Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Julai 15
“Wengi wametambua mwelekeo unaoongezeka wa watu kujitenga. Je, unafikiri kwamba huo ni mwendo wa hekima? [Acha mtu ajibu.] Ona maneno haya yenye hekima kuhusu thamani ya kushirikiana na wengine. [Soma Mhubiri 4:9, 10.] Gazeti hili linazungumzia kwa nini sisi sote tunahitaji wengine na jinsi tatizo la kujitenga linavyoweza kutatuliwa.”
Amkeni! Julai 22
“Watu wengi wana wasiwasi kwa sababu ya kuenea kwa ponografia. Je, unafikiri kwamba hilo ni jambo la kuhangaikiwa? [Acha mtu ajibu.] Shauri lenye kufaa linalopatikana katika Biblia linaweza kutulinda. [Soma Waefeso 5:3, 4.] Gazeti hili linaonyesha jinsi tunavyoweza kujilinda tusipatwe na hatari hiyo yenye kudhuru hatua kwa hatua.”
MNARA WA MLINZI Agosti 1
“Je, ulijua kwamba kulingana na ripoti moja, zaidi ya asilimia 50 ya hesabu ya watu ulimwenguni wana pato la chini ya dola 2 kwa siku? Je, unafikiri kwamba jambo fulani linaweza kufanywa ili kutatua jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linaonyesha jinsi umaskini utakavyotatuliwa kwa njia yenye kudumu, kama inavyoonyeshwa katika Biblia.”—Soma Zaburi 72:12, 13, 16.
Amkeni! Agosti 8
“Katika miaka ya karibuni, misiba iliyosababishwa na hali-hewa imeharibu vitu kotekote ulimwenguni. Unafikiri ni nini kinachoweza kufanywa ili kupunguza taabu inayosabishwa na hali hiyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia tatizo la hali za hewa zinazobadilika-badilika na suluhisho linaloonyeshwa katika Biblia.—Soma Isaya 35:1.