Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Je, umekwisha kujiuliza ikiwa mambo ambayo wanadamu wanafanya duniani yanaweza kugusa hisia za Mungu? [Acha mtu ajibu.] Ona jinsi matendo yetu yanavyoweza kugusa hisia za Mungu. [Soma Methali 27:11.] Gazeti hili linazungumzia mifano fulani ya watu waliofurahisha moyo wa Mungu, na linaeleza jinsi tunavyoweza kufanya hivyohivyo.”
Amkeni! Mei 22
“Sayansi ya kiganga imefanya maendeleo makubwa katika kupiganisha magonjwa, lakini, je, unafikiri kwamba tutapata kuona ulimwengu usio na magonjwa yoyote? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza kwamba siku moja kila mtu duniani atafurahia afya kamilifu katika utimizo wa ahadi hii.” Soma Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Watu fulani wanafikiri kwamba si lazima kuwa sehemu ya dini fulani ili kumwabudu Mungu. Je, umekwisha kujiuliza kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu alivyoshughulika na watu nyakati zilizopita. Linazungumzia pia maana ya kumwabudu Mungu katika kweli.” Soma Yohana 4:24.
Amkeni! Juni 8
“Watu wengi leo wanapatwa na upweke. Hilo linahusisha kujisikia wenye kutengwa na wengine. Je, unakubali kwamba jambo hilo linaweza kuumiza moyoni? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 25:16.] Toleo hili la Amkeni! linatoa mapendekezo yanayofaa ili kupiganisha upweke.”