Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 1
  • “Pigana pigano bora la imani”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Pigana pigano bora la imani”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Njia Mbalimbali za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kujikaza Ili Kufanya Mengi Katika Utumishi Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 1

“Pigana pigano bora la imani”

1 Mtume Paulo alimshauri Timotheo ‘apigane pigano bora la imani.’ (1 Tim. 6:12) Paulo mwenyewe aliishi kulingana na maneno hayo. Mwishoni mwa maisha yake, alisema kwa uhakika kwamba yeye binafsi alikuwa amepigana pigano bora. (2 Tim. 4:6-8) Katika kila njia, alifuatia huduma kwa ujasiri, kwa uhodari, na kwa uvumilivu. Kwa kuiga mfano wake, tunaweza kuwa na uhakika huohuo wa ndani kwamba tunafanya yote tuwezayo katika pigano letu kwa ajili ya imani ya Kikristo.

2 Tumia jitihada inayohitajiwa: Paulo alitumika kwa nguvu katika huduma. (1 Kor. 15:10) Nasi tunafanya hivyo kadiri tunavyotafuta ili kupata wale wote wenye kustahili katika eneo letu. (Mt. 10:11) Ili kufikia wengine kati yao, huenda tukalazimika kuamka mapema ili kutoa ushahidi kwa wale tunaokutana nao barabarani. Au huenda tukalazimika kutumika mwishoni mwa kisha mchana-kati au mapema jioni ili kukutana na watu baada ya wao kurudi nyumbani kwao.

3 Inaomba kujitia adabu na kupanga mambo vizuri ili kufika pa saa wakati tunapokutana na kikundi chetu cha funzo la kitabu kwa ajili ya utumishi wa shambani. Kwa mfano, wengine kati ya washiriki wa familia ya Betheli husafiri kwa dakika 60, wanapokwenda au kurudi, ili kushiriki katika huduma miisho-juma pamoja na makutaniko ambayo wamepewa mgawo kushirikiana nayo. Pia, tunaweza kusifu wahubiri na familia nyinginezo katika kutaniko letu ambazo husafiri mwendo wa kutosha lakini wanafika pa saa. Mifano kama hiyo ya bidii yenye kuendelea na upangaji-mambo wa kibinafsi inastahili kuigwa.

4 Tunapaswa kuchochewa kufuatia kupendezwa kote tunakopata. Hata wakati tunapoachia watu magazeti barabarani au kwenye vikao vya vivi-hivi, tunapaswa kufanya jitihada ya kupata anwani au namba ya simu ya kila mmoja wao. Kisha tunaweza kuwatembelea ili kukomaza kupendezwa na kujitahidi kuanzisha funzo la Biblia.

5 Uwe mwenye ukawaida katika utumishi: Paulo alikuwa asiyebadilika-badilika na mwenye kutimiza mambo kikamili katika mahubiri. (Rom. 15:19) Namna gani wewe? Je, unashiriki kikawaida katika huduma? Je, umekwisha kushiriki katika utumishi wa shambani mwezi huu? Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanapendezwa kuona kwamba kila mmoja katika kikundi chao anashiriki katika huduma mnamo Agosti. Watakusaidia kufanya hivyo.

6 Kwa kuiga mfano wa Paulo katika kutegemeza kikamili habari njema, tutaendelea ‘kupigana pigano bora la imani.’

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine