Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/02 uku. 1
  • Kazi ya Kuhubiri Ufalme Inasaidia Kuokoa Uhai!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kazi ya Kuhubiri Ufalme Inasaidia Kuokoa Uhai!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Tuendelee Kutambua Uhitaji Wa Kutenda Kwa Haraka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tuhubiri Tukiwa Wenye Kutambua Uhitaji wa Kutenda kwa Haraka!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • “Fulizeni kuwa macho”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 4/02 uku. 1

Kazi ya Kuhubiri Ufalme Inasaidia Kuokoa Uhai!

1 Hiyo ndiyo kazi ya maana zaidi inayofanyika katika ulimwengu kwa wakati huu. Yehova Mungu, Yesu Kristo, na makumi ya maelfu ya malaika wanaikazia uangalifu. Ni nini hiyo, na sababu gani ni ya maana sana? Ni kazi ya kuhubiri Ufalme, nayo inasaidia kuokoa uhai!​—Rom. 1:​16; 10:​13, 14.

2 Huenda watu fulani wakafikiri kwamba tungalisaidia wengine kwa njia bora zaidi ikiwa tungejaribu kuutengeneza ulimwengu unaotuzunguka. Wengi wanajishughulisha kabisa katika jitihada za kufikia amani, kuponya magonjwa, au kutengeneza uchumi. Lakini ni nini litakalowasaidia watu zaidi?

3 Kazi ya Maana Sana: Ujumbe wa Ufalme peke yake hueleza kusudi la uhai, sababu ya kuteseka kwa wanadamu, na tumaini pekee lenye kutegemeka kuhusu wakati ujao. Habari njema huwezesha watu kuwa marafiki za Yehova na hivyo kupokea “amani ya Mungu izidiyo fikira yote.” (Flp. 4:7) Ni ujumbe wa Ufalme pekee ndio unaotoa uongozi wenye kufaa ili kusaidia watu washindane na matatizo ya maisha sasa, na unaoeleza jinsi ya kuhifadhiwa ulimwengu mbovu utakapoharibiwa wakati ujao. (1 Yn. 2:​17) Je, kazi ya kuhubiri Ufalme haistahili kufanyiwa jitihada zote?

4 Tutoe mfano: Ni nini njia bora zaidi ya kusaidia kijiji ambacho wakaaji wacho wanalala usingizi na ambacho kinahatarishwa na maji ambayo karibuni yatabomoa kizuizi kilichojengwa ili kuyazuia? Kutoa na kutupa maji kutoka kizuizi kinachokuwa dhaifu? Kupamba kijiji kinachoangamia? Sivyo! Ni lazima wakaaji wa kijiji waamshwe, waonywe kuhusu msiba unaokaribia, na wasaidiwe kuponyoka! Wale wanaolala usingizi kiroho leo wamo katika hatari kubwa. (Luka 21:​34-​36) Kwa kuwa mfumo huu wa mambo utapitilia mbali karibuni, acheni tujitahidi kwa uharaka zaidi iwezekanavyo kuhubiria wote tuwezao kuhubiria!​—2 Tim. 4:2; 2 Pet. 3:​11, 12

5 Shikamana Nayo: Acheni tutafute njia za kuwafikia hata watu wengi zaidi ambao ni wanyofu kuelekea habari njema​—nyumbani kwao, barabarani, kwa njia ya simu, na kivivi-hivi. Kazi ambayo Yehova ametupatia tufanye ndiyo kazi ya maana zaidi tunayoweza kufanya. Ikiwa tunaitimiza kwa bidii, ‘tutajiokoa sisi wenyewe na wale wanaotusikiliza pia.’​—1 Tim. 4:​16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine