Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Kuhusu nini tunapaswa kuwa wangalifu tunapowaandikia barua watu ambao hatufikii kuwakuta nyumbani kwao?
Kwa sababu zilizo nyingi, tunaona kwamba ni vigumu zaidi na zaidi kuwakuta watu nyumbani kwao. Wahubiri fulani wanaona kuwa jambo lenye kufaa kuwaandikia, na namna hiyo ya kutenda inaweza kutokeza matokeo mazuri; hata hivyo, ni jambo la lazima kukumbusha nukta fulani ambazo zitatuepusha na matatizo:
Tusitumie anwani ya Sosaiti. Jambo hilo lingeweza kufanya watu wafikiri kimakosa kwamba barua inatoka kwenye maofisi yetu, lingeweza kuzusha magumu na kuna hatari lisababishe gharama zisizofaa.
Tuwe hakika kwamba anwani ya mtu tunayetumia barua ni sahihi na kwamba fedha za tikiti ya posta ni za kutosha.
Tusitume barua kwa mtu fulani bila kuonyesha jina lake. Tusiache barua milangoni.
Barua fupi ni bora zaidi. Badala ya kuandika habari ndefu isiyo na mwisho, tutie trakti au gazeti pamoja na barua.
Barua zilizoandikwa kwa mashini ni rahisi zaidi kusomeka na zinavutia vizuri.
Barua haihesabiwi kuwa ziara ya kurudia isipokuwa tuwe tulikuwa tumekwisha kumtolea ushuhuda kibinafsi mtu tunayemtumia barua.
Ikiwa tunaandikia mtu ambaye tayari ameonyesha kupendezwa, tungepaswa kuonyesha anwani au namba ya simu ambayo kupitia hiyo anaweza kuongea nasi. Tufasirie programu yetu ya masomo ya kibiblia.
Tumwalike mtu kwenye mikutano ya kutaniko, kwa kuonyesha wazi anwani na programu ya mikutano.
Tusitume tena barua kwa watu wasiokuwako baada ya kurudisha eneo; ni mhubiri ambaye amepewa sasa eneo hilo ndiye anapaswa kuhubiri ndani.