Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Watu wengi wanajiuliza kwa nini matatizo yanayowapiga wanadamu yanazidi kuendelea, na hayapunguki. Je, umekwisha kufikiria yale ambayo andiko hili linasema kuwa labda ndiyo sababu? [Soma Ufunuo 12:9. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mipango ya Ibilisi ya kupotosha watu na jinsi tunavyoweza kupinga uvutano wake.”
Amkeni! Nov. 22
“Ingawa kuna chakula cha kutosha ili kulisha kila mtu duniani, kuna watu karibu milioni 800 ambao wanakosa chakula. Je, jambo hilo si lenye kuhuzunisha? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia tatizo kubwa la kulisha watu katika miji. Linazungumzia pia ahadi ya Biblia kuhusu ulimwengu usio na njaa.” Soma Zaburi 72:16a.
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Watu wanaposikia neno ‘Har-magedoni,’ wengi wanaona uharibifu mkubwa wenye kuogopesha. [Onyesha kisanduku kwenye ukurasa 3.] Je, wewe ungeshangaa kujua kwamba kwa kweli Har-magedoni ni moja ya mambo bora zaidi ambayo yangeweza kutupata? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza kwa nini ni hivyo.” Soma 2 Petro 3:13.
Amkeni! Des. 8
“Nilipenda kukueleza kuhusu wakati kila mtu atakapokuwa na mahali penye kufaa pa kuishi. Je, si jambo lenye kusikitisha kuona kwamba watu wengi hawana makao? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Isaya 65:21, 22.] Gazeti hili linazungumzia sababu za ukosefu wa makao. Linaeleza pia jinsi Mungu atakavyotimiza ahadi ambayo tumesoma.”