Bidii inayochochea walio wengi.
Mtume Paulo alisifu Wakorintho kwa sababu bidii yao kwa ajili ya kazi nzuri ilikuwa “imechochea walio wengi” wa Wakristo wenzao. (2 Kor. 9:2) Mara nyingi, mtu fulani, familia, kikundi cha funzo la kitabu, au kutaniko zima linaweza kuwa na uvutano huohuo kupitia kushiriki kwao kwa bidii katika kazi ya kueneza evanjeli. Zifuatazo ni njia fulani ambazo katika hizo unaweza kuonyesha bidii kwa ajili ya huduma.
◼ Weka Siku zako za Posho kwa ajili ya utendaji wa Siku ya Magazeti.
◼ Shiriki katika utumishi fulani wa shambani Siku za Yenga.
◼ Shiriki katika siku za pekee zozote zinazopangwa kwa ajili ya kutoa ushahidi.
◼ Tumia likizo kutokana na kazi au shule ili kwenda katika utumishi.
◼ Tegemeza huduma wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko.
◼ Uwe painia msaidizi mwezi mmoja au miezi mingi katika mwaka.
◼ Rekebisha hali zako ili kuwa painia wa kawaida ikiwezekana.
Ona Kitabu-Mwaka 2000 cha Mashahidi wa Yehova, kurasa 17-19.