Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Je, haufikiri kwamba ingefurahisha kuishi chini ya hali zinazoelezwa katika andiko hili lililoongozwa na roho ya Mungu? [Soma 2 Petro 3:13. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linafasiria ni nini mbingu mpya na dunia mpya. Linaeleza pia jinsi maisha yatakavyokuwa mazuri wakati Mungu atakapotimiza kusudi lake kuhusu dunia.”
Amkeni! Mei
“Watu wengine wanafikiri kwamba ili kufanikiwa katika ulimwengu wa leo, ni lazima mtu awe mkali. Tofauti na hilo, ona jambo ambalo Yesu alisema. [Soma Mathayo 5:5, 9.] Je, unakubaliana na hilo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha faida tatu ambazo mtu anaweza kupata kwa sababu ya kuwa mwenye kufanya amani.” Kazia habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Wakati uliopita katika desturi za watu wengi, wazee walitendewa kwa heshima. Sheria hii ya zamani inaonyesha jambo hilo. [Soma Walawi 19:32.] Je, unafikiri kwamba leo wazee wanaendelea kuheshimiwa? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu anavyowahangaikia wazee na jinsi sisi pia tunavyoweza kufanya hivyo.”
Amkeni! Juni
“Ugaidi (mauaji na mashambulizi yanayofanywa kwa ajili ya kufikia makusudi fulani ya kisiasa) si jambo jipya. Leo ugaidi umeenea ulimwenguni pote, jambo hilo linamwogopesha kila mtu. Wewe unafikiri ni kwa nini mambo yanakuwa hivyo? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia mawazo ya Biblia yenye kuonyesha wakati gani ugaidi utakwisha na jinsi Mungu atakavyoleta amani ya kweli katika dunia.” Soma Mika 4:4.