Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/01 uku. 8
  • Shabaha Ni Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Shabaha Ni Nini?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuwaongoze Wanafunzi Kwenye Tengenezo La Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Saidieni wengine wahudhurie mikutano
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 10/01 uku. 8

Shabaha Ni Nini?

1 Kwa nini tunaongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani? Je, ni kwa kusudi pekee la kutoa ujuzi, kufanya maisha ya watu yawe bora, au kuwafanya waone wakati ujao kwa njia nyangavu zaidi? Hapana. Shabaha yetu kuu ni kufanya wanafunzi wa Yesu Kristo! (Mt. 28:19; Mdo. 14:21) Kwa sababu hiyo, wale tunaojifunza nao wanahitaji kushirikiana na kutaniko. Maendeleo yao ya kiroho yanahusiana moja kwa moja na uthamini wao kuelekea tengenezo la Kikristo.

2 Jinsi ya Kufikia Shabaha Hiyo: Tangu mwanzo kabisa na kwa kuendelea, himiza mwanafunzi ahudhurie mikutano ya kutaniko. (Ebr. 10:​24, 25) Eleza jinsi mikutano hiyo itakavyotia imani yake nguvu, msaidie afanye mapenzi ya Mungu, na umwezeshe ashirikiane ifaavyo na wengine wanaotamani kumsifu Yehova. (Zab. 27:13; 32:8; 35:18) Maneno yako mwenyewe yenye kuonyesha upendo na uthamini kuelekea kutaniko na mikutano yatachochea tamaa yake ya kuhudhuria.

3 Wapya wanahitaji kufahamu kwamba tengenezo la Yehova ni undugu wa kimataifa. Waonyesheni vidio Les Témoins de Jéhovah : un nom, une organisation na Ushirika Wetu Wote wa Ndugu (Kiing.). Wasaidieni waone kwamba Yehova anatumia mamilioni ya watu waliojiweka wakfu ili kutimiza mapenzi yake ulimwenguni pote. Julisheni wapya hao kwamba wao pia wanaalikwa wamtumikie Mungu.​​—Isa. 2:​2, 3.

4 Ni jambo lenye kufurahisha sana kuona mtu anayejifunza Biblia akiwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu. Hiyo ndiyo shabaha yetu!​​—3 Yn. 4. 

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine