Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 15
“Je, unafikiri kwamba bado tutaiona serikali itakayomaliza matatizo ya wanadamu? [Acha mtu ajibu.] Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali kwa ajili ya serikali kama hiyo katika Mathayo 6:9, 10. [Soma.] Gazeti hili linazungumzia kwa nini Ufalme wa Mungu unashinda serikali za wanadamu na linazungumzia baraka ambazo serikali hiyo italetea wanadamu.”
Amkeni! Julai
Unapokutana na kijana, unaweza kusema: “Vijana wengi wa miaka yako wanafikiria kuoa. Unafikiri ni wapi unaweza kupata habari yenye kutegemeka kuhusu mambo ya ndoa? [Acha mtu ajibu.] Ona yule aliyeanzisha mpango wa ndoa. [Soma Mathayo 19:6.] Gazeti hili linazungumzia kanuni fulani za Biblia zinazoweza kutusaidia ili kuwa na ndoa yenye furaha.”
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Ni jambo la kawaida leo kuona watu wakiwatesa wengine. Je, unafikiri kwamba mambo yangebadilika ikiwa watu wengi zaidi wangetumia maneno haya ya Yesu? [Soma Mathayo 7:12. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia wazo la Biblia lenye kuonyesha jinsi mwanadamu atakavyopata tena haki yake ya kuheshimiwa.”
Amkeni! Ago.
“Sisi wote tunahangaikia matunzo ya afya yetu. Je, unajua kwamba madaktari wengi leo wanasita kutia wagonjwa damu mishipani? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa sababu. Linazungumzia pia wazo la Biblia lenye kuonyesha kwa nini Mungu anaiona damu kuwa kitu cha bei sana.” Soma Walawi 17:11.