Utoaji Mbalimbali
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 6
“Sisi wote tumekwisha kufiwa na watu wa jamaa ao marafiki. Je, unatumaini kwamba unaweza kuwaona tena? [Acha mutu ajibu.] Ona wazo hili lenye kufariji.” Soma na kuzungumzia habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 wa Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 6 na andiko moja kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Umtolee mutu gazeti na ufanye mpango wa kumrudilia ili kujibu ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/06/11
“Wengi kati yetu wanateseka sana ili kupata chakula, na wengine hawana hata vitu vya lazima maishani. Je, unafikiri kwamba kutakuwa wakati ambapo hakutakuwa mutu aliye maskini? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Zaburi 9:18.] Gazeti hili linazungumzia sababu inayoleta umaskini na yale Biblia inasema kuhusu jinsi tatizo hilo litakavyokwisha.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Ugaidi (terrorisme) ni tatizo ambalo limeenea ulimwenguni pote. Unafikiri sababu ni gani? [Acha mutu ajibu.] Maneno haya ya Biblia yanatutolea tumaini. [Soma Zaburi 72:7, 14.] Gazeti hili linazungumzia sababu fulani zinazofanya kuwe ugaidi na linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu jinsi gani na wakati gani ugaidi utakwisha.”