Kisanduku Cha Maulizo
◼ Kwa nini kuna uhitaji wa kuwa waangalifu tunapotoa ushahidi kwa njia ya barua?
Kutoa ushahidi kupitia barua kumeonekana kwa muda mrefu kuwa njia yenye matokeo ya kushiriki habari njema. Hata hivyo, matukio ya ulimwengu ya karibuni yamefanya watu wawe waangalifu kuhusu kufungua barua wasizozijua. Bahasha kutoka vyanzo visivyojulikana au zisizo na anwani ya mtu aliyeziandika mara nyingi zinatiliwa mashaka, hasa ikiwa zimeandikwa kwa mkono na ikiwa ni nzito. Huenda wenye nyumba wakatupa barua ya aina hiyo bila kuifungua. Tunawezaje kuzuia jambo hilo lisitukie?
Ikiwezekana, barua na bahasha zinapaswa kuandikwa kwa mashini. Bahasha inapaswa kutumwa kwa mwenye nyumba kwa kutumia jina lake. Usiitume kwa “Mkaaji.” Zaidi ya hilo, toa sikuzote anwani ya kutumia ili kukurudishia jibu. Ikiwa si jambo lenye busara kuonyesha anwani yako binafsi, andika jina lako na anwani ya Jumba la Ufalme. Usitume barua bila kuonyesha jina lako. Usitumie kamwe anwani ya ofisi ya tawi.—Ona Majibu kwa Maulizo Yenu katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 1996.
Mapendekezo zaidi na barua ya mfano vinaweza kupatikana katika kitabu Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ukurasa wa 84-90. Miongozo hiyo itatusaidia kutumia barua kwa matokeo ili kufikisha habari njema kwa wengine.