Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago. 15
“Tunapenda kujua maoni yako kuhusu jambo fulani ambalo Yesu alisema. [Soma Mathayo 5:5.] Wakati ambapo ahadi hii itatimia, unafikiri kwamba hali duniani zitakuwa kama zilivyo leo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha kupitia Biblia jinsi Yesu atabadilisha dunia. Linazungumzia pia nani watakaoriti dunia.”
Amkeni! Ago.
“Je, unafikiri kwamba tutapata kuona tena wapendwa wetu waliokufa? [Acha mtu ajibu.] Ona ahadi ya Yesu kuhusu wafu. [Soma Yohana 5:28, 29.] Habari hii inaeleza wazo la Biblia kuhusu jambo linalotupata tunapokufa.” Kazia habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Watu wengi leo hawapendezwi na dini. Je, unafikiri kwamba kuwa mtu wa dini kunasaidia mtu awe mtu mzuri zaidi? [Acha mtu ajibu.] Ona jambo ambalo Biblia ilitabiri kuhusu yale ambayo watu watakuwa wakitafuta katika dini siku za mwisho. [Soma 2 Timotheo 4:3, 4.] Gazeti hili linazungumzia jinsi ibada ya kweli inavyomletea Mungu heshima na jinsi inavyotuletea faida.”
Amkeni! Sept.
“Watu wengi wanajiuliza ikiwa kumwamini Mungu kunapatana na sayansi. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waebrania 3:4.] Amkeni! hii ya pekee inazungumzia sababu ambazo zimeongoza wanasayansi fulani waamini kwamba kuna Muumba.”