, kujizuia, na usawaziko. (Gal. 5:22, 23; Flp. 4:5) Sisi sote tunapaswa kuonyesha aina ya upendo ambao “haujiendeshi bila adabu, hautafuti faida zake wenyewe, hauchokozeki.” Hata ikiwa matatizo au mambo yenye kuudhikisha yanatokea, tutataka ‘kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’—1 Kor. 10:31; 13:5.

4 Baada ya mkusanyiko mmoja, msimamizi wa hoteli moja alishangazwa na mwenendo, mvalio wa vijana na namna yao ya kujipamba hivi kwamba alitamani “kuwa na wageni Mashahidi wa Yehova siku zote katika hoteli yake.” Ni jambo lenye kufurahisha kama nini! Sifa hiyo inatokana na mazoezi na uongozi mzuri wenu ninyi wazazi. Lingekuwa jambo lisilo la hekima kwa wazazi kuruhusu watoto wao kubaki katika makao wanamopanga bila kujali au kutupia jicho yale wanayofanya. Wakati wote watoto wanapaswa kuangaliwa vizuri. (Met. 29:15) Mwenendo wao bora na umletee Yehova sifa na kufurahisha moyo wake—Met. 27:11.

5 Kuvalia na Kujipamba kwa Kiasi: Kila mmoja wetu anaweza kufanya watazamaji wawe na maoni mazuri kuelekea mkusanyiko kwa kuepuka mitindo ya mavazi na ya kujipamba inayopita kiasi, ya upuuzi au ya ovyoovyo. Kanuni hiyo inatumika wakati wa kusafiri kwenda kwenye mahali pa mkusanyiko au tunaporudi kutoka huko, wakati tunaposaidia kufanya kazi fulani kwenye mahali pa mkusanyiko, na wakati tunapohudhuria kwenye vipindi vya mkusanyiko. Tukiwa watumishi wa Mungu, hangaiko letu la kwanza ni jina na sifa ya Yehova, wala si mambo yetu ambayo sisi tunapendelea. Vichwa vya familia wana daraka la kuhakikisha kwamba namna ya kuvalia na ya kujipamba ya familia zao inaonyesha wakati wote kiasi na utimamu wa akili—1 Tim. 2:9.

6 Ni jambo la maana pia kuvalia na kujipamba kwa heshima wakati wa kujiburudisha. Ni vizuri kuvaa mavazi yaleyale tuliyovaa kwenye mkusanyiko tunapotumia chakula mahali fulani baada ya vipindi vya mkusanyiko. Kuvaa kadi yetu ya utambulisho kunatokeza nafasi nyingi kwetu ili kutoa ushahidi wa vivihivi.—2 Kor. 6:3, 4.

7 Isaya alitabiri: “Yehova ataendelea kutarajia kuwaonyesha ninyi kibali, na kwa hiyo atasimama ili kuwaonyesha ninyi rehema.” (Isa. 30:18a) Shukrani kwa rehema na fadhili zisizostahiliwa za Yehova inapaswa kutuchochea kumheshimu kupitia mwenendo wetu, namna yetu ya kuvalia na ya kujipamba tunapokusanyika sote pamoja kwenye mikusanyiko yetu. Mkusanyiko wa Wilaya “Ukombozi Unakaribia!” na umtukuze Mungu wetu na kutusaidia kuendelea kumtarajia yeye!

[Maulizo ya Funzo]

1. Ni nini kichwa cha mkusanyiko, na kwa nini ni chenye kufaa?

2. Tunawezaje kuonyesha kwamba tunathamini mkusanyiko wetu wa wilaya?

3. Ni sifa gani ambazo watu wa Yehova wanapaswa kuonyesha katika mji wa mkusanyiko?

4. Wazazi wanawezaje kuwasaidia watoto wao wajiendeshe katika njia inayomletea Yehova sifa?

5. Tunawezaje kumheshimu Yehova kupitia mavazi na kujipamba kwetu?

6. Kwa nini tunapaswa kujipamba na kuvalia kwa heshima wakati wa kujiburudisha kama tu tunavyofanya muda wa vipindi vya mkusanyiko?

7. Tunaweza kufanya nini ili kuwe na utaratibu na furaha kwenye mkusanyiko? (Ona Kisanduku “Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mkusanyiko wa Wilaya.”)

[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 5]

Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mkusanyiko wa Wilaya

◼ Wakati Kuhusu Programu: Siku zote tatu programu itaanza pa saa 3:30 asubuhi. Milango itafunguliwa pa saa 2:00 asubuhi. Dakika chache kabla ya kuanza kipindi, msimamizi atakaa jukwaani huku muziki wa Ufalme wenye kufungua ukichezwa. Wakati huo sisi wote tunapaswa kukaa ili programu iweze kuanza katika njia yenye kuleta heshima. Siku ya Tano programu itamalizika pa saa 11:15 kisha mchana-kati, Siku ya Posho pa saa 11:05 kisha mchana-kati, na Siku ya Yenga itamalizika pa saa 10:10 kisha mchana-kati.

◼ Kuchunga Nafasi ya Kukaa: Mnaweza kuchungia viti wale tu wanaosafiri nanyi katika gari moja au wale mnaoishi pamoja nao katika nyumba moja.

◼ Mlo wa Saa Sita: Ilipendekezwa kwamba kila mtu alete kitu fulani cha kula kisicho kizito lakini cha kujenga mwili, mfano: sandwichi (mikate au keki), matunda (ndizi), karanga, vitumbua au ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa au chai vinapaswa kutiwa katika vyombo visivyoweza kuvunjika ili kuepuka misiba. Hairuhusiwi kuleta pombe kwenye mkusanyiko. Ikiwa tunapeleka chakula na kinywaji chetu, jambo hili litaondoa uhitaji wa kununua vyakula kwa wale wachuuzi. (Taarifa: Wachuuzi wa vyakula hawataruhusiwa kuingia katika eneo la mkusanyiko wakati wowote.—Yohana 2:13-17.) Wale wanaotumia jiko la makaa (mbabula) ili kutayarisha chakula kwenye mahali pa mkusanyiko, wanapaswa kupata kwanza ruhusa ya ndugu wanaosimamia mkusanyiko ili kujua mahali ambapo wanaweza kulitia. Ni lazima kuwa waangalifu ili kuepuka misiba.—Luka 10:38-42.

◼ Zawadi: Gharama kubwa inafanywa katika kutayarisha mkusanyiko wa wilaya. Tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini mpango huo kwa kufanya michango ya kujipendea kwa kazi ya ulimwenguni pote kwenye Jumba la Ufalme au kwenye mkusanyiko.

◼ Aksidenti na Mambo Yanayoomba Kutenda kwa Uharaka: Ndugu wanaohusika na mambo yanayoomba kutenda kwa uharaka wametoa malalamiko kwamba wanapokea simu nyingi zinazohusu mambo madogo madogo. Ikiwa kunatokea jambo la matunzo linaloomba kutenda kwa uharaka kwenye kituo cha mkusanyiko, tafadhali, mnaweza kumuelezea ndugu mkaribishaji aliye karibu ambaye atajulisha bila kuchelewa Huduma ya Kwanza ili ndugu wenye kuhusika kwenye kituo wakadirie uzito wa jambo hilo na kutoa msaada.

◼ Kurekodi: Vifaa vya kurekodi vya aina yoyote havipaswi kuunganishwa na mfumo wa umeme au vifaa vya sauti vya mkusanyiko na vinapaswa kutumiwa tu katika njia ambayo haitasumbua wengine.

◼ Kupiga Picha: Ukipiga picha wakati wa mkusanyiko, tafadhali usitumie mwangaza.

◼ Simu za Mkononi: Zinapaswa kutiwa katika hali ambayo haitakengeusha watu.

◼ Usafi: Imeonekana kwamba mara nyingi, wale wanaonunua vyakula kutoka kwa wachuuzi, wanatupa chini karatasi za kufungia. Hivyo eneo lote linajaa na makaratasi, vifuko vya plastiki, vifuniko vya machupa ya vinywaji-sukari nk. Ikiwa mtu anachagua kununua chakula kwa wachuuzi (mfano: keki, vitumbua, vipande vya samaki au chakula kingine), ana daraka la kutupa karatasi za kufungia katika pipa la kutupia uchafu wala si chini. Tukiona mtu fulani ametupa kipande cha karatasi au cha plastiki chini, tunapaswa kukiokota na kukitia katika pipa la kutupia uchafu. Tafadhali ndugu acheni tufanye jitihada ya pekee kuhusu jambo hilo ili kulinda mahali petu pa mkusanyiko na eneo la kandokando vikiwa safi. Kuhangaikia usafi ni jambo linalopaswa kufikiriwa na kila mtu anayehudhuria. Ikiwa kila mtu anafanya sehemu yake, mwisho wa siku, mahali pa mkusanyiko pataachwa pakiwa safi. Tunapenda kuonyesha sifa za Mungu ambaye tunaabudu na ambaye ni mtakatifu.—1 Pet. 1:15, 16; Kut. 19:10; Kum. 23:14.

◼ Mahali Tunapopangishwa: (1) Usiwe na watu wengi zaidi katika chumba au nyumba isivyoruhusiwa au isivyokubaliwa na mtu aliyekukaribisha. (2) Ikiwa utavunja ombi lako la upangishaji, tafadhali fanya hivyo bila kukawia. (3) Kabla ya kupika chakula, uwe hakika kwamba ulimwuliza mkaribishaji wako au ndugu wanaoshughulika na upangishaji katika Jumba la Ufalme ili kujua kile kinachohitajiwa. (4) Usitumie vibaya maandalizi yoyote yanayotolewa kwa ajili ya wageni. Kanuni ya mwenendo ni kuwa mwenye kiasi na mwenye usawaziko. (5) Usafi na woga wa Mungu vinakaribiana sana. Kila siku, acha mahali ulipopangishwa pakiwa na utaratibu, penye kusafishwa na safi. Hilo linatia ndani Jumba la Ufalme, ambalo huenda likatumiwa kuwa mahali pa upangishaji kwa ajili ya ndugu waliotoka katika makutaniko ya mbali. (6) Onyesha matunda ya roho katika kushughulika na wengine, iwe ni mkaribishaji wako au ndugu wengine Wakristo ambao huenda mnapangishwa pamoja.—Gal. 5:22, 23.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine