Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/08/07
“Ningependa kujua wazo lako kuhusu jambo linalosemwa katika andiko hili. [Soma Waebrania 3:4.] Je, unakubali kwamba ulimwengu uliumbwa na Muumba mwenye akili? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia ikiwa kuamini kwamba kuna Muumba kunapatana na sayansi ya kweli.”
Amkeni! Mwezi wa 8
Unapokutana na kijana, unaweza kusema hivi: “Vijana wengi wa miaka yako wameumizwa wakati wengine wanapowateta . Je, hilo limekwisha kukufikia? [Acha kijana ajibu.] Biblia inatoa shauri nzuri ambalo linaweza kutusaidia ikiwa tunaumizwa wakati watu wengine wanapotuteta. Inaonyesha pia jinsi tunavyoweza kujiepusha kuteta watu wengine.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12, na soma andiko moja kati ya yale yaliyo katika habari hiyo.
Mnara wa Mlinzi 01/09/07
“Watu wengi wanafikiri kwamba ‘Agano la Kale’ linatoa habari ya kihistoria yenye kusaidia. Lakini wanajiuliza ikiwa mashauri yake ni yenye kufaa leo. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waroma 15:4.] Gazeti hili linaonyesha jinsi ‘Agano la Kale’ linavyotoa mashauri yenye faida kuhusu maisha ya kila siku na tumaini la kweli kuhusu wakati ujao.”
Amkeni! Mwezi wa 9
“Je, unafikiri kwamba ni Mungu ndiye anayetokeza misiba? [Acha mtu ajibu. Kisha Soma Kumbukumbu la Torati 32:4.] Gazeti hili linazungumzia kwa nini Mungu ameruhusu misiba itokee. Linaeleza pia jinsi ya kulinda familia yako.”