Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/05 uku. 4-5
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Endelea Kumtarajia Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Mfuate Kristo kwa Kuonyesha Heshima
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Kipindi cha Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 4/05 uku. 4-5

Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa

1, 2. Ni nafasi gani ambayo mkusanyiko wa wilaya unatutolea, na tunaweza kutimiza jambo hilo katika njia gani?

1 Kila mwaka mikusanyiko yetu ya wilaya inatutolea nafasi bora ya kumtukuza Yehova. Hisia zetu ni kama zile za Daudi, aliyeimba: “Nitakusifu katika kutaniko kubwa; kati ya kikundi cha watu wengi.” (Zab. 35:18) Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya ujao wenye kichwa “Utii wa Kimungu,” tunawezaje kuwa hakika kwamba tunamtolea Yehova sifa tukiwa watu wenye umoja?

2 Njia moja katika hiyo tunaweza kufanya hivyo ni kupitia mwenendo wetu. Msimamizi wa jengo moja la mkusanyiko alisema: “Kwa kuona mikusanyiko yenu, tumewaambia washiriki wa vikundi vingine vya kidini wanaotaka kulikodi jengo kwamba waje waone jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyotengeneza mkusanyiko, jinsi wanavyopangia mambo vizuri.” Kupitia mavazi na kujipamba kwetu, ushirikiano wetu na mwenendo wetu, kila mmoja wetu anashiriki katika kutokeza semi hizo nzuri za kusifu, zinazostahili kumwendea Mungu wetu.—1 Pet. 2:12.

3, 4. Namna gani kiasi itatusaidia kuvalia katika njia inayofaa wahudumu Wakristo, kwenye mkusanyiko na baada ya vipindi?

3 Mvalio na Kujipamba: Ili tuvae na tujipambe katika njia inayomletea Yehova sifa inatuomba kuwa na kiasi. (1 Tim. 2:9) Kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 132 kinasema: ‘Mtu mwenye kiasi anakuwa mwangalifu asiwaudhi wengine isivyofaa na kutojielekezea fikira mno.’ Katika nchi nyingi, mavazi yasiyo na kiasi yamekuwa ya kawaida. Hata hivyo, Yehova anathamini bidii tunayofanya ili kumwakilisha inavyofaa. (Mdo. 15:14) Ijapokuwa mkusanyiko unaweza kufanyika katika jengo la michezo au majengo ya kujiburudishia, mkutano unakuwa “kutaniko kubwa” letu mnamo siku hizo tatu za mkusanyiko. Kwa hiyo, kwa kuwa tunakusanyika mbele ya Yehova, tunapaswa kuvalia kwa heshima inayomstahili Mtu aliye juu zaidi katika ulimwengu.—1 Sik. 29:11.

4 Tunapaswa pia kuwa waangalifu kuhusu mvalio na kujipamba kwetu baada ya kipindi cha mwisho kila siku. Hata ingawa huenda tukatamani kuvalia mavazi kwa namna tujisikie vizuri zaidi wakati wa kujiburudisha au wakati wa kula kwenye mkahawa (restaurant), ni jambo la lazima kwamba mavazi yetu na kujipamba kwetu kuendelee kuwa kule kunakofaa wale “wanaodai kumheshimu Mungu.” (1 Tim. 2:10) Hatutaamua kwamba mavazi fulani yanakubaliwa kwa kuwa yanapendwa na watu wengi katika ulimwengu. (1 Yoh 2:16, 17) Vichapo vyetu vya Kikristo vinatoa mifano inayosaidia ya wanaume na wanawake wanaovalia kwa kiasi na kwa mpangilio mzuri katika hali mbalimbali. Kuvaa kadi zetu za vitambulisho tunapopatikana katika mji wa mkusanyiko kutatukumbusha kwamba sisi ni wahudumu wakati wote.—2 Kor. 6:3, 4.

5, 6. Namna gani tunaweza kuonyesha heshima kwa meza ya kiroho ya Yehova?

5 Tuiheshimu Meza ya Yehova: Bwana Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu ametuandalia karamu. (Isa. 25:6; 1 Kor. 10:21) Tukithamini sana nafasi yetu kwenye meza ya kiroho ya Yehova, mradi wetu utakuwa kuhudhuria siku zote tatu za mkusanyiko. Je, umefanya mipango kuhusu upangishaji, usafirishaji, na kuomba mapumziko kazini? Je, umechukua wakati wakutosha kuhusu matayarisho na kusafiri ili ufike kwenye mahali pa mkusanyiko mapema vyakutosha ili kujipatia viti, kushirikiana na ndugu zetu, na kuungana nao katika kumtolea Yehova sifa kwa wimbo na sala ya kufungua?—Zab. 147:1.

6 Kuheshimu meza ya Yehova kutatuchochea tuwe waangalifu sana kuhusu programu na kuepuka kuzungumzazungumza na wengine bila sababu ya lazima, kula au kutembeatembea katika vijia vya jengo. Kupitia jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara, Yehova anatutolea chakula cha kiroho tunachohitaji sasa. (Mt. 24:45) Hatupaswi kukosa hata sehemu moja ya programu. Wazazi wanapaswa kukaa na watoto wao na kuwasaidia wafaidike kikamili.—Kum. 31:12.

7. Tunaombwa kufanya nini kuhusu chakula cha saa sita, na kwa nini?

7 Inaombwa kwamba tulete chakula cha mchana badala ya kuacha mahali pa kusanyiko ili kutafuta chakula wakati wa mapumziko ya saa sita. Lilikuwa jambo la kusifiwa kwamba wahudhuriaji wengi walifuata kwa uangalifu uongozi huo kwenye mkusanyiko wa mwaka uliopita. Litakuwa jambo lenye kusifiwa tena zaidi ikiwa wote watafanya hivyo mwaka huu. (Ebr. 13:17) Mpango huu unatoa nafasi nzuri ya kufurahia ushirika wenye kujenga pamoja na ndugu zetu na unachangia hali ya umoja na amani inayomletea Yehova heshima —Zab. 133:1.

8, 9. Ni nafasi gani ya ziada ya kumsifu Yehova ambayo mkusanyiko wa wilaya unatutolea?

8 Kutoa Ushahidi wa Vivihivi: Tunaposafiri kwenda au kutoka kwenye mkusanyiko, tuna nafasi nyingi za kumsifu Yehova kwa midomo yetu. (Ebr. 13:15) Iwe tunapokula kwenye mkahawa (restaurant) au kuzungumza pamoja na wafanyakazi wa hoteli, na tutafute njia za kutoa ushahidi. Akili zetu na mioyo yetu vitajaa na hazina za kiroho kutokana na mkusanyiko. Na tushiriki mambo hayo mazuri na wale tunaokutana nao katika kutoa ushahidi wa vivihivi.—1 Pet. 3:15.

9 Tunatazamia kimbele kwa hamu sana nafasi hii ya kumbariki Yehova “kati ya makundi yaliyokutanika.” (Zab. 26:12) Na tumtukuze Yehova kwa umoja kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wenye kichwa “Utii wa Kimungu.”

[Kisanduku kwenye ukurasa wa 5]

Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mkusanyiko wa Wilaya

◼ Wakati Kuhusu Programu: Siku zote tatu programu itaanza pa saa 3:30 asubuhi. Milango itafunguliwa pa saa 2:00 asubuhi. Dakika chache kabla ya kuanza kipindi, msimamizi atakaa kwenye jukwaa huku muziki wa Ufalme wenye kufungua ukichezwa. Wakati huo sisi wote tunapaswa kukaa ili programu iweze kuanza katika njia yenye kuleta heshima. Siku ya Tano na Siku ya Posho programu itamalizika pa saa 11:05 kisha mchana-kati na Siku ya Yenga programu itamalizika pa saa 10:10 kisha mchana-kati.

◼ Zawadi: Gharama kubwa inafanywa katika kutayarisha mkusanyiko wa wilaya. Tunaweza kuonyesha kwamba tuna thamini mpango huo kwa kufanya michango ya kujipendea kwa kazi ya ulimwenguni pote kwenye Jumba la Ufalme au kwenye mkusanyiko.

◼ Mlo wa Saa Sita: Ilipendekezwa kwamba mtu alete kitu fulani kwa kula kisicho kizito lakini kilicho na lishe, mfano: sandwichi (au mkate), matunda (ndizi), karanga, vitumbua au ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa au chai vinapaswa kuwekwa katika chombo kisichoweza kuvunjika ili kuepuka misiba. Hairuhusiwi kuleta vinywaji vya alkoholi kwenye mkusanyiko. Ikiwa tunapeleka chakula na kinjwaji chetu, jambo hili litaondoa uhitaji wa kununua vyakula kwa wale wachuuzi. (Taarifa: Wachuuzi wa vyakula hawataruhusiwa kuingia katika eneo la mkusanyiko wakati wowote.—Yoh. 2:13-17.) Wale wanaotumia jiko la makaa (mbabula) ili kutayarisha chakula kwenye mahali pa mkusanyiko, wanapaswa kupata kwanza ruhusa kutoka ndugu wanaosimamia mkusanyiko ili kujua mahali ambapo wanaweza kulitia. Ni lazima kuwa waangalifu ili kuepuka misiba.—Luka 10:38-42.

◼ Usafi: Imeonekana kwamba mara nyingi, wale wanaonunua chakula kwa wachuuzi, wanatupa chini karatasi za kufungia. Hivyo eneo lote linajaa na makaratasi, vifuko vya plastiki, vifuniko vya machupa ya vinywaji-sukali nk. Ikiwa mtu anaamua kununua chakula kwa wachuuzi [mfano: peremende (bonbon), keki (gateaux), vitumbua, vipande vya samaki au vyakula vingine], ana daraka la kutupa karatasi za kufungia katika pipa la kutupia uchafu wala si chini. Ikiwa tunaona kwamba mtu fulani ametupa kipande cha karatasi au kipande cha plastiki kwenye sakafu au chini, tunapaswa kukiokota na kukitupa katika pipa la kutupia uchafu. Tafadhali ndugu acheni tufanye jitihada ya pekee kuhusu jambo hilo ili kulinda uwanja na eneo la kandokando vikiwa safi. Usafi ni daraka la kila mtu anyehudhuria. Ikiwa kila mtu anafanya sehemu yake, mwisho wa siku, majengo ya mkusanyiko yataachwa yakiwa safi. Tunataka kuonyesha sifa za Mungu ambaye tunaabudu na ambaye ni mtakatifu.—1 Pet. 1:15, 16; Kut. 19:10; Kum. 23:14.

◼ Wazazi na watoto: Watazamaji wameshangazwa kuona watoto wadogo wakikaa kwa makini wakati wa programu, wakichukua maandishi na kufuatana na usomaji wa Maandiko katika Biblia zao. Vijana hawapaswi kuachwa bila ulinzi ufaao. Ikiwa wanahitaji kwenda kwenye choo, mzazi au ndugu au dada wa watoto anapaswa kuwasindikiza. Lingekuwa pia jambo la hekima kuwa na maji ya kunywa; hilo lingeepusha uhitaji wa kuondoka mahali tunapoketi ili kutafuta maji wakati wa kipindi cha mkusanyiko. Wakati wa mapumziko, tunataka kutazama ikiwa watoto wetu hawakimbiikimbii kwenye ngazi, hilo linaweza kusababisha hatari ya kuanguka au kufanya wengine waanguke. Kukosa utulivu kunasababisha mambo yenye kusumbua na kutukanisha jina la Yehova. Mwenendo wetu mzuri unamletea Yehova, yeye aliye Mungu wa utaratibu, sifa na utukufu. —1 Kor. 14:40.

◼ Kurekodi: Kurekodi kwa aina yoyote hakupaswi kuunganishwa na vifaa vya umeme au mfumo wa sauti na kunapaswa kutumiwa tu katika njia ambayo haitasumbua wengine.

◼ Simu za Mikononi: Simu hizo zinapaswa kufungwa ili zisikengeushe.

◼ Mahali Tunapopangishwa: (1) Usiwe na watu wengi zaidi katika chumba au nyumba isivyoruhusiwa au isivyokubaliwa na mtu aliyekukaribisha. (2) Ikiwa utavunja ombi lako la upangishaji, tafadhali fanya hivyo bila kukawia. (3) Kabla ya kupika, uwe hakika kwamba ulimwuliza mkaribishaji wako au ndugu wanaoshughulika na upangishaji katika Jumba la Ufalme ili kujua kile kinachohitajiwa. (4) Usitumie vibaya maandalizi yoyote yanayotolewa kwa ajili ya wageni. Kanuni ya mwenendo ni kuwa mwenye kiasi na mwenye usawaziko. (5) Usafi na woga wa Mungu vinakaribiana sana. Kila siku, acha mahali ulipopangishwa pakiwa na utaratibu, penye kusafishwa na safi. Hilo linatia ndani Jumba la Ufalme, ambalo huenda likatumiwa kuwa mahali pa upangishaji kwa ajili ya ndugu waliotoka katika makutaniko ya mbali. (6) Onyesha matunda ya roho katika kushughulika na wengine, iwe ni mkaribishaji wako au ndugu wengine Wakristo ambao huenda mnapangishwa pamoja.—Gal. 5:22, 23.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine