Tujikaze Sote Pamoja Ili Kutangazia Watu Ulimwenguni Pote Mkusanyiko wa Wilaya “Mfuate Kristo!”
Wahubiri Watagawanya Tena Kikaratasi cha Pekee cha Kualika Watu
1 Kampanye ya mwaka jana ya kutangaza Mkusanyiko wa Wilaya “Ukombozi Unakaribia!” ilikuwa na matokeo yenye nguvu juu ya watu wenye kupendezwa. Wale waliokubali mwaliko wa pekee walifurahia kwa mara ya kwanza karamu kubwa ya kiroho pamoja na Mashahidi wa Yehova. (Isa. 65:13) Walifurahia ushirika wetu wenye kuchangamsha, undugu wa Kikristo wenye umoja. (Zab. 133:1) Ili kusaidia wengi iwezekanavyo kuhuzuria Mkusanyiko wa Wilaya “Mfuate Kristo!” tutagawa tena ulimwenguni pote kikaratasi cha pekee cha kualika watu.
2 Matokeo ya Mwaka Jana: Kulingana na ripoti kutoka sehemu zote za ulimwengu, kutangaza Mkusanyiko wa Wilaya “Ukombozi Unakaribia!” kulileta matokeo mazuri sana. Mahali pengi, tulisifiwa. Kwa mfano, gazeti moja, kwenye sehemu kubwa ya ukurasa lilisema hivi kuhusu kampanye hiyo: “Ili kukutana na kila mtu kabla ya mkusanyiko wa wilaya kuanza, Mashahidi wamejikaza sana kukutana na jirani zao na wanatembea kwa saa nyingi wakifanya safari ndefu, na kusema kwa haraka.” Katika mji mwingine, ugawanyaji uliopangwa vizuri wa kikaratasi cha mwaliko ulivutia sana watangazaji wa habari, hivi kwamba wakazungumzia sana jambo hilo katika vyombo vya habari. Karibu magazeti matatu yalizungumzia vizuri kazi tuliyofanya mbele ya mkusanyiko wa wilaya kuanza. Mwandishi mmoja wa habari aliandika habari nyingi kwenye kurasa zaidi ya mbili katika habari zinazotangazwa Siku ya Yenga. Gazeti hilo lilizungumzia kwa urefu mambo tunayoamini, undugu wetu, ugawanyaji wa kikaratasi cha mwaliko, na mkusanyiko wa wilaya. Mhubiri mmoja alipotoa kikaratasi hicho cha mwaliko kwenye mlango moja, msikilizaji alimkatiza na kusema, “Ndiyo. Nilikuwa nikisoma kuhusu jambo hilo katika gazeti fulani!” Msikilizaji mwingine alishangaa na kusema hivi: “Nimekuwa nikisoma kuwahusu ninyi, na sasa tazama ninyi mumefika hapa! Je, huo ni mwaliko wangu?” Kisha mwanamke huyo aliongeza, “Hilo ni jambo nzuri sana ambalo Mashahidi wa Yehova wanafanya.”
3 Tuliona watu wengi wenye kupendezwa wakija mahali pa mkusanyiko wakiwa na kikaratasi chao cha mwaliko mkononi. Watu fulani wenye kupendezwa walitoka mbali ili kuja kuhuzuria vipindi vya mkusanyiko. Kwa kuwa tulijikaza sana kualika watu, hilo lilisaidia kuongeza hesabu ya watu waliohuzuria, kwa mfano inchi moja ilikuwa na 27% ya zaidi ya watu waliohuzuria mkusanyiko kwa kulinganisha na mwaka wa 2005.
4 Kuachia Kila Mtu Kikaratasi Katika Eneo: Unaweza kuanza kugawa kikaratasi cha mwaliko majuma matatu mbele ya kuanza mkusanyiko wenu. Tunapaswa kufanya kila tuwezalo ili kuachia kila mtu kikaratasi katika eneo nzima la kutaniko. Katika makutaniko yaliyo na eneo kubwa, juma la mwisho mbele ya mkusanyiko wa wilaya kuanza, wahubiri wanaweza kuacha kikaratasi cha mwaliko kwa wale wasiokuwa nyumbani; wakifanya hivyo bila kuonwa na wapita-njia. Makutaniko yanapaswa kujikaza kugawa vikaratasi vyao vyote na kuachia kila mtu katika eneo kikaratasi, kadiri iwezekanavyo. Karatasi zozote za zaidi zinaweza kutumiwa na mapainia wa kutaniko.
5 Tuseme Nini: Unaweza kusema jambo fulani kama hili: “Ulimwenguni pote tunajikaza kugawa kikaratasi hiki cha mwaliko kuhusu jambo fulani la maana litakalofanyika. Kamata mwaliko wako. Maelezo mengine utayasoma katika mwaliko huu.” Kusema maneno machache kutakusaidia ugawe vikaratasi vingi. Kwa kweli, ikiwa msikilizaji ana maulizo, basi, uyajibu. Mahali ambapo watu wanaonyesha kupendezwa, andika jina na adresi ya mtu na kisha umrudilie haraka iwezekanavyo.
6 Ni jambo la maana kabisa kujikaza kumfuata Kristo! (Yoh. 3:36) Mkusanyiko wetu wa wilaya unaokuja utasaidia watu wote wenye kuhuzuria kutimiza kabisa jambo hilo. Bila shaka, tunatazamia kwamba ushahidi mkubwa utatolewa tena kutokana na kujikaza kwetu sisi wote pamoja ili kutangazia watu Mkusanyiko wa Wilaya, “Mfuate Kristo!” Kwa hiyo, alika kwa bidii watu wengi iwezekanavyo, ili wahuzurie mkusanyiko huo. Yehova na awabariki mnapojikaza kushiriki kwa bidii katika kazi hii yenye umoja ya ulimwenguni pote.