Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Nov. 15
“Wakati uliopita, wengi waliamini kwamba siku moja dunia ingekuwa paradiso. Leo, watu fulani wanashakia ikiwa hata itaokoka. Maoni yako ni nini kuhusu wakati ujao wa dunia? [Acha mtu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo. [Soma Zaburi 37:11.] Gazeti hili linazungumzia zaidi yale ambayo Biblia inatabiri kuhusu dunia.”
Amkeni! Nov. 22
“Watu fulani wana wasiwasi kwamba mazingira yameharibiwa sana hivi kwamba hayawezi tena kutengenezwa. Je, unafikiri kwamba hali hiyo inatuacha bila tumaini? [Acha mtu ajibu.] Muumba hakukusudia dunia iwe mahali pa kutupia takataka pasipoweza kukaliwa. [Soma Isaya 45:18.] Gazeti hili linaeleza jinsi dunia itakavyookolewa.”
MNARA WA MLINZI Des. 1
“Watu fulani leo wanapoteza imani katika Mungu. Sababu moja ya hilo ni kwamba hawawezi kupata majibu yanayotosheleza kwa maulizo yanayowasumbua kama haya. [Toa mfano kutoka katika kisanduku kwenye ukurasa wa 6.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia njia moja ya maana ya kujenga imani ya kweli katika Mungu.” Soma Wafilipi 1:9.
Amkeni! Des. 8
“Je, unafikiri kwamba wanadamu watafurahia wakati wowote hali kama zile zinazofafanuliwa hapa? [Soma Isaya 14:7. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili lina habari zenye kufaa zinazoweza kutufaidi tunapongojea utimizo wa ahadi za Mungu.” Onyesha makala “Unawezaje Kushinda Tamaa Mbaya?”