Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/02 uku. 3
  • “Tufanye Lililo Jema Kuelekea Wote”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Tufanye Lililo Jema Kuelekea Wote”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Aprili—wakati wa ‘kufanya kazi kwa bidii na kujitahidi’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 4/02 uku. 3

“Tufanye Lililo Jema Kuelekea Wote”

1 ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’ na ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’ ndivyo vichwa vya habari vilivyotumiwa katika nyongeza za Februari na Machi 2002 za Huduma Yetu ya Ufalme. (Kol. 1:​25; 1 Tim. 6:​18) Katika matoleo hayo tulitiwa moyo tufanye jitihada ya ziada ili kusaidia wale wenye kupendezwa wahudhurie Ukumbusho, kusaidia wale wasiotenda washiriki tena katika utendaji wa kutaniko, na kusaidia watoto wetu na wanafunzi wa Biblia wenye kustahili waanze kutangaza habari njema. Bila shaka, tumefurahia mafanikio fulani yaliyotokana na jitihada zetu zenye bidii. Sasa, “maadamu tuna wakati wenye kufaa kwa ajili ya hilo, acheni sisi [tuendelee kufanya] lililo jema kuelekea wote.”​—Gal. 6:​10.

2 Tuwaalike Wahudhurie Tena: Katika eneo la tawi letu, zaidi ya watu 450,000 wasio wahubiri wa habari njema huhudhuria Ukumbusho kila mwaka. Kwa sababu kuwako kwao kunaonyesha kwamba wanapendezwa kwa kiasi fulani, tunapaswa kufanya nini ili kuchochea wale ‘walio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uhai udumuo milele’ ili wawe “waamini”? (Mdo. 13:​48) Watieni moyo warudi kwenye mikutano ya kutaniko mapema zaidi iwezekanavyo.

3 Kwa nini usialike mtu mwenye kupendezwa ahudhurie Funzo la Kitabu la Kutaniko ili afurahie mazungumzo yenye kupendeza ya unabii wa Isaya? Ikiwa wewe ni mshiriki wa familia ya mtu huyo au ikiwa unajuana naye na kwamba unapangwa kutoa hotuba wakati ujao kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, unaweza kumwalika aje na kusikiliza hotuba yako. Endelea kumjulisha kuhusu vichwa vya hotuba za watu wote zitakazotolewa majuma yenye kuja. (Programu ya kisasa inapaswa kuwekwa kwenye ubao wa matangazo.) Tafuta nafasi yoyote ya kuamsha ndani ya mtu huyo tamaa ya kumwabudu Yehova. Na bila shaka, ikiwa hajaanza kujifunza Biblia na mtu fulani katika kutaniko, unaweza kwa wema kumtolea funzo.

4 Tuendelee Kutia Moyo Wale Wasiotenda: Hesabu fulani ya wale wanaohudhuria Ukumbusho wamekwisha kujiweka wakfu kwa Yehova. Lakini, kufikia hatua fulani waliacha kuhubiri habari njema kwa njia yenye kutenda. Na bado, Paulo anatuhimiza “tufanye lililo jema . . . hasa kuelekea wale ambao katika imani ni jamaa zetu.” (Gal. 6:​10) Kwa hiyo, wale wasiotenda wanapaswa kuhangaikiwa kwanza kabisa.

5 Labda wengine wamekwisha kuitikia kitia-moyo cha wazee na wengine cha kushiriki tena katika huduma. Ikiwa wazee wanakutolea mgawo wa kutumika na mtu aliyesaidiwa awe mhubiri mwenye kutenda tena, jua kwamba upendo wako mwenyewe kwa Yehova na kwa huduma ya shambani utajenga uhakika ndani ya mtu huyo. Mwonyeshe jinsi unavyoshiriki katika sehemu mbalimbali za huduma ili aweze kupata furaha katika hiyo, ili aendelee na kazi ya kuhubiri, na apate baraka za Yehova.

6 Tuwape Wahubiri Wapya Mwanzo Mzuri: Wakati mwanamke mmoja aliyeanza kupendezwa karibuni alipotambua kwamba alikuwa amepata tengenezo la kweli la Mungu, alitaka kuanza utumishi papo hapo. Baada ya kusikia kilichotakiwa kwake, akasema: “Acheni tushughulikie jambo hilo mara moja.” Ikiwa mtu fulani ambaye umekuwa ukijifunza Biblia pamoja naye anakubaliwa kuanza kushiriki katika utumishi wa shambani, msaidie aone uhitaji wa ‘kushughulikia jambo hilo mara moja,’ na hivyo umsaidie aanze vizuri. Msaidie asitawishe zoea la kujitayarisha kwa ajili ya huduma ya shambani na kuishiriki kwa ukawaida kila juma.

7 Ikiwa ni mtoto wako mwenyewe ndiye amekuwa mhubiri asiyebatizwa, tumika naye ili afanye maendeleo kulingana na umri na uwezo wake. Kwa msaada kidogo kutoka kwako, anaweza kukushangaza unapoona jinsi anavyoweza kuhusisha mtu fulani kwa matokeo katika mazungumzo, kusoma maandiko ya Biblia, na kutolea watu vichapo. Anapopata mtu mwenye kuitikia vizuri katika utumishi wa shambani, msaidie afanye ziara ya kurudia na kufuatia kupendezwa.

8 Tupanue Utumishi Wetu Wenyewe: Je, hali zako zinakuruhusu kuongeza ushiriki wako katika kazi ya kueneza evanjeli hata baada ya majira ya Ukumbusho? Je, unaweza kuongeza saa moja au mbili kila juma juu ya wakati unaopitisha kwa kawaida katika utumishi? Je, unatazamia kwenye kalenda wakati ambapo unaweza kuwa painia msaidizi tena? Au je, unaweza kupanga maisha yako ili kuingia katika huduma ya wakati wote? Jitihada yote tunayofanya katika huduma inaweza kusaidia mtu fulani akubali kweli! (Mdo. 8:​26-​39) Kadiri tunavyotazamia siku zinazokuja, acheni ‘sikuzote tufuatie lililo jema kuelekea mtu na mwenzake na kwa wengine wote.’​—1 Thes. 5:​15.

[Picture on page 3]

Tuendelee Kusaidia

[Picture on page 3]

□✔ Wahudhuriaji wa Ukumbusho

□✔ Wahubiri waliosaidiwa wawe wenye kutenda tena

□✔ Wahubiri wapya wasiobatizwa

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine