Kisanduku Cha Maulizo
◼ Namna gani kila mutu anaweza kusaidia ili kufanya mikutano ya kutaniko iendeshwe vizuri na pia wasikilizaji wafuate mafundisho katika hali ya utulivu? (Kum. 31:12)
Ili kuonyesha kwamba tunamheshimu Yehova sana na pia mpango wake wa mikutano ya kutaniko, sisi wote tunatiwa moyo kufika mbele ya wakati kwenye na kuwa tayari kufundishwa naye. Inasaidia sana ikiwa watu wanakaa kwenye viti vya mbele katika Jumba la Ufalme, na kuacha viti vya nyuma kwa ajili ya wale walio na watoto wachanga na wale wanaofika nyuma mara kwa mara. Mbele ya kuanza mikutano, telefone zinapaswa kutiwa katika hali ambayo haitasumbua wasikilizaji. Wasikilizaji wote wanapoonyesha heshima nyingi muda wote wa mikutano, hilo litafanya kusiwe na mambo mengi yenye kuvuruga.—Mhu. 5:1; Flp. 2:4.
Wapya wanapoanza kuhuzuria mikutano, mutu fulani anayefahamiana nao anaweza kuomba akae pamoja nao. Hilo litawasaidia zaidi sana ikiwa wana watoto wachanga ambao wanahitaji kuzoezwa. Kuhuzuria mikutano kunaweza kuwa jambo mpya ambalo inaomba watu wa familia wajizoeleshe. Ikiwa ni hivyo, labda watapenda kukaa kwenye viti vya nyuma ili waepuke kuwazuru wengine inapokuwa lazima wazazi waende inje ili kuwasaidia watoto wao wachanga. (Met. 22:6, 15) Wale walio na watoto wachanga hawapaswi kukaa katika chumba cha pili ambamo watoto wanaweza kuona kwamba humo wanaweza kuchezacheza. Kwa kawaida, ikiwa mzazi anataka kuadibisha (discipliner) mtoto ao kumsaidia kuhusu jambo fulani, ni vizuri zaidi aende naye inje na kisha arudi pamoja naye katika Jumba la Ufalme.
Wakaribishaji wanasaidia ili kuwe hali ya utulivu katika nyumba ya ibada. Wanasaidia familia na wale wanaokuja nyuma mara mojamoja wapate mahali pa kukaa penye kufaa. Wakaribishaji wanapowaomba wengine wakae mahali ambapo hawatakengeushwa, wanapaswa kufanya hivyo kwa adabu na kwa busara. Wanatumia akili nzuri wanaposhugulika na hali zenye kuvuruga ambazo zinatokea bila kutazamia. Mtoto anapokuwa na tabia ya kuvuruga wengine, wakaribishaji wanaweza kutoa msaada kwa njia ya upendo.
Wote wanaokuja kwenye mikutano kwa ajili ya ibada wanaweza kusaidia ili kuwe hali ya utulivu inayowezesha wasikilizaji wajifunze kumhusu Yehova na kusudi lake la kuleta ulimwengu mpya wenye amani na wenye haki.—Ebr. 10:24, 25.