Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Jan. 15
“Watu wengi hutumia sanamu katika ibada yao. Je, unafikiri kwamba vitu hivyo vina uwezo wa kuokoa? [Acha mtu ajibu.] Tafadhali ona yale ambayo Mungu wa kweli atafanya kwa ajili yetu. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Mungu aliye halisi tu ndiye anayeweza kutimiza jambo hilo. Gazeti hili linaonyesha yeye ni nani na jinsi tunavyoweza kufaidika kwa kumtumaini yeye.”
Amkeni! Jan. 22
“Huenda tukaona kuwa jambo la kawaida kuwa na nyumba. Lakini mamilioni ya wakimbizi ulimwenguni pote huzurura-zurura bila msaada, nao hawapati kamwe usalama wanaoutafuta. Amkeni! huchunguza sababu ya kuwako kwa tatizo hilo na pia ahadi ya Biblia kwamba siku fulani kila mmoja atakuwa na nyumba yake mwenyewe.”
MNARA WA MLINZI Feb. 1
“Kuna hangaiko kubwa kuhusu uchafuzi wa mazingira. Lakini, je, umekwisha kufikiria uchafuzi wa akili? [Acha mtu ajibu.] Biblia inakazia umaana wa kuwa safi kimwili na kiroho. [Soma 2 Wakorintho 7:1.] Nina hakika kwamba utaona habari hii kuwa yenye kusaidia na yenye kufaa.”
Amkeni! Feb. 8
“Bila shaka umeona kwamba ingawa ndoa nyingi huwa na mwanzo wenye furaha, nyingi huvunjika. Ningetaka kukuachia toleo hili la Amkeni!, kwa kuwa linazungumzia maoni ya Biblia kuhusu jinsi ya kufanya ndoa iwe yenye kudumu na yenye furaha.”