Tuendelee na Bidii Yetu Katika Kazi ya Kuhubiri
1 Kuanzia mwaka wa 1992, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wametumia kwa bidii zaidi ya saa bilioni moja (1,000,000,000) kila mwaka katika kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. Sisi ni wenye furaha kabisa kwa mchango wetu mdogo tuliotoa katika utimizo huo wa ajabu.—Mt. 28:19, 20.
2 Bila shaka, shukrani na sifa zote zimuendee Yehova, ambaye ametutegemeza katika kazi yetu ya kuhubiri katika hizi “nyakati za hatari.” (2 Tim. 3:1) Inaomba tufanye nini ili kuendelea kushiriki kwa bidii katika kazi hii ya maana?
3 Jambo Linalochochea Bidii Yetu: Upendo mwingi kwa Mungu na kwa jirani, na pia tamaa yenye kutoka moyoni ya kuishi kulingana na wakfu wetu, vinatuchochea tuwe na bidii katika kazi ya Ufalme. (Mt. 22:37-39; 1 Yoh. 5:3) Upendo unatuchochea tujinyime mambo fulani ili tuweze kushiriki sana katika kazi ya kuhubiri.—Luka 9:23.
4 Tufanye Nguvu Ili Kulinda Bidii Yetu: Adui yetu Ibilisi, anatumia nguvu zake zote ili kupunguza bidii yetu kwa ajili ya mahubiri. Hali ya ubaridi ya watu wa eneo letu, mambo ya ulimwengu yenye kukengeusha, mikazo ya maisha ya kila siku, na kuhangaikia hali yetu ya afya inayoendelea kuhabirika ni kati ya mambo ambayo anatumia ili kujaribu kutuvunja moyo.
5 Kwa hiyo, tunapaswa kufanya nguvu ili kuendelea kuwa na bidii. Ni jambo la maana kwetu kuendelea na ‘upendo tuliokuwa nao mwanzoni.’ Hilo linatia ndani kusoma kwa ukawaida Neno la Mungu Biblia na kufikiri sana juu ya yale tunayosoma, na kufaidika na mipango yote ya kiroho ambayo “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” anatutolea.—Ufu. 2:4; Mt. 24:45; Zab. 119:97.
6 Kama unabii mbalimbali wa Biblia unavyoonyesha waziwazi, Siku ya Yehova ya kuwaharibu wale wasiomwogopa inakaribia sana. (2 Pet. 2:3; 3:10) Tukijua vizuri jambo hilo, na tujikaze kuendelea kuwa na bidii tukishiriki sana katika kazi ya ulimwenguni pote ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi, kazi inayozidi kuendelea leo!