Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/00 uku. 7
  • Kisanduku cha maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku cha maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kisanduku Cha Maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 5/00 uku. 7

Kisanduku cha maulizo

◼ Wakaribishaji wanaweza kusaidiaje wazazi katika kusaidia watoto wao wadumishe utaratibu wenye kufaa kwenye mikutano?

Kwa kawaida, watoto wana nguvu nyingi, nao hawazoei kukaa kwa vipindi virefu vya wakati. Baada ya mkutano, watoto wana nguvu iliyozuiwa kutenda ambayo inaweza kuwasukuma wakimbie-kimbie au kukimbiza watoto wengine katika Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mikutano, mahali pa kuegeshea magari, au kwenye njia za waendao kwa mguu. Hata hivyo, mithali ifuatayo ni ya kweli: ‘Mutoto anayeachwa kwa yeye mwenyewe atapatia mzazi wake haya.’​​—Mez. 29:15.

Ni jambo la kuhuzunisha kuona kwamba ndugu na dada zetu fulani walio wazee-wazee wameumizwa vikali kwa sababu watoto waliwagonga na kuwaangusha. Hilo limetokeza mateso yasiyofaa na pia gharama isiyohitajika kwa wazazi na kwa kutaniko. Kwa ajili ya usalama wao na ule wa wengine, watoto hawapaswi kuruhusiwa kukimbia-kimbia na kucheza ndani au nje ya Jumba la Ufalme.

Wazazi wanalo daraka la Kimaandiko la kufundisha watoto wao kuheshimu kama inavyofaa mahali petu pa ibada. (Mhu. 5:1a) Kwenye mikutano yetu ya Kikristo, makusanyiko na mikusanyiko, wakaribishaji hupewa mgawo wa kuangalia kwamba “mambo yote yatukie kwa adabu” na kwamba kuweko ‘utaratibu mzuri.’ (1 Kor. 14:40; Kol. 2:5) Wanapaswa kuendelea kuwa waangalifu ndani na nje ya jumba kabla ya programu, wakati hiyo inapoendeshwa, na baadaye. Ikiwa mtoto fulani ni mwenye kukimbia-kimbia au anakuwa asiyetulia, mkaribishaji anaweza kwa upole kumsimamisha na kumweleza kwa nini vitendo kama hivyo havikubaliki. Mzazi wa mtoto huyo pia anapaswa kujulishwa kwa wema kuhusu tatizo na uhitaji wa kuangalia mtoto. Mzazi anapaswa kuitikia ifaavyo.

Inaeleweka kwamba, nyakati nyingine, watoto wachanga sana wanaweza kulia au kuwa wenye kuvuruga mambo wakati wa mikutano. Wakaribishaji, wakifika yapata dakika 20 mbele ya programu kuanza, wanaweza kulinda mistari miwili ya mwisho ya viti mahali wanapokaa wasikilizaji kwa ajili ya wazazi ambao wangetaka kukaa hapo pamoja na watoto wao wadogo. Wengine wetu wanapaswa kushirikiana kwa kuwaachia viti hivyo.

Ikiwa mtoto ni mwenye kutokeza mvurugo, mzazi anapaswa kutenda kwa njia fulani. Ikiwa mzazi hafanyi jambo lolote na kwamba mvurugo unaendelea kukengeusha fikira, mkaribishaji anapaswa kwa wema kuuliza ikiwa mzazi huyo anaweza kumpeleka mtoto nje ya mahali wanapokaa wasikilizaji. Wakati tunapoalika wapya wakiwa na watoto kwenye mikutano, tunapaswa kukaa pamoja nao na kuwasaidia kushughulikia watoto ikiwa hao wanalia au kuvuruga mambo kwa njia nyinginezo.

Ni jambo lenye kutuletea furaha kuona watoto wa umri wote kwenye Jumba la Ufalme na kutazama mwenendo wao mzuri katika nyumba ya Mungu. (1 Tim. 3:​15) Kwa kuheshimu kwao mpango wa Yehova kwa ajili ya ibada, hao humletea heshima na wanathaminiwa na wote katika kutaniko.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine