Kisanduku Cha Maulizo
◼ Tunapotoa ushahidi kwa njia ya simu, je, tunapaswa kueleza mpango wa kutoa michango?
Tunapotoa ushahidi moja kwa moja, inawezekana kueleza kwamba kazi ya ulimwenguni pote ya elimu ya kibiblia ya Mashahidi wa Yehova inategemezwa kikamili na michango ya kujipendea na kwamba tunafurahi kupokea michango kama hiyo. Lakini, hatupaswi kusema kuhusu michango au mpango wa kutoa michango tunapotoa ushahidi kwa njia ya simu, kwa kuwa hilo linaweza kufikiriwa vibaya kuwa namna ya kuombaomba kupitia simu. Huduma ya Mashahidi wa Yehova si ya kibiashara kwa njia yoyote ile.—2 Kor. 2:17.
◼ Tunapotoa ushahidi kwa njia ya simu, tunapaswa kufanya nini ikiwa mtu fulani anaomba Mashahidi wa Yehova wasimpigie simu tena?
Mapenzi ya mtu huyo yanapaswa kuheshimiwa. Maandishi yaliyo na tarehe na jina la mtu yanapaswa kutiwa katika bahasha ya eneo ili wahubiri waepuke kuita namba hiyo wakati ujao. Mara moja katika mwaka, orodha ya watu walioomba tusiwapigie simu inapaswa kuchunguzwa upya. Chini ya uongozi wa mwangalizi wa utumishi, wahubiri wenye uzoefu na wenye busara wanaweza kupewa mgawo wa kutembelea watu hao ili kujua jinsi wanavyohisi sasa.—Ona Majibu kwa Maulizo Yenu katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1994.