Shabaha Ni Nini?
1 Kwa nini tunaongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani? Je, ni kwa kusudi pekee la kutoa ujuzi, kufanya maisha ya watu yawe bora, au kuwafanya waone wakati ujao kwa njia nyangavu zaidi? Hapana. Shabaha yetu kuu ni kufanya wanafunzi wa Yesu Kristo! (Mt. 28:19; Mdo. 14:21) Kwa sababu hiyo, wale tunaojifunza nao wanahitaji kushirikiana na kutaniko. Maendeleo yao ya kiroho yanahusiana moja kwa moja na uthamini wao kuelekea tengenezo la Kikristo.
2 Jinsi ya Kufikia Shabaha Hiyo: Tangu mwanzo kabisa na kwa kuendelea, himiza mwanafunzi ahudhurie mikutano ya kutaniko. (Ebr. 10:24, 25) Eleza jinsi mikutano hiyo itakavyotia imani yake nguvu, msaidie afanye mapenzi ya Mungu, na umwezeshe ashirikiane ifaavyo na wengine wanaotamani kumsifu Yehova. (Zab. 27:13; 32:8; 35:18) Maneno yako mwenyewe yenye kuonyesha upendo na uthamini kuelekea kutaniko na mikutano yatachochea tamaa yake ya kuhudhuria.
3 Wapya wanahitaji kufahamu kwamba tengenezo la Yehova ni undugu wa kimataifa. Waonyesheni vidio Les Témoins de Jéhovah : un nom, une organisation na Ushirika Wetu Wote wa Ndugu (Kiing.). Wasaidieni waone kwamba Yehova anatumia mamilioni ya watu waliojiweka wakfu ili kutimiza mapenzi yake ulimwenguni pote. Julisheni wapya hao kwamba wao pia wanaalikwa wamtumikie Mungu.—Isa. 2:2, 3.
4 Ni jambo lenye kufurahisha sana kuona mtu anayejifunza Biblia akiwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu. Hiyo ndiyo shabaha yetu!—3 Yn. 4.