Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/08/08
“Je, unakubali kwamba kutii amri hii ya Yesu kunaweza kuongeza furaha katika familia? [Soma Yohana 13:34. Acha mtu ajibu.] Habari hii inaonyesha jinsi mafundisho na mfano ambao Yesu alituwekea vinahusu kila mshiriki wa familia.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 16 na 17.
Amkeni! Mwezi wa 8
“Je, unafikiri kwamba serikali za wanadamu zinaweza kushugulikia vizuri joto ya dunia? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yeremia 10:23.] Utafurahia habari hii. Inazungumzia jinsi Mungu atamaliza matatizo yote yanayotia dunia yetu katika hatari.”
Mnara wa Mlinzi 01/09/08
“Watu wengi wanajua vizuri maneno ya Yesu yaliyo kwenye Mathayo 6:9. [Soma.] Hata hivyo, wengi wanaona kwamba ni vigumu kumkaribia Mungu kama Baba. Unafikiri tunaweza kumkaribia Mungu namna gani? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia sifa mbalimbali za Baba yetu wa mbinguni na jinsi tunaweza kumjua kabisa.”
Amkeni! Mwezi wa 9
“Kwa muda wa miaka mingi, watu wamekuwa na maoni tofauti tofauti kuhusu uzima kisha kifo. Wewe unawaza nini? [Acha mtu ajibu.] Ona jambo ambalo Ayubu aliamini. [Soma Ayubu 14:14, 15.] Habari hizi zinazungumzia maoni ya Biblia kuhusu uzima kisha kifo.”