Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Je, haukubali kwamba ni vigumu kulea watoto katika ulimwengu wa sasa? [Acha mtu ajibu.] Angalia uhakika huu kwamba wazazi wanaweza kufanikiwa. [Soma Methali 22:6.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linatoa shauri linalofaa ili kusaidia wazazi washinde tatizo hilo.”
Amkeni! Juni 22
“Watu fulani wanafikiri kwamba kuamini Mungu ni kinyume na sayansi. Lakini ulijua kwamba kuna wanasayansi wanaosema kwamba kwa kweli sayansi inaunga mkono imani katika Muumba? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia uhakikisho fulani uliowafanya wafikie kusema hivyo.” Soma Waroma 1:20.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Wakati wa msiba, wengi wanajiuliza ikiwa kweli Mungu anajali watu na kuona mateso yao. Je, umekwisha kujiuliza kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu anavyotuhangaikia leo na jinsi ambavyo ametoa msingi wa kuondoa mateso yote.” Soma Yohana 3:16.
Amkeni! Julai 8
“Kwa watu wengi, miaka ya ujana ni wakati wa furaha na wa magumu, je, unakubaliana na hilo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mabadiliko ambayo vijana wanapitia. Linazungumzia pia mashauri fulani yenye hekima yanayoweza kuwasaidia wafanye miaka yao ya ujana kuwa wakati bora zaidi.” Soma Mhubiri 12:1.