Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/11/07
“Sisi wote tunapenda kuwa na maisha yenye furaha na yenye kusudi. Je, unakubaliana na maneno ambayo Yesu alisema hapa kuhusu siri ya kupata furaha? [Soma Mathayo 5:3. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza jinsi kutosheleza tamaa yetu kubwa ya kumwabudu Mungu, tamaa ambayo tulizaliwa nayo, kunavyoweza kufanya maisha yetu yawe na kusudi.”
Amkeni! Mwezi wa 11
“Katika wakati wetu huu wa sayansi na wa mashaka, watu wengi wanafikiri kwamba Biblia ni kitabu cha zamani ambacho hakina tena maana leo. Unafikiri nini kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Je, unajua kwamba kila andiko la Biblia lenye kuhusu mambo ya sayansi ni la kweli? [Soma Ayubu 26:7.] Amkeni! hii ya pekee inatoa sababu zenye kusadikisha zinazotufanya tutegemee Biblia.”
Mnara wa Mlinzi 01/12/07
“Namna gani unaweza kujibu ulizo hili? [Soma ulizo kwenye jalada. Kisha acha mtu ajibu.] Mungu ana kusudi la kuunganisha wanadamu wote. [Soma Zaburi 46:8, 9.] Gazeti hili linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu jinsi wanadamu wote watakavyounganishwa.”
Amkeni! Mwezi wa 12
“Watu fulani wanafikiri kwamba kifo si mwisho wa maisha; wengine wanaamini kwamba kifo ni mwisho wa maisha. Je, wewe unafikiri kwamba tunapaswa kuogopa kifo? [Acha mtu ajibu.] Ona jinsi Ayubu alifikiri kuhusu kifo chake. [Soma Ayubu 14:14, 15.] Gazeti hili linatoa maoni ya Biblia yaliyo wazi kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa.”