Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Agosti 15
“Watu wengi wanathamini sifa nzuri. Wengine wanajiuliza hata jinsi watakavyokumbukwa baada ya wao kufa. Je, umekwisha kufikiria jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mhubiri 7:1.] Gazeti Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi tunavyoweza kujifanyia jina zuri pamoja na watu na Mungu.”
Amkeni! Agosti 22
“Ikiwa wewe au mshiriki wa familia yako amekwisha kutendewa kikatili, unajua jinsi jambo hilo linavyotaabisha. [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linatoa mapendekezo yenye kufaa kwa wale wanaotendewa kikatili. Linazungumzia pia ahadi ya Mungu ya wakati ambapo maisha yatakapokuwa bila matatizo hayo.” Soma Mika 4:4.
MNARA WA MLINZI Sept. 1
“Watu wengi wanafikiri kwamba dini mbalimbali za wanadamu ni barabara tofauti tu zinazoongoza kwenye lengo lilelile moja. Wengine wanafikiri kwamba kuna imani moja tu ya kweli. Je, umekwisha kujiuliza kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mfano moja wa zamani unaotusaidia kupata jibu kwa ulizo hilo.” Zungumzia mambo makuu ya Mathayo 13:24-30.
Amkeni! Sept. 8
“Kufuatia mitindo kuna uvutano wenye nguvu juu ya maisha ya watu wengi leo. Watu fulani wanafikiri kwamba mkazo mwingi unatiwa juu ya mavazi na sura ya nje. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu.] Gazeti Amkeni! linatoa maoni yanayosawazika kuhusu mtindo.” Soma Wakolosai 3:12.