Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/07/08
“Je, unafikiri inawezekana watu wafanye urafiki wa karibu pamoja na Mungu Mweza Yote? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Matendo 17:27.] Habari hii inaeleza kwa nini tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu anataka tumkaribie.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Amkeni! Mwezi wa 7
“Viburudisho vingi vya leo vinaonyesha kwamba watu wanaendelea kupendezwa na mambo ya uchawi. Je, unafikiri kwamba kujihusisha katika mambo ya uchawi hakuna hatari? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12.] Habari hii inaonyesha maoni ya Biblia kuhusu hatari zilizo katika mambo ya uchawi.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/08/08
“Kwa kuwa hali ya mazingira ni yenye kuharibika, watu wengi wana mashaka juu ya wakati ujao wa dunia. Unafikiri nini kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 37:11.] Gazeti hili linazungumzia sababu fulani zilizo katika Biblia zinazotutolea tumaini kuhusu wakati ujao wa dunia.”
Amkeni! Mwezi wa 8
“Watu wengi wanasadiki kwamba kuongezeka kwa joto kunafanya maisha yawe katika hatari hapa duniani. Kwa maoni yako, jambo hilo litakwisha namna gani? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Isaya 11:9.] Gazeti hili linaeleza kwa nini hakuna shaka kwamba dunia itaendelea kukaliwa na wanadamu.”