Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/07/07
“Watu tunaowapenda wanapokufa, tunakuwa wenye huzuni sana. Je, unafikiri kwamba kuna sehemu fulani ya mwili wao inayoendelea kuishi? [Acha mtu ajibu.] Yesu alitoa ahadi hii yenye kutia moyo. [Soma Yohana 5:28, 29.] Kwa kuwa Yesu alisema kwamba ufufuo ‘unakuja,’ gazeti hili kupitia Biblia, linaeleza mahali ambapo wafu wanapatikana kwa sasa.”
Amkeni! Mwezi wa 7
“Watu wengi wanajikaza kuishi maisha yanayowafanya waonekana kuwa watu wema na wanafikiri kwamba ni jambo la maana kuwa mtu mwema. Je, hayo ndiyo maoni yako kuhusu maisha? [Acha mtu ajibu.] Ona hatari iliyoko ikiwa namna yetu ya kufikiri kuhusu kuwa mtu mwema ni tofauti na namna Mungu anavyofikiri. [Soma Methali 14:12.] Gazeti hili linafasiria maana ya kuwa mtu mwema machoni pa Mungu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi 01/08/07
“Ningependa kujua mawazo yako kuhusu jambo fulani alilosema Yesu. [Soma Mathayo 5:3.] Je, unafikiri kwamba kuwa na hali nzuri ya kiroho ni jambo la maana ili kuwa na furaha? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali nzuri ya kiroho na jinsi tunavyoweza kuipata.”
Amkeni! Mwezi wa 8
“Unafikiri wazazi wanaweza kupata wapi mashauri yatakayowasaidia kabisa kulea watoto wao? [Acha mtu ajibu.] Ona ahadi ambayo Biblia inatutolea. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyoweza kusaidia wazazi walee watoto wenye furaha.”