Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 6
“Karibu kila mutu tunayezungumuza naye anataka kuwe amani duniani. Lakini, vita zinaendelea. Wewe unawaza sababu gani ni vigumu kupata amani duniani?” Acha mutu ajibu. Kisha umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 6, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja iliyo hapo. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Tangazo: Kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri wa tarehe 1 Mwezi wa 6, munapaswa kufanya onyesho kuhusu namna ya kuanzisha mafunzo ya Biblia mukitumia pendekezo lililo hapa juu.
Munara wa Mulinzi 01/06/13
“Tunatembelea watu ili kuzungumuzia kwa muda mufupi tatizo linalohusu watu wote. Watu wengi wamekwisha kutambua kwamba wengine wanawachukia. Unawaza kuna mahali fulani duniani ambapo hakuna chuki? [Acha mutu ajibu.] Ona namna Mungu anavyowaona watu wote. [Soma Matendo 10:34.] Gazeti hili linazungumuzia namna Mungu ataondoa chuki milele.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Tungetaka kujua maoni yako juu ya jambo fulani. Kwa kawaida kila mutu anataka kuwa na maisha mazuri. Unawaza tunaweza kuwa na maisha mazuri kwa kununua vitu vingi zaidi? [Acha mutu ajibu.] Ona maneno ya Yesu yenye hekima. [Soma Luka 12:15.] Gazeti hili linatoa maoni yenye kusawazika kuhusu vitu vya kimwili na linatoa mapendekezo yanayoweza kutusaidia tutumie feza vizuri.”