Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/02 uku. 3-4
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • “Tufanye Lililo Jema Kuelekea Wote”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 3/02 uku. 3-4

‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’

1 Katika miaka ya mwisho ya huduma yake yenye bidii, mtume Paulo alitumika kwa ukaribu na Timotheo na Tito. Aliandikia kila mmoja wao maneno ya kitia-moyo yenye kufanana na ya mwenzake. Alimwambia Tito kwamba “wale ambao wameamini Mungu” wanapaswa “kuweka akili zao juu ya kudumisha kazi zilizo bora.” (Tito 3:8) Alimwambia Timotheo kwamba wale wanaoweka tumaini lao juu ya Mungu wanapaswa “kuwa matajiri katika kazi zilizo bora.” (1 Tim. 6:​17, 18) Hilo ni shauri bora kwetu sote! Lakini ni nini kitakachotuchochea tufanye kazi zilizo bora katika maisha yetu? Na ni kazi gani hasa tunazoweza kufanya katika siku zijazo?

2 Kichocheo cha kuwa matajiri katika kazi zilizo sawa kinatokana na imani yetu katika Yehova na upendo wetu kwake; kinatokana pia na tumaini zuri ajabu alilotutolea. (1 Tim. 6:​19; Tito 2:​11) Hasa wakati huu wa mwaka, tunakumbushwa kwamba Yehova alituma Mwana wake duniani ili Yesu atetee Baba yake na kutayarisha njia ya kupata uzima kwa ajili ya wanadamu wote wanaostahili. (Mt. 20:​28; Yn. 3:​16) Hilo litaonyeshwa waziwazi kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho wa kifo cha Kristo mnamo Machi 28. Kwa kuitikia lile tumaini tulilo nalo la kupata uzima wa milele, je, hatuchochewi kufanya yote tuwezayo ili “kuwa matajiri katika kazi zilizo bora”? Bila shaka! Ni kazi gani tunazoweza kufanya sasa?

3 Kazi Bora za Kufanya Mnamo Machi na Baadaye: Bila shaka, tutahudhuria Ukumbusho​—tukio la maana zaidi mwakani kwa Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. (Luka 22:​19) Lakini tunataka kushiriki furaha ya tukio hilo pamoja na watu wengi zaidi iwezekanavyo. Tazama kwenye ripoti ya utumishi katika Annuaire 2002, na utaona kwamba katika nchi nyingi ulimwenguni pote mwaka uliopita, hudhurio kwenye Ukumbusho lilikuwa mara tatu, mara nne, mara tano, au zaidi ya hesabu ya wahubiri. Bila shaka, iliomba jitihada yenye bidii kwa wote katika makutaniko ili kufanya ugawaji mkubwa wa vikaratasi vya mwaliko kwa ajili ya Ukumbusho katika eneo lao lote. Kwa hiyo, tunataka kupitisha wakati mwingi zaidi iwezekanavyo tangu sasa mpaka Machi 28 tukialika watu kwenye Ukumbusho na tukiwasaidia wajifunze kuhusu tumaini la wokovu.

4 Tunawezaje kutumia vizuri hali zetu binafsi zenye kufaa ili kuwa “matajiri katika kazi zilizo bora”? Kwa kuendelea kushiriki kwa shauku katika kazi ya kuhubiri habari njema, tukiwa “wenye bidii kwa kazi zilizo bora.” (Tito 2:​14; Mt. 24:​14) Ikiwa haukuweza kuwa painia msaidizi mnamo Machi, je, unaweza kufanya hivyo mnamo Aprili na/au Mei? Ikiwa unapainia mnamo Machi, je, unaweza kuendelea?

5 Watu fulani wanaofanya kazi ya kimwili wanaona kwamba wanaweza kupitisha saa moja au zaidi katika utumishi wanapokuwa njiani kwenda kazini, wakitoa ushahidi barabarani au wakitembelea watu wanaofanya kazi za biashara zinazoanza mapema asubuhi. Wengine hupanga sehemu ya saa yao ya chakula cha mchana ili kutoa ushahidi. Ndugu na dada fulani wameona kuwa inawezekana kuongoza funzo la Biblia pamoja na mfanyakazi mwenzao katika kipindi hicho. Akina dada wengi walio wake wa nyumbani wamekuwa na uwezo wa kupanga wakati kwa ajili ya huduma ya shambani wakati watoto wao wanapokuwa shuleni. Kwa kuamka mapema zaidi siku fulani ili kushughulikia kazi zao za nyumbani, wana wakati zaidi katika mchana kwa ajili ya kazi ya kuhubiri na kufundisha.​—Efe. 5:​15, 16.

6 Hata ikiwa hauna uwezo wa kuwa painia msaidizi, labda unaweza kufanya programu ya kibinafsi ili kushiriki zaidi katika huduma, ukifanya yote uwezayo ili ‘kufanya mema, kuwa tajiri katika kazi zilizo bora, kuwa mkarimu, tayari kushiriki’ kweli pamoja na wengine.​—1 Tim. 6:​18.

7 Kumbuka ile Kazi Bora ya Kufanya Wanafunzi: Kila mwaka kuna watu wenye kupendezwa wanaokuja kwenye Ukumbusho. Je, itawezekana kwa watu fulani katika kutaniko kutoa uangalifu kwa wale wanaohudhuria lakini ambao hawajifunzi sasa? Je, wanaweza kurudiliwa ili kuwasaidia wafanye maendeleo ya kiroho? Labda wengine kati ya wahudhuriaji hao wa Ukumbusho ni washiriki wa familia za Mashahidi. Labda wengine ni watu waliojifunza wakati uliopita na ambao wanahitaji kitia-moyo fulani tu ili kuanza tena kujifunza na kuhudhuria mikutano kwa ukawaida. Italeta furaha kama nini kuwaona wakiwa watumishi wa Yehova wenye kutenda pamoja nasi!

8 Kwa kushiriki zaidi katika huduma mnamo Machi na baadaye, yaelekea tutapata watu zaidi wenye kupendezwa ambao tunaweza kurudilia. Jaribu kuwaachia ulizo fulani. Kisha, ahidi kwamba utajibu ulizo hilo kwenye ziara yenye kufuata. Tunapofanya hivyo, tutakuwa tumetayarisha njia kwa ajili ya ziara ya kurudia. Ni vizuri kufanya ziara ya kurudia mapema zaidi iwezekanavyo. Ikiwa hatukuweza kuanzisha funzo kwenye ziara ya kwanza, tunataka kujaribu kulianzisha kwenye ziara ile yenye kufuata, ikiwa inawezekana kwa vyovyote.

9 Tunaposhiriki katika kutoa ushahidi barabarani, tunapaswa kuwa na nia ya kujaribu kuanzisha mazungumzo pamoja na watu. Wahubiri wengi wamepewa majina, anwani, na namba za simu kutoka kwa watu wenye kupendezwa waliokutana nao wakati wahubiri hao walipokuwa wakitoa ushahidi barabarani. Ikiwa mtu uliyekutana naye haishi katika eneo lenu, toa habari alizokutolea kwa mwandishi wa kutaniko, ambaye atazitoa kwa kutaniko lililo katika eneo anamoishi mtu huyo. Ikiwa mwandishi hawezi kufanya hivyo, atatuma habari hizo kwa ofisi ya tawi ili hiyo izishughulikie. Katika njia hiyo, kupendezwa kunaweza kukomazwa.

10 Ikiwa unapata namba ya simu badala ya anwani, fanya ziara ya kurudia kwa kumpigia mtu simu. Tayarisha kimbele yale unayotaka kuzungumzia. Uwe na kitabu Kutoa Sababu karibu ili kukiendea kwa uharaka. Ndugu na dada fulani wanapata mafanikio mazuri katika kujifunza na watu kwa njia ya simu, kutia ndani wale ambao walipata shida kukuta nyumbani. Dada mmoja alianza kuomba namba za simu kwa wanawake wenye kupendezwa aliokutana nao katika huduma ya nyumba kwa nyumba, na kama tokeo aliweza kuanzisha mafunzo mawili ya Biblia.

11 Shirikiana na Wazee Katika Kusaidia Wale Wasiotenda: Wazee wanapendezwa sana na kutoa uangalifu wenye upendo kwa watu hao. Hesabu kubwa ya wasiotenda hao wamekwisha kuchukua hatua wenyewe ili kuanza tena kuhudhuria mikutano ya kutaniko. Wanatambua uhitaji wa kutafuta kushirikiana kwa ukaribu na tengenezo la Yehova ili kupata usalama wa kiroho unaofafanuliwa kwenye Zaburi ya 91. Wengine kati ya hao sasa wako tayari kushiriki tena katika utumishi wa shambani. Ikiwa wengine wasiotenda wanahudhuria Ukumbusho mwezi huu, huenda wakakubali kwa furaha kujifunza tena Biblia. Ikiwa ni hivyo, wazee watachukua mipango ili mtu fulani ajifunze na wale wanaotaka msaada. Ikiwa unaombwa kusaidia katika njia hiyo, ushirikiano wako utathaminiwa sana.​—Rom. 15:​1, 2.

12 Endelea “Kudumisha Kazi Zilizo Bora”: Wengi walioshiriki katika kazi ya upainia msaidizi kwa mwezi mmoja au zaidi wameona kwamba utendaji wao shambani uliongezeka katika miezi iliyofuata. Walikutana na watu wenye kupendezwa ambao waliona uhitaji wa kurudilia. Hilo liliwachochea wafanye jitihada ya ziada ili kwenda katika utumishi wa shambani mara nyingi zaidi ili kukutana tena na watu hao wenye kupendezwa. Wengine walianzisha mafunzo ya Biblia, na jambo hilo liliwasaidia kushiriki zaidi katika huduma.

13 Na bado wengine walipata furaha kubwa sana katika kufanya zaidi katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi hivi kwamba walichochewa wafikirie mambo wanayotanguliza. Kama tokeo, wengine waliweza kupunguza wakati wanaopitisha katika kazi ya kimwili ili waendelee kuwa mapainia wasaidizi. Wengine wameweza kuingia katika utumishi wa painia wa kawaida. Waliweza kuweka tumaini lao kikamili zaidi juu ya Mungu, wala si juu ya vitu ambavyo ulimwengu huu unaweza kutoa. Waliona kwamba “kuwa wakarimu, tayari kushiriki” kulileta baraka tele kutoka kwa Yehova na kuliimarisha tumaini lao la kufurahia “uhai ulio halisi.” (1 Tim. 6:​18, 19) Bila shaka, wengine zaidi wanapoanza utumishi wa painia, kutaniko zima linafaidika. Mapainia wana mwelekeo wa kusema juu ya mambo waliyojionea na kualika wengine washiriki katika huduma pamoja nao, na jambo hilo linatokeza hali ya kiroho yenye kuinuliwa katika kutaniko.

14 Acheni sote ‘tuwe matajiri katika kazi zilizo bora’ katika majira haya ya Ukumbusho na baadaye kwa kuongeza ushiriki wetu katika huduma ya Kikristo. Acheni tuonyeshe uthamini wetu kuhusu yale ambayo Yehova amefanya kwa kututolea tumaini la kuishi milele katika dunia mpya yenye uadilifu.​—2 Pet. 3:​13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine