Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/00 uku. 5
  • Iweni waangalifu kwa matamko matakatifu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Iweni waangalifu kwa matamko matakatifu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Sikilizeni na Mwongezewe Elimu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Sikiliza na Ujifunze
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • “Imani Katika Neno La Mungu” —Kusanyiko La Wilaya 1997
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Makusanyiko ya Wilaya 1999 “Neno la Unabii la Mungu”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 5/00 uku. 5

Iweni waangalifu kwa matamko matakatifu

1 Si kila kitu kinachosemwa na mwanadamu kinastahili uangalifu wa pekee. Lakini wakati Mungu anaposema, kuna sababu ya maana sana ya kusikiliza. (Kum. 28:​1, 2) Sisi ni wenye shukrani kuona kwamba waandishi fulani wameandika “maneno yaliyo matakatifu ya Mungu” kwa faida yetu. (Rom. 3:2) Mkusanyiko wa wilaya ujao utatoa nafasi bora za kusikiliza matamko hayo kadiri yanavyosomwa na kuzungumziwa. Unawezaje kuwa mwangalifu kwa njia ya pekee?

2 Fika Mapema Kila Asubuhi: Fikiria msisimuko wa Waisraeli wakati walipoambiwa wakutane na Yehova kwenye Mlima Sinai ili kusikiliza Sheria yake! (Kut. 19:​10, 11, 16-​19) Ikiwa una mtazamo huohuo kuhusu kupokea maagizo ya Yehova kwenye mkusanyiko wa wilaya, utachukua mipango ili kufika mapema kila siku. Hatuwezi kusikiliza programu yote ikiwa tunafika nyuma na kuvuruga wengine kwa jitihada zetu za kupata mahali pa kukaa. Milango itafunguliwa mahali pa mkusanyiko pa saa 2:00 za asubuhi, na programu itaanza pa saa 3:30 kila siku.

3 Hata wengine ambao hufika mapema hawakai ili kungoja mwanzo wa kipindi cha mkusanyiko. Kwa nini hivyo? Wao hungoja mwenye-kiti atoe maneno ya utangulizi ya wimbo ili waache kuongea na marafiki na kuanza kwenda mahali wanapokaa. Tungepaswa kutambua kwamba dakika nyingi kabla ya wimbo wa kufungua kila kipindi cha kusanyiko, mwenye-kiti atakuwa mwenye kukaa jukwaani huku muziki wa Ufalme ukichezwa kuwa utangulizi. Hiyo ndiyo alama yetu ya kuonyesha kwamba wakati wa kukaa umefika! Kisha, wakati utakapofika kwa ajili ya wimbo wa kwanza, tutakuwa tayari kujiunga katika kumwimbia Yehova sifa.

4 Sikilizeni Mkiwa Familia Yenye Kuungana: Wakati matamko matakatifu yaliposomwa kwa Waisraeli wenye kukusanyika, familia, kutia ndani “wadogo,” walipaswa kusikiliza na kujifunza. (Kum. 31:12) Kwenye mikusanyiko yetu, watoto hawapaswi ‘kuachwa kwa wao wenyewe.’ (Mez. 29:15) Wazazi, chukueni mipango ili familia yenu yote ikae pamoja​—kutia ndani matineja. Wazazi wengine hungoja wimbo wa kwanza ili kupeleka watoto wao chooni. Hata hivyo, hilo halitafundisha watoto kwa vyovyote umaana mkubwa wa nyimbo na sala katika ibada yetu. Ni vizuri zaidi kama nini kushughulikia mahitaji ya kwenda chooni mbele ya mwanzo wa kila kipindi cha mkusanyiko, ikiwa inawezekana kwa vyovyote!

5 Ikiwa tunapumzika vya kutosha kila usiku na kuepuka vyakula vizito mchana, hilo litatusaidia kusikiliza. Kaza fikira juu ya yale anayosema msemaji. Usikubali kuacha akili yako itangetange. Fuata katika Biblia wakati maandiko yanaposomwa. Chukua maandishi mafupi. Kadiri kila hotuba inavyokuwa ikitolewa, rudilia akilini mwako yale ambayo msemaji amesema, na ufikirie jinsi utakavyotumia habari hiyo. Mwishoni mwa siku, zungumzieni programu mkiwa familia. Ni nukta gani ambazo kila mmoja alifurahia? Familia yenu inaweza kufanyaje matumizi mazuri ya habari hiyo?

6 Onyesha Heshima kwa Neno la Mungu: Mikusanyiko hututolea nafasi nzuri za kuzungumza na marafiki zetu na kufurahia ushirika wenye kujenga. Kwa kufika mapema, tutakuwa na wakati wa kuongea mbele ya programu kuanza. Ingawa hivyo, wengine hujihusisha katika maongezi wakati programu inapokuwa ikiendeshwa, wakifikiri kimakosa kwamba hilo halikengeushi sana watu mahali wanapokaa wasikilizaji wengi. Hata wakati mikutano inapofanywa mahali pa watu wengi, huo ni wakati wa kusikiliza, kama tu wakati tunapohudhuria mkutano kwenye Jumba la Ufalme. Matumizi ya télécel, kamera ya vidio-kaseti, na kamera ya picha havipaswi kuachwa vikengeushe fikira za watu muda wa programu.

7 Wakati Musa alipokuwa akipokea Sheria kutoka kwa Yehova, yeye “hakula chakula, wala kunywa maji.” (Kut. 34:28) Vivyo hivyo, halingekuwa jambo lenye kufaa kula au kunywa huku vipindi vya mkusanyiko vikiwa vyenye kuendeshwa. Isipokuwa hali kali za afya zinahusika, ngojeni mpaka ‘wakati wenye kufaa’ kwa ajili ya hilo.​​—Mhu. 3:1.

8 Kwenye mikusanyiko fulani, kunaendelea kuwa tatizo kuhusu ndugu na dada wengi na hata watoto wanaotembea kwa vikundi katika vinjia muda wa vipindi vya mkusanyiko. Wakaribishaji watapewa maagizo ili waombe watu hao warudi mahali wasikilizaji wanapokaa. Wenye kujipendea ambao hutumika katika idara mbalimbali wanapaswa kuwa wenye kukaa pamoja na wasikilizaji mara tu kazi yao inapomalizika. Isipokuwa wenye kujipedea wanapewa mgawo wa kufanya kazi ya maana muda wa vipindi vya mkusanyiko, hao wangepaswa kuwa wenye kukaa, wakisikiliza programu. Hawapaswi kuongea huku programu ikiwa yenye kuendeshwa.

9 Hatutaki kuwa ‘wazito katika kusikia kwetu’ wakati tunaposikiliza Neno la Mungu. (Ebr. 5:​11) Kwa hiyo, acheni tuwe wenye kuazimia kuonyesha heshima yenye kufaa kwa kusikiliza kwa uangalifu kadiri matamko matakatifu kutoka kwa Yehova yanavyozungumziwa kwenye mkusanyiko wa wilaya unaokuja.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine