Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Wakati huu wa mwaka, watu wengi wanafikiri kuhusu Yesu Kristo, iwe kwamba wanamwamini au hawamwamini. Wengine husema kwamba hakuwa mtu halisi. Maoni yako ni gani? [Baada ya kusikia jibu, soma Mathayo 16:15, 16.] Nina hakika utafurahi kusoma makala hii kuhusu ‘Yesu Halisi’ ili kuona jinsi alivyo na uvutano juu yako leo na jinsi atakavyokuwa na uvutano juu yako wakati ujao.”
Amkeni! Des. 22
“Je, hautakubali kwamba ili kufanya maisha yawe salama, tunahitaji chakula kisicho na hatari na chenye kutegemeka? [Acha mtu ajibu.] Ona kile ambacho Mungu aliahidi watu wake katika nyakati za kibiblia. [Soma Walawi 26:4, 5.] Amkeni! inazungumzia wasiwasi iliyopo leo kuhusu chakula chetu. Inaonyesha pia wakati ambapo Mungu atatutolea usalama ulimwenguni pote.”
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Je, unajiuliza kwa nini watu fulani wanaonekana kuwa na maisha mepesi huku wengine wakishindana ili kupata riziki? Biblia inazungumzia jambo hilo [Soma Yobu 34:19.] Maelezo yanatolewa katika gazeti hili ili kuonyesha jinsi Mungu anavyokusudia kumaliza tofauti za tabaka.”
Amkeni! Jan. 8
“Sisi sote tunajua kuhusu msiba huu uliotikisa ulimwengu. Tangu wakati huo, watu wamehitaji faraja na msaada kwa kiasi kikubwa. Makala hii inaeleza, kati ya mambo mengine, yale ambayo Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakifanya ili kusaidia waokokaji, wafanyakazi wanaoshughulikia hali zinazoomba kutenda haraka, na wale waliofiwa.”