Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/02 uku. 7
  • Itikio Lenye Shauku!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Itikio Lenye Shauku!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Chagua Marafiki Wako kwa Hekima
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Video Inayostahili Kufikiriwa Sana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Je, Unajitahidi Kusoma na Kuandika?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Ufanye Angalisho na Marafiki Wabaya Katika Siku Hizi za Mwisho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 10/02 uku. 7

Itikio Lenye Shauku!

1 Familia za Kikristo mahali pote zimeonyesha shukrani zao zenye shauku kwa ajili ya vidio Les jeunes s’interrogent... Comment se faire de vrais amis ? Baba mmoja katika Shirikisho la Amerika alisema kwamba baada ya kuitazama wana wake walikaa kimya—walielewa kila jambo katika vidio hiyo na waliitikia ifaavyo! Ripoti kutoka Malawi inasema kwamba ndugu na dada vijana wa huko waliielewa na kuitikia ifaavyo kwa kuwa wanapatwa na mikazo hiyohiyo kutoka kwa wenzao shuleni. Baba mmoja katika Ujerumani alisema hivi kuhusu vidio hiyo: “Ninaona hiyo kuwa jibu kwa sala zangu.” Kijana mmoja alisema: “Asante kwa kunikumbusha kwamba Yehova ananijali.” Mzee mmoja katika New Zealand aliripoti: “Ilisaidia mmoja wa vijana wetu arudi kwenye njia inayoongoza kwenye uzima.” Mwanamke mmoja aliyeolewa aliitazama na kusema: “Ningependa sana kila kijana katika kweli atazame vidio hii na kusukumwa afanye ukweli uwe mali yake!” Familia, kwa nini msiitazame tena? Baadaye, zungumzieni pamoja maulizo yafuatayo.

2 Utangulizi: Urafiki wa kweli ni nini?—Mez. 18:24.

3 Mambo Yanayozuia Urafiki: Unawezaje kushinda hisia ya kujisikia unatengwa? (Flp. 2:4) Kwa nini unapaswa kuwa na nia ya kuboresha utu wako, na ni nani anayeweza kukusaidia ufanye hivyo? Ni nini kitakachotokeza nafasi za kupata marafiki zaidi, na hao wanaweza kupatikana wapi?—2 Kor. 6:13.

4 Urafiki Pamoja na Mungu: Unawezaje kusitawisha uhusiano pamoja na Yehova, na kwa nini ni jambo linalostahili kufanyiwa jitihada? (Zab. 34:8) Ni nani anayeweza kwa njia bora zaidi kutia nguvu urafiki wako pamoja na Mungu?

5 Aina Mbaya ya Marafiki: Ni nani walio mashirika mabaya? (1 Kor. 15:33) Marafiki wabaya wanawezaje kuongoza mtu kwenye angamizo la kiroho? Simulizi la Biblia kuhusu Dina linakufundisha nini?—Mwa. 34:1, 2, 7, 19.

6 Drama ya Ki-Siku-Hizi: Upweke ulikuwa na uvutano gani juu ya Tara? Aliteteaje ushirika wake na vijana wa kilimwengu? Vijana hao walimweka katika hatari gani? Kwa nini wazazi wake walishindwa kuona hatari aliyokuwa ndani yake, lakini walimsaidia arudilie hali njema ya kiroho wakiwa na mtazamo gani? Dada mmoja painia alionekanaje kuwa rafiki wa kweli wa Tara? Kwa nini Wakristo wanapaswa kutii Mezali 13:20 na Yeremia 17:9? Ni somo gani la maana ambalo Tara alijifunza?

7 Maneno ya Kumalizia: Umejifunza masomo gani kutokana na vidio hii? Unawezaje kuitumia ili kusaidia wengine?—Zab. 71:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine