Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Agosti 15
“Unafikiri ni nini iliyo aina ya juu zaidi ya uaminifu-mshikamanifu? [Acha mtu ajibu.] Makala hii inakazia uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu wa kweli. [Onyesha ukurasa wa 5, na usome 2 Samweli 22:26.] Je, unajua kwamba uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu unaweza kuzuia watu wasitendee wengine katika njia ya kukosa upendo? Ninajua utafurahi kusoma kuhusu jambo hilo.”
Amkeni! Agosti 22
“Je, umepata kuwa na wasiwasi kuona kwamba tatizo la uchafuzi unaofanywa na mwanadamu halizuiwi? [Acha mtu ajibu.] Sababu kubwa inayotokeza tatizo hilo ni akili ya uharibifu. Yesu alifundisha wafuasi wake kutokuwa waharibifu. [Soma Yohana 6:12.] Gazeti hili linaonyesha jinsi kufuata kanuni za Biblia kunavyosaidia familia ziepuke akili ya kutupa-tupa vitu.”
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Je, umetambua kwamba mahali pengi majirani hawajuani kama ilivyokuwa zamani? [Acha mtu ajibu.] Yesu alisema kanuni ambayo ni ya maana sana ili kuwa jirani mwema. [Soma Mathayo 7:12.] Makala hizi zinaonyesha jinsi tunavyoweza kuwa majirani wema na kutia wengine moyo wafanye hivyohivyo.”
Amkeni! Sept. 8
“Kwa watu wengi leo, maisha yanajaa na wasiwasi. [Soma Mhubiri 9:11.] Uongozi wenye kutegemeka unaweza kupatikana wapi? [Acha mtu ajibu.] Watu fulani wanaendea watu wanaojifunza maana ya kifumbo ya hesabu. Je, hiyo ndiyo njia ambayo kwa hiyo mambo yatakayokupata yanaweza kufunuliwa? Unaweza kupata wapi habari yenye kutegemeka kuhusu wakati ujao? Amkeni! inajibu maulizo hayo.”