Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/11/06
“Kwa sababu ya uovu mwingi sana ulio duniani, watu fulani wanajiuliza: ‘Kwa nini nijisumbue sana kufanya yaliyo mema?’ Je, umekwisha kufikiri hivyo? [Acha mtu ajibu.] Ona maneno haya yenye kutia moyo. [Soma Methali 2:21, 22.] Gazeti hili linafasiria sababu kubwa zaidi ya kufanya mambo yaliyo mema.”
Amkeni! Mwezi wa 11
“Watu fulani wanafikiri kwamba Mungu ndiye chanzo cha kila jambo lenye kutokea. Wakati msiba fulani unapotokea, wanasema kwamba kunapaswa kuwa sababu fulani ya maana iliyomfanya Mungu atokeze msiba huo. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yakobo 1:13.] Gazeti hili linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu sababu ya mateso na yale ambayo Mungu anafanya ili kuyamaliza.”
Mnara wa Mlinzi 1/12/06
“Je, unafikiri kwamba unabii huu wa Biblia ni wenye kutimia leo? [Soma Mathayo 24:11. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mafundisho fulani yenye kukubaliwa na watu wengi. Linaonyesha pia lile tunaloweza kufanya ili tusidanganywe na walimu wa uongo.”
Amkeni! Mwezi wa 12
“Unaweza kumtaja nani kuwa ndiye mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi? [Acha mtu ajibu.] Wengi wanamtaja Yesu kuwa ndiye mtu mkuu zaidi. Ona yale ambayo atafanya kwa ajili ya dunia akiwa Mtawala wa Ufalme wa Mungu. [Onyesha picha kwenye ukurasa wa 8-9 na soma andiko moja kati ya maandiko yenye kuonyeshwa.] Gazeti hili linazungumzia namna gani na wakati gani Yesu atatimiza mambo hayo.”